image

Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI WAKE.

Mkuu sasa nakwenda nakwenda kukuhadithia habari ya ngu na huyu mbuzi niliye naye. Kwanza tambua huyu mbuzi unayemuona hapa ni mke wangu wa ndoa niliyeishi naye kwa muda wa miaka 30 bila ya kupata mtoto. Pale nyumbani kulikuwa na mtumwa hivyo nikamfanya mwanangu kwa maandishi.

 

Mke wangu kumbe kitendo hiki hakukipenda kitendo kile. Nilitoka kwa ajili ya shughuli za kibiashara huyu mke wangu alijifundisha uchawi na akambadili mtoto wangu na mama yake kuwa ng’ombe. Kisha akawapeleka kwa mfanya kazi wangu wa shambani ili awalishe na kkuwatunza.

 

Haikupita muda nikarudi kutoka safarini kwangu, na nikamuuliza kuhusu mtoto wangu na mama yake lakini akanijibukuwa mama wa mtoto wangu amefariki inapata miezi miwili sasa. Na kuhusu mtoto wangu ametoweka nyumbani na hafahamiki alipo. Jambo hili lilinishangaza sana lakini sikuwa na la kufanya zaidi ya kumtafuta bila ya mafanikio.

 

Ulipofika msimu wa sikukuu nilimwambia mfanyakazi wangu aniletee ng’ombe aliyenona ili nimchinje kwa ajili ya kusherehekea sikukuu. Nililetewa ng’ombe mmoja mzuri sana mwenye afya. Jambo lililonishangaza wakati nataka nimchinje ng’ombe huyu alikuwa akitoa machozi na akiniangalia kwa huruma. Kwakweli jambo hili halijawahi kutokea. Nikaagizwa arudishwe na niletewe mwengine.

 

Mkewangu alikasirika kuona ng’ombe anarudishwa, akanifata na kunisisitiza nimchinje. Nikamweleza mfanyakazi wangu amchinje yeye mii siwezi. Basi akamchinja ng’ombe yule. Jambo la ajabu ni kuwa ijapokuwa ng’ombe yule alikuwa amenenepa lakini hakuwa na nyamba ila ni mifupa mitupu. Nilishangazwa sana. Nikaagiza niletewe mwengine, na akaletwa ndama mmoja aliyenenepa vizuri. Huyu pia alifanya kama yule wa mwanzo alikuwa akitowa machozi na akajilaza miguuni mwangu kama anaomba aachiwe asiuliwe.

 

Huruma ilinijaa na nikaamua aondolewe aletwe mwingine. Mke wangu akanilazimisha ili nimchinge. Nikamuweka vizuri ili kuanza kumchinja, niliweka kisu kooni na nilipokaribia kumchinja aliniangalia kwa jinjo la unjonge na huku akitowa machozi. Kisu kilianguka na nikashindwa kumchinja. Nikaagiza arudishwe. Mke wangu alikasirika sana lakini mara hii sikubadili kauli yanngu

 

Siku ilofata mfanyakazi wangu alinifata kwa mazungumzo ya faragha akanieleza kuwa binti yake ana taaluma ya uchawi hivyo anataka kuzungumza na wewe faragha. Ilibidi nikutane nae, mazungumzo yake yaninistaajabisha sana. “mkuu ulipoondoka mkeo alijifunza uchawi na akambadili mtoto wako na yule mama yake kuwa ng’ombe. Yule ulomchinja jana ni mama yake na yule ng’ombe mdogo ulomrudisha ndiye mwanao. Nitaweza kumrudisha mwanao kawaida kwa masharti, kwanza uniwachie mkeo nimpe adhabu, na pili uniozeshe mwanao.” haya yalikuwa maneno ya binti wa mfanyakazi wangu. Nilikubaliana na masharti yale.

 

Yule binti akachukuwa maji na akatamka maneno nisiyoyajuwa kisha akammwagia yule ng’ombe, papo hapo akawa katik umbo labinadamu. Nilifulahi sana. Kama mashart tulokubaliana alimfata mke wangu na kutamka maneno flani na mke wangu akageuka kuwa mbuzi huyu ambaye unamuona.

 

Ni muda mrefu sasa hatujaonana na mwanangu hivyo nimetoka ili kama nitaweza kupata taarifa zake zozote. Hivyo nimeona ubaya kumuacha mke wangu huyu mbuzi chin ya uangalizi wa watu wengine. Nikaona bora nimchukuwe. Hii ndio stori yangu ewe mkubwa katika majini.

 

“naam nakubaliana na stori yako, kweli inasikitisha hivyo nitampunguzia adhabu huyu mtu” ni maneno ya jini akimwambia mzee wa kwanza. Baada ya huyu mzee wa kwanza kuzungumza, mzee wa pili akapiga magoti kwa lile jini akaliambia, “ewe mkuu katika majini naomba usikilize na mimi stori yangu na hawa mbwa wawili, kama utaona inasikitisha zaidi naomba umpunguzie adhabu huyu mtu”.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1125


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA: HADITHI YA MFANYABIASHARA NA JINI
Soma Zaidi...

HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Hadithi ya kifo cha Damu
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

KUELEKEA BONDE LA UOKOZI
Download kitabu Hiki Bofya hapa KUELEKEA BONDE LA UOKOZI Alinibeba akapaa angani sana hata sikuona ardhi. Soma Zaidi...

Wanyama ambao hutolewa zaka
(ii) Wanyama wafugwao kwa ajili ya chakula Wanyama wafugwao wanaotolewa Zakat ni ngamia, ngo’ombe, mbuzi na kondoo. Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo wa pili mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

SAFARI YA TATU YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA TATU YA SINBAD Siku ile ya pili Sinbad mbeba mizigo alivaa ngup zake safi alizonunua na kijipamba vyema na kuelekea kwenye kikao chao. Soma Zaidi...

KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO
Download kitabu Hiki Bofya hapa KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO. Soma Zaidi...

Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Safari ya nne ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo wa kwanza mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA (sehemu ya kwanza): KIAPO CHA SULTAN
Soma Zaidi...