image

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 4: Kisa cha waziri aliyeadhibiwa

Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA

HADITHI YA WAZIRI ALIYEADHIBIWA.

 

Kulikuwa na mfalme aliyekuwa na mtoto wake mmoja wa kiume. Alimpenda sana mtoto huyu, huenda ni kwa sababu alikuwa ni mmoja na ni wakipekee. Mtoto huyu alipenda sana kuwinda na alikuwa ni hodari wa kupanda farasi, hasa alikuwa na uwezo wa kumdandia farasi kwa haraka sana. Zaidi haayo aliweza kuelewa lugha nyingi. Alikuwa anapokwenda kuwinda akienda na waziri ambaye alipewa kazi ya kumlinda mtoto huyu.

 

Walitoka sikumoja kwenda kuwinda, waliwinda kwa muda mrefu bila ya kupata kitu. Mtoto huyu akaona kibendera kimenyanyuliwa (isharaya kuonekana kiwindwa) alijuwa kuwa aliyonyanyuwa ni waziri. Basi akakifata kibendera na akakutana na swala mzuri mwenye afya. Alimfata na swala akikimbia, alichukuwa muda mwingi na hatimaye akaamuwa kurudi. Kwa bahati mabya alipotea nyia na asijuwe pa kurudia. Hakujuwa waziri yupo wapi, hivyo akazidi kutokomea mwituni

Ilipofika karibia na jioni alikutana na bint mmoja msituni, akamkaribia na kumsalimia. “unafanya nini hapa na na ninnani wewe?” ni maswali aliyomuuliza binti yule. “mimi ni mtoto wa mfalme wa hindi na hapa nimepote” yalikuwa majibu ya bint. Basi akamchukuwa kwenye farasi wake na wakawa wanatafuta njia. Wakapita sehemu kuna jumba lililohamwa siku nyingi. Yule bint akashuka na kijana akashuka pia. Bint akawa anaelekea mule ndani. Alipoingia ndani yule kijana akiwa nje akasikia sauti ya yule bint ndani kwa lugha ya kihindi (yule binti alidhani yule kijana hatelewa lugha ile) “wanangu nimekuleteeni nyama kubwa yenye afya leo” akasikia sauti nyingine zikijibu “iko wapi mama tuile tuna njaa sana mama”. Kijana akagunduwa yule bint si mtu wa kawid,

 

Yule kijana kusikia vile kwa uhodari alio nao akaruka kweye farasi haraka na kuondoka. Baada ya mwendo wa dakika kadhaa akakutana na njia ya kuelekea kwao. Alipofika akamweleza baba yake kuhusu kilicho tokea. Mfalme alikasirika na akamwadhibu waziri kwa kutokuwa makini na kusababisha ajali kwa mwanae.

 

Baada ya kusimulia hadithi hii waziri akamwambia mfalme “angalia sana mfalme, unaonekana umemwamini sana tabibu, lakini usijejuta kwa kumuamini kwako kama alivyojuta huyu mfalme aliyemwadhibu waziri wake baada ya kumwamini”. Maneno haya yalimpenye sana mfalme, hivyo akaamuwa kumuamini waziri wake. Hivyo akaamuwa kumuuwa yule tabibu wake.

 

Siku iliyofuata akaamrisha askari wakamkamate tabibu na kumleta mbele yake. Tabibu akiwa hajui kinachoendelea, anashangaa kuambiwa amekamatwa kwa kosa la kupanga njama za kumuua mfalme. Tabibu akawa anajitetea “sasa kama ningetaka kumuuwa mfalme ina maana gani nikamponya?”. Ijapokuwa alizidi kujitetea lakini mfalme alishaamuwa ubaya hivyo hakusikiliza maelezo yake.

