image

Kisiwa cha uokozi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad

KISIWA CHA UOKOZI

Nikajisogeza vyema hata nikafika kwenye kivuli. Na kwa kuwa miguu yangu haikuwa na nguvu nilibuluzika tu. Nililala bila ya kijitambua niliamshwa na maji yaliyokuwa yakinipiga miguuni kumbe maji yalikuwa yanajaa. Haukupita muda ghafla nikaona kuna kijahazi kinaingia kikiwa kina mifugo kadhaa. Walipofika pale kisiwani wakawafungulia mifugo yao na kuanza kuwaosha na kuwapaka dawa. Mmoja wao akaenda mbali kidogo akaja na majani mengi sana na kuanza kuchagua baadhi ya ng’ombe na kuanza kuwapa majani yale.

 

Niliwafuata na kuwaomba msaada wa chakula. Wakanipa maziwa na mkate wa nyama. Nilipomaliza kula wakaniuliza habari yangu na eneo lile na nikawaeleza kila kitu. Basi wakaniambia kama ungekuja kesho usingetukuta na pengine ungefia hapa maana hakuna majahazi yanayokuja hapa ila ni sisi tu na huchukuwa miezi 3 ndo tunakuja tena. Na kisiwa hiki hakina chakula, hivyo pengine ungeishia kufariki hapa. Basi wakanipatia na nguo na nikawauliza pia sababa ya wao kuja hapa na ni kinanani wao.

 

Mkubwa wao akanieleza kuwa wao ni watumishi wa mfalme aliyepo karibu na eneo hili. Mfalme huyo amekiteua kisiwa hiki kama eneo la kutibia mifugo yake na amepanda majani maalumu kama dawa ya mifugo yake. Hivyo eneo hili hawaruhusiwi watu wengine hapa. Basi walipomaliza shuhuli zao walifunganya mizigo yao na kuchukuwa majani mengi na nikaondoka pamoja nao.

 

Tulipofika kwenye utawala wao wakanipeleka kwa mfalme wao na nikamueleza mimi ni nani na nini kazi yangu na kumueleza kuwa natokea baghdada nchini kwa sultan Harun Rashid. Basi mfalme yule nikamueleza mengi kadir alivyouliza na mimi sikuwacha kuu;liza mambo kadhaa. Kwa haraka zaidi mfalme yule alionekana kunipenda sanan na kunikubali. Basi alinifanya katika watu wa karibu yake na ni kama mshauri pia. Niliishi pale nikawa nafanya biashara chini ya mfalme yaani nilikuwa naendeleza bishara za mtoto wake wa kike.

 

Siku moja niligundua kuwa kuna kisiwa jirani ambapo kunasikika sauti za furaha kila siku. Nilipouliza nikajibiwa kuwa ni kisiwa jirani huwa wannafanya sherehe kila wanaporudi kutoka kutafuta lulu. Hicho ni kisiwa pekee kinachofahamika kwa kuwa ni wafanyabiashara wa lulu. Basi kwa kuwa sikuijua lulu ilibidi niumuombe ruhusa mfalme ili na mimi nikashuhudie sherehe zao na nipate kuijua lulu. Mfalme alikubali na akanipa msafara wa wafanyakazi wake waende pamoja nami.

 

Tulipofika kule nilifurahi kuiona lulu kwa mara ya kwanza na nikafurahia pia sherehe zao. Basi katika hali kama zile nilishangaa kuona kuwa watu wanashusha mizigo kutoka bandarini lakini katika ile mizigo kuna ambayo imeandikwa Sinbad, nilipoangalia kwa uzuri nikagundua kuwa nahodha wa lile jahazi alikuwa ni yule nahodha wetu. Hivyo kumbe zile mali zilikuwa ni zakwangu na lile jahazi lilikuwa ni lile letu. Nikamuita kijana mmoja na nikamuuliza habari zao na akanieleza kuwa walibahatika kuliokoa jahazi lao na watu wote walipona isipokuwa Sinbad ndo hakuonekana. Kijana huyu alizungumza bila ya kunijuwa kama ndo mimi

 

Basi nikamfuata nahonda na kumueleza kuwa mimi ndo Sinbad na zile mali ni za kwangu. Basi nahonda alliponiona akanikumbuka na kutoa machozi kwa furaha maana walifahamu kuwa nimekufa. Nahodha akanikabidhi mali zangu na nikaziuza, nikapata habari kuwa jahazi letu litarudi Baghdad wiki ijayo. Nilichukua bidhaa zangu na kuuza baadhi na kurudi kwa mfalme na baadhi ya bidhaa. Nikamuelezea kilichotokea na alifurahi sana kwa kupata bidhaa zangu. Na hivi ndo Mwenyezi Mungu anavyowafanyia watu wenye subira.

