SAFARI SABA 7 ZA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI SABA ZA SINBAD Katika nchi ya Baghdad kulikuwepo na kijana aliyejulikana kama Sinbad mbeba mizigo.

SAFARI SABA 7 ZA SINBAD

pic
Download kitabu Hiki Bofya hapa

SAFARI SABA ZA SINBAD

Katika nchi ya Baghdad kulikuwepo na kijana aliyejulikana kama Sinbad mbeba mizigo. Kijana huyu alijaaliwa kuwa na uwezo mkubwa wa nguvu za kuweza kubeba mizgo. Pia alikuwa na uwezo mzuri wa kiakili. Sinbad aliipenda sana kazi yake pia watu walimpenda kwa kuwa alikuwa akifanya kazi zake kwa umakini.

Ilitokea sikumoja alipokuwa katika kituo chake cha kufanyia kazi alikuwa mtu mmoja asiyemfahamu kabisa na kumpa kazi ya kupeleka mzigo wake sehemu husika. Mtu yule alitoweka baada ya kutoa maelekezo na kumpatia pesa yake. Sinbad baada ya kupewa maelekezo aliuchukuwa ule mzigo na kuanza kuukokota kwenye mkokoteni wake kuupeleka alikoelekezwa.

Njiani Sinbad alikutana na geti liliozungukwa na mauwa mazuri yenye kuvutia ndege, wadudu na wanyama kwa harufu na utamu wake. Sinbad alisimama kidogo eneo hili ili apate kushangaa uzuri ulioje wa eneo hili. Akilini alijiambia kuwa bila shaka ndani ya eneo hili kuna nyumba kubwa yenye bosi mkubwa.

Sinbad akiwa katika hali hiyo alituwa mzigo wake chini na kuanza kufuta jasho lake. Alisogea kidogo kwenye geti lile na kuona ndani kuna mambo ya kuvutia. Sinbad alikuwa ni kijana mwenye adabu na heshima lakini leo alisahau mambo yote hayo na akaanza kuchungulia ndani kwa watu. Alipokuwa hatoshelezi macho yake aliamua kuingia kwenye geti lile ili aone zaidi.

Sinbad hakuamini macho yake kama yanamuonesha sahihi, aliona nyumba kubwa yenye kila akijuacho kuwa kinahitajika, na aliona pia ambavyo havijui. Aliona nyumba iliyozungushiwa malumalu na lulu zikiwa zinaningi’inia kama mauwa mazuri yaliyopambwa. Rangi za nyumba utadhani ni dhahabu iliyochovywa. Kawahakika Sinbad alistaajabu sana. Kisha akaanza kuzungumza maneno yaloonesha kumalaumu mwenyezi Mungu kwa kuwapa watu wengine mali nyingi kama anazoziona pale. Pa aliendelea kumlaumu mwenyezi mungu kwa kumfanya yeye apate rizki kwa jasho jingi lakini watu wengine wapo wamekaa na bila jasho wanapata rizk.

Sinbad alilalamika sana hata akasikiwa na mwenye nyumba. Basi akaamrisha aletwe, akiwa natetemeka kwa woga Sinbad alipelekwa mbelel za Mkuu wa nyumba. Kisha akamwambia akae. Sinbad hakuamini kama meambiwa akae maana alifikiri atapewa adhabu kali. Basi mkuu wa nyumba akamuuliza “unaitwa nani kijana” “naitwa Sinbad “ au Sinbad mbeba mizigo. Yule mzee akamwambia jina zuri sana na inaonekana wewe ni wajina wangu. Mimi naitwa Sinbad au ukipenda niite Sinbad wa baharini.

Baada ya kutambulishana majina Sinbad wa baharini akaanza kumwambia Sinbad mbeba mizigo. “kijana nimekusikia maneno yako, ila sio kosa lako kusema maneno yale na wewe pia si wa kwanza. Kwani wapo wengi wamesema kama wewe. Sasa leo nataka nikueleze kuwa mimi sikupata mali zote hizi kwa kukaa hapa bila ya jasho. Kabla sijapata mali hizi nilipata tabu kubwa sana na pengine hakuna anayeweza kunifikia jasho na taabu nilizopata wakati natafuta malihizi”

Huu ni wakatii sasa wa mimi kula na kuulia kwani mchumia juani hula kivulini. Kabla ya hapo mimi nilikuwa ni mfanya biashara wa majini yaani nasafiri visiwa mbalimbali. Utajiri wote kuu umettoka na na taabu na mashaka yalonikuta. Nilisafiri safari SABA ambazo hizo nilipata taabu kubwa sana na sito sahau. Leo nitakueleza wewe na walokuwepo hapa yalonikuta kwenye safari hizo.”

Basi kabla hajaanza kusimulia Sinbad mbeba mizigo akamwambia Mkuu mimi nina mzigo wangu natakiwa niupeleke sehemu hivyo niruhusu niondoke. Palepale Sinbad wa baharini akamwambia nitakupa mtu umuelekeze apeleke yeye hiyo mizigo na nitakulipa pato la siku yako yote ila ukae na mimi leo upate kusikia hadithi saba za safari zangu saba. Basi palepale akamuagiza mtu apeleke mzigo ule na vinywaji na vyakula vialetwa. Watu wakakusanyika na kukaa tayari kusikiliza hadithi za safari saba za sinbad. Badi bila ya kuchelewa akaanza kusimulia hadithi ya safari zake kama ifuatavyo:-


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela1 Main: Burudani File: Download PDF Views 1567

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

SAFARI YA SABA YA SINBAD

Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA SABA YA SINBAD Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani

Soma Zaidi...
Ndani ya pango la makaburi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad

Soma Zaidi...
HADITHI YA BINTI MWENYE KUFICHWA MTOTO WA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA BINTI MWENYEKUFICHWA, MTOTO WA MFALME.

Soma Zaidi...
Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya binti wa pili mwimba mashairi mwenye makovu

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME.

Soma Zaidi...
Hadithi ya binti mwenye kufichwa mtoto wa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Kitabu Cha hadithi ya Chongo

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...