Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi


image


Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela


HADITHI YA MZEE WA PILI NA MBWA WAWILI WEUSI.

Mzee wa pili akapewa ruhusa ya kusimulia stori yake na mbwa wawili weusi. “kwanza utambue ewe mkuu wa majini kuwa hawa mbwa unaowaona ni ndugu zangu wa baba na mama mmoja, stori ilikuwa hivi”

 

Baba yety alikuwa ni tajiri mkubwa katika mji tuliokuwa tukiishi. Alipofariki alituachia mali kubwa na tukaigawa mafungu matatu kulingana na idadi yetu. Tuligawana sawa kwa sawa. Ndugu zangu hawa wakajikita kwenye biashara za nje na ndani ya mji. Wakawa wanasafirisha bdhaa kwenda miji mbali mbali, na hata kwenye visiwa.

 

Mimi niliamua kufungua duka hapa mjini na kwa neema za Allah biashara ikawa nzuri. Mali yangu ilifikia mara tatu ya ile niliopata kutoka kwenye urithi. Sikumoja ndugu zangu walitoka kibiashara, walikaa kwa muda wa miezi isiyopunguwa miwili. Baada ya hapo nikaona kuna watu wawili wamesimama mbele ya duka langu. Sikuwatambuwa watu hawa kutokana na mavazi yao. Walikuwa wamevaa mavazi yaliyochakaa ama yaliyookotwa jaani. Niliataajanu kuona wana nifahamu, baada ya kuzingatia zaidi nikagunduwa ni ndugu zangu.

 

Nikawapa mavazi na chakula kisha wakanihadithia mkasa wao. Walikuwa wamepata ajali na malizao zote zimetokomea majini. Nikachukuwa ile faida yangu na nikaigawa sasa kwa sawa kati yao. Wakaanza biashara tena na hawakukoma baada ya muda wakaamua kusafiri tena kibiashara. Hali ilikuwa mbaya zaidi wakati huu. Walipata ajali tena majini na wakktupiwa nchi kavu wakuiwa hata mavazi hawana.

 

Niwalipfika nyumbani sikuwatambuwa kwa kuwa walikuwa uchi na wakiwa wamechafuka ngozi zao. Wakajitambulisha na niliilia kwa huruma. Machozi yangu nhayakufaha kitu kwa kuwa tayari jambo lilisha tokea. Kama mara ya kwanza nikawapa mtaji na wakaanza upya biashara zaoi. Baada ya muda biashara zao zikakaa vizuri, na wakaamuwa kutoka tena kibiashara. Ila mara hii walitaka niende pamoja nao. Nilipinga zaidi safari hii lakini walinilazimisha na hata maandalizi pia wakanifanyia.

 

Sikuwa na jinsi nikajiandaa na mimi kwa safari. Nikachukuwa mali zangu nikazigawa sehemu mbili na sehemu moja nikachukuwa na nyingine nikaificha. Safari ilianza vizuri na tulifika miji mbalimbali tukifanya biashara. Nilipata faida kubwa na nikanunuwa baadhi ya bidhaa ambazo ningeziuza pindi nitakapo rejea.

 

Muda wa kurudi uliwadia tukawa tunaanda safari ya kurudi. Nilipokuwa matembezini nikitafuta bidhaa na zawadi za kwenda nazo nyumbani, nilipita ufukweni nikakutana na mwanamke aliyevaa mavazi yaliyo chakaa. Nilimsalimia na akarudisha salamu, nikamchukuwa na kumtafutia mavazi yaliyo mazuri. Kwa mavazi yale uzuri wake ulidhihiri mbele yangu. Kwakuwa sikuwa na mke ilibidi nifuate taratibi za kufunga nae ndoa na akakubali. Maandalizi yote yalipoisha nilimchukuwa mke wangu kurudi nae nyumbani.

 

Tukiwa kwenye jahazi zikugunduwa kumbe ndugu zangu walikuwa wananionea wivu. Wakawa wananipangia njama ya kuniuwa. Ulipofika usiku walinichukuwa na kunitumbukiza majini. Baada ya pale sikujuwa kilichoendelea nikajikuta nipo nchi kavu. Mke wangu akanieleza khabari za yote yaliyotokea na akanieleza kuwa yeye si mtu wakawaida. Akaniambia pia hatoweza kuwasamehe ndugu zangu kwa walichonifanyia. Nilimuomba asiwaue ila nipo radhi kwa adhabu yeyote ile.

 

Alinichukuwa mpaka nyumbani kwangu, kisha akalizamisha jahazi waliopanda ndugu zangu. Mali zangu zote akaziokoa. Siku iliyofata nikiwa nyumbani nikaona kuna mbwa wawili weusi wanakuja huku wakionesha majonzi na hali ya kuomba msamaha. Nilistaajabishwa na tukio hili. Haukupita muda mke wangu akatokea na akaniambia hawa ni nduguzangu amewapa adhabu hii. Watakuwa hivyo kwa muda wa miaka 10.

 

Miaka 10 sasa imefika, na kwakuwa alinielekeza sehemu ya kukutana, ndio nimetoka kuelekea hapo sehemu. Nikaona niwachukuwe ndugu zangu kwa kuhofia kuwaacha kwa mtu asie akawadhuru.

 

Hii ndio stori yangu na mbwa hawa ewe mkuu wa majini. “hii ya kwako inamakubwa zaidi” ni maneno ya jini. Baada ya hapo mzee wa tatu akazitupa miguuni kwa jini na kutaka ruhusa aruhusiwe kughadithia stori yake ili iwe ni kafara ya kuachiwa huru mfanya biashara. Lile jini likasema “hapana nimetosheka na hizi mbili, na nimekubali kumuacha huru mfanya biashara” jini lilizungumza maneno haya na kuondoka.

 

Mfanya biashara akawashukuru wazee wale. Basi wakati wazee wale wapokaribu na kuondoka yule mfanya biashara akamuuliza mzee yule wa tatu mwenye mbwa mwekundu kuhusu habari ya mbwa yule. Mzee akamwambia ni stori ndefu ila kwa ufupi huyu ni mke wangu. Akaanza kusimulia hadithi yake kwa ufupi huku akiwa na haraka ya kutaka kuondoka eneo lile



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Kisa Cha mfugaji na mkewe
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Mtihani penzini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Hadithi ya waziri aliyeadhibiwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Aladini katika pango la utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara. Soma Zaidi...

image Mshenga wa aladini mbele ya mfalme
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Hadithi ya mji uliogeuzwa mawe
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Kuelekea bonde la uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambao walipoteana katika hali za kukimbizwa na wazazi Ili waweze kutimiza ndoto zao na siku wakakutana wakiwa watu wazima. Soma Zaidi...