 

Nikampatia mfalme bidhaa zilizobaki kama zawadi na nikamuomba ruhusa ya mimi kurudi nyumbani kwetu wiki ijayo. Kwa majonzi na kinyongo mfalme aliniruhusu na hata binti yake alikuwa na majonzi sana lakini haina budi “milima haikutani binadamu hukutana” ni maneno nilojisemea moyoni. Basi wiki ilipoisha mfalme alinipatia mali nyingi sana kama zawadi. Nilipata pia lulu kutoka kwenye kisiwa kile. Kwa hakika katika safari hii nilipata taabu na faida kubwasana.

 

Tulipofuka Baghdadi niliwaelezea ndugu zangu habari ya yalonikuta, kwakweli waliniambia niwachanena habari za biashara hii. Hata mimi nikajiapiza kwa yalonikuta kwa hakika sitarudia tena bishara hii. Basi nikatoa sadaka kutoka katika faida yangu na nikatoa na zaka muda ulipo fika. Nilitumia faida ile kujiendeleza kibiashara hata miezi mingi ikapiata. Nilisahau kabisa yalonikuta kwenye safari ile. Baada ya muda nahodha wetu wa mwanzo nilikutana nae, na katika mazungumzo yetu alinieleza kuwa wanatarajia kuanza safari wiki ijayo.

 

Kwa hakika nilivutiwa tena na biashara ile. Na kwa kuwa nilisahau machungu yalonikuta katika safari ya kwanza nikaazimia kuanza safari ya pili wiki ijayo. Mpaka kufikia hapa Sinbad kwa baharini akamaliza kusimulia hadithiya safari yake ya kwanza. Na kwa kuwa muda ulukuwa umekwenda hakuweza kuanza hadithi ya safari yake ya pili. Basi akampatia Sinbad mbeba mizigo zawadi nyingi na pesa kadhaa ya kutumia kama fidia ya kuvunja kazi zake. Na akamuahidi kesho awahi kuja maana safari ya pili ina mambo mengi na makubwa zaidi kuliko ya kwanza.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 903


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

SAFARI YA KWANZA YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA KWANZA YA SINBAD Tambua kuwa baba yangu alikuwa ni mfanya biashara mkubwa sana katika nchi ya baghdad wakati wa utawala wa sultan harun Rashid. Soma Zaidi...

BINTI WA NDOTONI
Download kitabu Hiki Bofya hapa BINTI WA NDOTONI. Soma Zaidi...

Kisiwa cha uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo watatu wa mfalme na wanawake wa Baghdad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

KISIWA CHA UOKOZI
Download kitabu Hiki Bofya hapa KISIWA CHA UOKOZI Nikajisogeza vyema hata nikafika kwenye kivuli. Soma Zaidi...

HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME Mimi ni mtoto wa mfalme kama nilivyotangulia kusema na ni mtoto wa kipekee kwa baba na mama. Soma Zaidi...

Kitabu Cha hadithi ya Chongo
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Safari ya tatu ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

HADITHI YA CHONGO WATATU NA WANAWAKE WA BAGHADAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa HATITHI YA CHONGO WATATU WATOTO WA WAFALME NA WANAWAKE WA BAGHDAD Hapo zamani katika nchi ya Baghdad kulikuwepo na mbeba mizigo maarufu sana. Soma Zaidi...

SAFARI YA SABA YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA SABA YA SINBAD Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani Soma Zaidi...

HADITHI YA KISIWA CHA MAWE YANAYOLIA
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YAKISIWA CHA MAWE YANAYOLIA. Soma Zaidi...

Kuingia kwa wageni
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...