Ndani ya pango la makaburi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad

NDANI YA PANGO LA MAKABURI

Mmoja wapo akatowa kamba na kulifunga jeneza vizuri na kuanza kulishusha chini ya mapango kwa kamba ile.hatimaye n ikahisi jeneza limefika chini kutokana na kugonga chini. Nikalifungua jeneza lile na kutowa mikate yangu nane na maji yangu. Nikaangalia huku na huku hakuna pa kutokea. Nikaangalia juu ni mbali sana na tundu ni dogo na hata sauti haifiki. Nilizunguka mchana mzima sikupata pa kutokea. Sikuya kwanza, pili, tatu mpaka siku ya nne sikupata pa kutokea. Nilikata tamaa nikajua sasa huu ndio mwisho wa Sinbad.

 

Nikaanza kula mikate yangu kwa kuilinda ili isiishe kwa araka. Sasa imefika siku ya sita nikiwa na mikate miwili mkononi. Ilipofika siku ya saba mida ya mchana nikasikia migongano. Nikasogea karibu kwenye lile tundu loo!! ni jeneza linakuja. Nilikuwa nikihisabu siku kwa kuangalia mwanga kwenye tundu lile dogo la kuingizia majeneza. Jeneza lile lilipofika chini nikaona mwanamke aliye hai amezikwa na mumewe. Mwanamke yule nikamsaidia kutoka pale nikiwa na imani kuwa ana mikate yake saba ambapo huenda akanisaidia pindi ya kwangu ikiisha. Nikamsaidia kutoka pale na kujanae pembeni kabisa ya lile pango ambapo harufu za wafu hazifiki kwa kasi.

 

Siku ile usiku nilipolala ghafla nikasikia sauti ya mnyama anayechimba, nikasogea vizuri ila kwa kuwa ni kiza nisione vyema. Nikamwacha akaenda kule kwenye wafu na kuanza kula mizogo. Aple nilipo nikajisemea kuwa sasa huenda hii ndio nusura. Mnyama yule akala mizoga na muda wake ulipofika akatoka. Mimi nikawa namfatilia kwa nyuma usiku ule, tukapita njia nyembamba sana hatimaye akatokea baharini. Basi nikarudi tena kule pangoni kwenda kumchukuwa yule mwenzangu na kuchukuwa mali ambazo watu wamekuwa wakizikwa nazo kama mikufu ya dhahabu na thamani nyinginezo.

 

Nilibeba mzigo mkubwa sana wa mali za dhahabu na thamani nyingine nzuri. Tukatka mimi na mwenzangu yule na kwa bahati tukakutana na jahazi linaloelekea baghadad. Tulipanda mimi na mwenzangu yule. Tulipofika baghadad niliwahadithia kila kilichotokea na walishangaa sana kuniona nipo hai. Yule mwanamke nilompata kule nilisubiri eda yake ilipoisha kulingana na tamaduni za waislamu nikamwoamimi. Kwa hakika safari hii nimepata faida sana na mafunzo mengi.

 

Sin bad alipomaliza hadithi hii ya safari yake ya nne akamwambia Sinbad mbeba mizigo kuwa awahikesho ajesikia yalompata kwenye safari ya tano. Safari hii ya tano kuna matukio kadhaa yalinikuta hivyo uwahi mapema. Kisha akampatia pesa kwa ajili ya matumizi ya siku ile na ijayo. Watu wote wakatawanyika.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela1 Main: Burudani File: Download PDF Views 1269

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Safari ya saba ya Sinbad

Posti hii inakwenda kukuletea muendelezo wa safari saba za Sinbad

Soma Zaidi...
Hadithi ya chongo wa pili mtoto wa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Kitabu Cha hadithi ya Chongo

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Alif lela u lela 1

Alif lela u lela ni hadithi zilizosheheni utamu na machungu pamoja na visa vya wachawi na majinim soma sasa.

Soma Zaidi...
MWANZO WA USALITI

Download kitabu Hiki Bofya hapa USALITI UNANZA HAPA Baada ya kukaa pale siku moja nahodha akaamrisha chombo kiondoke pale na kurudi nyumbani.

Soma Zaidi...
Kutokana kwenye kisima mpaka kuwa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
JINI NA MFANYABIASHARA

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA JINI NA MFANYA BIASHARA.

Soma Zaidi...
SAFARI YA TANO YA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA TANO YA SINBAD Baada ya watu kukusanyika siku ilofata sinbad akaanza kusimulia stori ya safari yake ya tano.

Soma Zaidi...
HADITHI YA KINYOZI MSIRI WA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA KINYOZI MSIRI WA MFALME.

Soma Zaidi...