image

Hatua na Mambo (Taasisi za Kisiasa) za msingi alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah

Kuanzishwa kwa Dola ya Kiislamu Madinah.

Hatua na Mambo (Taasisi za Kisiasa) za msingi alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah

Kuanzishwa kwa dola ya kiislamu Madina

Kuanzishwa kwa Dola ya Kiislamu Madinah.
- Kabla ya kufika Madinah, Mtume (s.a.w) akiwa mji wa Quba aliamuru msikiti ujengwe uliokuwa Ukiitwa ‘Masjid Quba.’
Rejea Qur’an (9:108).
- Mtume alifika Madinah (Yathrib), Oktoba 622 A.D.
- Kwa heshima ya Mtume (s.a.w) Madinah ikapewa jina la Madinatun-Nabii (mji wa Mtume) na Al-Madinah Al-Munawwarah (mji ung’aao).


Hatua na Mambo (Taasisi za Kisiasa) za msingi alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah.

1.Kujenga Msikiti.
- Msikiti ulikuwa ndio Ikulu, mahakama, kituocha jeshi, ukumbi wa bunge (shura), n.k. Qur’an (3:95), (2:150).
- Ulikuwa kituo muhimu cha kiharakati katika kusimamisha na kuendeleza Uislamu. Rejea Qur’an (22:40), (2:114), (72:18) na (9:19).

2.Kujenga Ummah wa Kiislamu.
- Mtume (s.a.w) aliwapatanisha kabila la Aus na Khazraj Madinah waliokuwa na uadui wa muda mrefu baina yao. Qur’an (3:103).
- Mtume (s.a.w) pia aliwaunganisha udugu imara kati ya Muhajirina wa
- Makkah na Answaar wa Madinah na kuwa ummah mmoja. Qur’an (8:75).
- Pia aliimarisha uchumi kwa kuunganisha ummah wa Kiislamu na kuwa kitu kimoja. Qur’an (59:8-9).

3.Kuweka Mkataba wa Madinah (Madinah Charter).
- Mtume (s.a.w) alijieleza katika mkataba huo kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na ndiye kiongozi mkuu wa Dola ya Kiislamu.
- Mkataba uliainisha vipengele vya amani na wajibu wa kila kundi kati ya makabila ya Mayahudi na Waarabu washirikina wa Madinah na Dola ya Kiislamu Madinah.
- Uliainisha nafasi, majukumu na wajibu wa waumini katika Dola.
- Mkataba uliainisha uhuru wa kila mtu kuabudu kwa mujibu wa imani na dini zao.

4.Kuweka Mikataba ya amani na Makabila ya Mayahudi na mengine yaliyokuwa pembezoni mwa Dola ya Kiislamu Madinah.
- Makabila na koo tatu za Kiyahudi zenye nguvu zilizokuwa pembezoni mwa mji wa Madinah yalikuwa;
?Banu Quraizah
?Banu Qainuqa na
?Banu Nadhir

5.Kuunda Shura na Sekretarieti.
- Mtume (s.a.w) aliteua washauri wake wakuu katika kuendesha Dola ambao Walikuwa Abu Bakr (r.a), Umar bin Khattab (r.a), Uthman bin Affan (r.a), Ally bin Abu Twalib (r.a) na Hamza bin Abdul-Muttalib (r.a).

- Aliteua waandishi maalumu wa kuandika na kutunza mikataba, takwimu, kumbukumbu na nyaraka zote za Dola ya Kiislamu Madinah.

6.Kuandaa Ummah wa Kiislamu Kijeshi na Kiusalama.
- Mtume (s.a.w) aliwaanda na kuwahimiza waislamu kuwa wakakamavu na hodari katika shabaha, mieleka na kutumia silaha.
- Kila Muislam alikuwa mpiganaji na mpelelezi dhidi ya maadui wa waislamu na Dola ya Kiislamu. Rejea Qur’an (4:71).
- Aliunda na kuweka vikosi vya doria na ulinzi kuzunguka mipaka ya Dola ya Kiislamu Madinah. Qur’an (8:26).

7.Kuimarisha Uchumi.
- Mtume (s.a.w) aliwahimiza waislam kufanya kazi kwa bidii ili kujiimarisha Kiuchumi na kuendeleza Dola.
- Utoaji wa Zaka, Sadaka na mapato mengine yalihimizwa na kukusanywa Kijamii na kuboresha huduma za jamii.
Rejea Qur’an (22:41).

Mafunzo yatokanayo na Kuanzishwa kwa Dola ya Kiislamu Madinah.
Kutokana na mambo ya msingi aliyoyafanya Mtume (s.a.w) katika kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah tunajifunza yafuatayo;

1.Hatunabudi kuanzisha na kuendesha vituo vya harakati, msikiti ukiwa ndio kitovu cha msingi.

2.Mshikamano, kuhurumiana na kupendana kwa vitendo baina ya waislamu ndio nyenzo pekee katika kuhuisha na kuendeleza harakati za Kiislamu.

3.Hatunabudi kuishi vizuri, kuwahesimu na kuwatendea haki, wasiokuwa waislamu hasa wale wasiopiga vita waislamu na Uislamu wazi wazi.

4.Ni wajibu kwa kila muislamu kuwa mkakamavu, jasiri na kujifunza mafunzo ya kijeshi na kuwa tayari kulinda na kuupigania Uislamu katika jamii.

5.Hatunabudi kuwajua vema maadui wa Uislamu na Waislamu, mbinu na silaha zao na kuchukua tahadhari dhidi yao.

6.Ni wajibu kuimarisha uchumi wetu kwani ndio nyenzo muhimu na ya msingi katika kuendesha harakati za Kiislamu.

7.Uongozi bora, makini na uwajibikaji wa kila mmoja kulingana nafasi yake ndio kiungo muhimu katika kuendesha harakati za Kiislamu.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 809


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA NABII SALIH(A.S
Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Siffin na matokeo yake: Vita vya Ally na Muawia
Soma Zaidi...

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)
Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...

Hitimisho juu ya Historia ya maimam wanne
Soma Zaidi...

Bani Israil Kuabudu Ndama
Wakati Nabii Musa(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SHUAIB
Soma Zaidi...

Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake
Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri. Soma Zaidi...

Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mapambano Dhidi ya Maadui wa Dola ya Kiislamu
1. Soma Zaidi...

Maswali kuhusu Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake
Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s. Soma Zaidi...

MAMA YAKE MTUME MUHAMMAD (S.A.W) ANAMLEA MTUME MUHAMAD AKIWA NA UMRI WA MIAKA MINNE (4)
KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s. Soma Zaidi...