picha

HISTORIANA MAISHA YA MTUME ISA(A.S)

Nabii Isa(a.

HISTORIANA MAISHA YA MTUME ISA(A.S)

HISTORIA YA MTUME ISA(A.S)


Nabii Isa(a.s) huitwa “Yesu”, na “Jesus” katika Biblia ya Kiswahili na Kiingereza. Majina yote hayo matatu yanamkusudia mwana wa Maryamu aliyezaliwa bila baba, ambaye ni Mtume wa mwisho kwa Bani Israil.


Nasaba na kuzaliwa Nabii Isa(a.s)


Nabii Isa(a.s) ni mtoto wa Maryamu aliyekuwa mwana wa Imraani. Kizazi cha Imraani kilichaguliwa na Allah(s.w) kupewa Utume kama tunavyofahamishwa:


Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adamu na Nuhu na kizazi cha
Ibrahiimu na kizazi cha Imraani juu ya walimwengu wote(3:33)


Kuzaliwa Maryamu, Mama wa Nabii Isa(a.s)


Mke wa Imraani aliweka nadhiri kwa Allah(s.w) kuwa mtoto atakayemzaa atamuweka wakfu. Alitarajia kuwa atazaa mtoto wa kiume.



Aliposema mke wa Imraani: “Mola wangu! Nimeweka nadhiri kwako aliye tumboni mwangu kuwa wakfu, basi nikubalie, bila shaka Wewe ndiye usikiaye na ujuaye.(3:35)



Basi alipomzaa alisema: “Mola wangu! Nimezaa mwanamke”- Na Mwenyezi Mungu anajua sana aliyemzaa -”Na mwanaume si sawa na mwanamke. Na nimempa jina Maryam. nami namkinga kwako, yeye na kizazi chake, uwalinde na shetani aliyewekwa mbali na rehema zako (3:36)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 4364

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 web hosting     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni

“Na (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza.

Soma Zaidi...
Makubaliano ya Mkataba wa Al Fudhul

Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 13. Hapa utajifunza historia ya Mkataba wa al fudhul na makubaliano yake.

Soma Zaidi...
NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU

Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua.

Soma Zaidi...