Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu
Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.
عَنْ أبي Ø¹ÙŽØ¨Ù’Ø¯Ù Ø§Ù„Ù„Ù‡Ù Ø§Ù„Ù†Ù‘ÙØ¹Ù’مَان٠بْن٠بَشÙير٠رَضÙÙŠÙŽ الله٠عَنْهÙما قَالَ : سمعت٠رَسÙولَ الله٠صلى الله عليه وسلم ÙŠÙŽÙ‚ÙولÙ: ((إن الْØÙŽÙ„الَ بَيّÙÙ†ÙŒ وَإنَّ الْØÙŽØ±ÙŽØ§Ù…ÙŽ بَيّÙÙ†ÙŒ وَبَيْنَهÙما أمورٌ Ù…ÙØ´Ù’تَبÙهَاتٌ لا يَعْلَمÙÙ‡Ùنَّ ÙƒÙŽØ«ÙŠÙØ±ÙŒ Ù…ÙÙ†ÙŽ Ø§Ù„Ù†Ø§Ø³ÙØŒ Ùَمَن٠اتَّقَى Ø§Ù„Ø´Ù‘ÙØ¨Ùهَات٠Ùَقَد اسْتَبْرَأَ Ù„ÙØ¯ÙينÙÙ‡Ù ÙˆÙŽØ¹ÙØ±Ù’ضÙÙ‡ÙØŒ وَمَنْ وَقَعَ ÙÙŠ الشَّبÙهات٠وَقَعَ ÙÙŠ الْØÙŽØ±ÙŽØ§Ù…ÙØŒ كالرَّاعÙÙŠ يَرْعَى ØÙŽÙˆÙ’Ù„ÙŽ الْØÙÙ…ÙŽÙ‰ ÙŠÙوشÙك٠أَنْ يَرْتَعَ ÙÙÙŠÙ‡ÙØŒ أَلا وَإنَّ Ù„ÙÙƒÙلّ٠مَلÙÙƒÙ ØÙمىً أَلا وَإنَّ ØÙÙ…ÙŽÙ‰ الله Ù…ÙŽØÙŽØ§Ø±ÙÙ…Ùه، أَلا وَإنَّ ÙÙŠ Ø§Ù„Ø¬ÙŽØ³ÙŽØ¯Ù Ù…ÙØ¶Ù’غَةً إذَا صَلَØÙŽØªÙ’ صَلَØÙŽ Ø§Ù„Ù’Ø¬ÙŽØ³ÙŽØ¯Ù ÙƒÙلّÙه٠وإذَا Ùَسَدَتْ Ùَسَدَ الْجَسَد٠كÙلّÙÙ‡ÙØŒ أَلا ÙˆÙŽÙ‡ÙÙŠÙŽ الْقَلْبÙ)) Ø±ÙŽÙˆÙŽØ§Ù‡Ù Ø§Ù„Ù’Ø¨ÙØ®ÙŽØ§Ø±ÙÙŠÙ‘Ù ÙˆÙŽÙ…ÙØ³Ù’Ù„ÙÙ…ÙŒ
Imepokelewa kutoka kwa Abuu ‘Abdillaah An-Nu’umaan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye alisema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Hakika halaal imebainika na haraam imebainika na baina ya mawili hayo mna yenye kutia shaka. Wengi miongoni mwa watu hawayajui. Basi atakayejiepusha yenye kutia shaka, atakuwa amejiepushia shaka katika Dini yake na heshima yake.
Na Atakayetumbukia katika yenye kutia shaka, ataingia kwenye haraam. Kama mchunga anayechunga kando ya mipaka, ni haraka kulisha humo (mpaka mwingine wa watu). Zindukeni! Kila mfalme ana mipaka. Zindukeni! Kwa yakini mipaka ya Allaah ni haraam Alizoziharamisha.
Zindukeni! Kwa yakini katika mwili mna kinofu cha nyama, kinapokuwa salama, mwili wote unakuwa salama. Kinapoharibika, mwili wote unaharibika. Zindukeni! Kinofu hicho ni moyo.” [Al-Bukhaariy na Muslim]
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
AL-ARBAUWN AN-NAWAWIYYAH HADITHI YA 4: Uumbwaji wa mwanadamu
HAdithi hii itakufundisha namna ambavyo mwanadamu anapitia hatuwa mbalumbali tumboni mwa mama yake
Soma Zaidi...