Nabii Isa(a.
Nabii Isa(a.s) huitwa “Yesu”, na “Jesus” katika Biblia ya Kiswahili na Kiingereza. Majina yote hayo matatu yanamkusudia mwana wa Maryamu aliyezaliwa bila baba, ambaye ni Mtume wa mwisho kwa Bani Israil.
Nabii Isa(a.s) ni mtoto wa Maryamu aliyekuwa mwana wa Imraani. Kizazi cha Imraani kilichaguliwa na Allah(s.w) kupewa Utume kama tunavyofahamishwa:
Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adamu na Nuhu na kizazi cha
Ibrahiimu na kizazi cha Imraani juu ya walimwengu wote(3:33)
Mke wa Imraani aliweka nadhiri kwa Allah(s.w) kuwa mtoto atakayemzaa atamuweka wakfu. Alitarajia kuwa atazaa mtoto wa kiume.
Aliposema mke wa Imraani: “Mola wangu! Nimeweka nadhiri kwako aliye tumboni mwangu kuwa wakfu, basi nikubalie, bila shaka Wewe ndiye usikiaye na ujuaye.(3:35)
Basi alipomzaa alisema: “Mola wangu! Nimezaa mwanamke”- Na Mwenyezi Mungu anajua sana aliyemzaa -”Na mwanaume si sawa na mwanamke. Na nimempa jina Maryam. nami namkinga kwako, yeye na kizazi chake, uwalinde na shetani aliyewekwa mbali na rehema zako (3:36)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi.
Soma Zaidi...Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.
Soma Zaidi...KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S.
Soma Zaidi...Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.
Soma Zaidi...Mitume huzaliwa Mitume.
Soma Zaidi...