Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu

Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.

 Ø¹ÙŽÙ†Ù’ أبي عَبْدِ اللهِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُما قَالَ : سمعتُ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ:  ((إن الْحَلالَ بَيِّنٌ وَإنَّ الْحَرَامَ بَيِّنٌ وَبَيْنَهُما أمورٌ مُشْتَبِهَاتٌ لا يَعْلَمُهُنَّ كَثيِرٌ مِنَ الناسِ، فَمَنِ اتَّقَى الشُّبُهَاتِ فَقَد اسْتَبْرَأَ لِدِينِهِ وَعِرْضِهِ، وَمَنْ وَقَعَ في الشَّبُهاتِ وَقَعَ في الْحَرَامِ، كالرَّاعِي يَرْعَى حَوْلَ الْحِمَى يُوشِكُ أَنْ يَرْتَعَ فِيهِ، أَلا وَإنَّ لِكُلِّ مَلِكٍ حِمىً أَلا وَإنَّ حِمَى الله مَحَارِمُه، أَلا وَإنَّ في الجَسَدِ مُضْغَةً إذَا صَلَحَتْ صَلَحَ الْجَسَدُ كُلُّهُ وإذَا فَسَدَتْ فَسَدَ الْجَسَدُ كُلُّهُ، أَلا وَهِيَ الْقَلْبُ))  رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ  وَمُسْلِمٌ

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu  ‘Abdillaah An-Nu’umaan bin  Bashiyr  (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye alisema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Hakika halaal imebainika na haraam imebainika na baina ya mawili hayo mna yenye kutia shaka. Wengi miongoni mwa watu hawayajui. Basi atakayejiepusha yenye kutia shaka, atakuwa amejiepushia shaka katika Dini yake na heshima yake. 

 

Na Atakayetumbukia katika yenye kutia shaka, ataingia kwenye haraam. Kama mchunga anayechunga kando ya mipaka, ni haraka kulisha humo (mpaka mwingine wa watu). Zindukeni!  Kila mfalme ana mipaka. Zindukeni! Kwa yakini mipaka ya Allaah ni haraam Alizoziharamisha. 

 

Zindukeni! Kwa yakini katika mwili mna kinofu cha nyama, kinapokuwa salama, mwili wote unakuwa salama. Kinapoharibika, mwili wote unaharibika. Zindukeni! Kinofu hicho ni moyo.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 543

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

AL-ARBAUWN AN-NAWAWIYYAH HADITHI YA 4: Uumbwaji wa mwanadamu

HAdithi hii itakufundisha namna ambavyo mwanadamu anapitia hatuwa mbalumbali tumboni mwa mama yake

Soma Zaidi...
Zijuwe nyakati ambazo ukiomba dua hujibiwa kwa urahisi

Post hii inakwenda kukugundisha ni nyakati zipi ambazo Allah hukubali dua kwa urahisi.

Soma Zaidi...
Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w

Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari.

Soma Zaidi...
Dua za kuomba wakati unapokuwa na maumivu kwenye mwili

Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako.

Soma Zaidi...
Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo

Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi.

Soma Zaidi...
SWALA YA MTUME (s.a.w)

SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s.

Soma Zaidi...