 

Katika hali ngumu kama hii, yule tabibu akataka apewe ruhusa ya mwisho kuzungumza. “zungumza bila shaka, hata uzungumze vip leo utauliwa tu rafiki yangu tabibu.”. Ni maneno yaliyojaa kejeli kutoka kwa mfalme. Tabibu akazungumza “mimi sina kosa mfalme, ninaapa kwa jina la Allah, mimi sina kosa kabisa, lakini kama haina budi mimi kuuliwa, kuna kitabu changu kipo nyumbani, kitazungumza ukweli wote, juu yangu mimi. Kitabu hiki kitazungumza pindi utakapo niua”.

 

Baada ya mazungumzo haya mfalme akapatwa na mshangao na kuzungumza kimoyomoyo “yaani ili hicho kitabu kizungumze ukweli wa mambo mpaka wewe nikuuwe ndo kizungumze? Hii kweli ni khabarikubwa. Basi sina budu kukuuwa ili nione maajabu ya kitabu kinachozungumza”. Mfalme akamuuliza tabibu tukupe muda gani ukakilete hicho kitabu? “miachieni leo ili niweze kukiandaa kisha kesho nitakuja nacho hapa, na hukumu yangu itatekelezwa.” ni maneno ya tabibu kumwambia mfalme.

 

Basi mfalme akaamrisha askari wake wamlinde tabibu. Tabubu alipotoka pale akaenda nyumbani kwake na kuiaga familia yeke kwa uchungu na machozi ya hali ya juu. Baada ya pale akachukuwa hicho kitabu akakipaka dawa iliyo na rangi ya kijibu. Dawa hii ipo kama ungaunga, na haina harufu kali. Akakipaka kitabu kurasa zote. Ilipofika asubuhi akachukuwa beseni la maji lakini halikuwa na kitu ndani na akatoka kwake akiongozwa na askari wa mfalme. Alipofika sehemu ya hukumu akaanza kutoa maelekezo yake.

 

“nitakapokuwa nimeuliwa chukueni kichwa changu kisha kiwekeni juu ya kitabu kilichopo kwenye beseni hili. Pindi damu itakapoanza kutotesha gamba la nje la kitabu hiki mfalme atakichukuwa na kufungua mpaka ukurasa wa 6 wa kitabu hiki.” haya yalikuwa ni maelekezo ya tabibu kwa mfalme kuonesha maandalizi ya kitabu kitakachozubgumza. Basi haukupita muda dabibu akauawa kwa upanga.

 

Kwa shauku mfalme akafuata maelekezo kama alivyoambiwa. Damu ilipoanza kutotesha kitabu akakichukuwa kwa shauku kubwa. Akawa analamba kidole chake kutia mate ili afunguwe kurasa kwa urahisi, kichwa kikasema “funguwa mpaka ukurasa wa sita”. Akaanza kufunguwa huku anatia mate kidole na kisha nafungua, alifanya hivi mpaka akafika kurasa wa sita na hakukuta maandishi yoyote. Kichwa kikasema “fungua mpaka mwisho” akaendelea kufungua huku analamba kidole kutia mate, mpaka akafika mwisho na asione chochote.

 

Ghafla macho yake yakaanza kulegea na mwili ukaanza kupoteza nguvu, damu zikaanza kutoka puani, kisha kichwa kikaseme “na ukatili wako, haukujuwa kama ulikuwa ukilamba sumu iliyopo kwenye kurasa. Umebakiwa na muda mchache kufa. Hivi ndivyo watu waovu wanavyolipwa uovu.” baada ya maneno haya kichwa kikapoteza maisha na haukuchukuwa muda mfalme akafa huku anajuta kwa kumuua tabibu na kuamini maneno ya waziri wake.

 

Baada ya kumaliza kusimulia hadithi hii mvuvi akamwambia jini “kama mfalme angemwamini tabibu na kupotezea maneno ya waziri wake, haya yole yasingetokea. Hivi pia ndivyo itakavyokuwa kati ya mimi na wewe, nikikuamini nitajuta. Hivyo mimi nakutupa baharini sasa hivi na nitaweka alama na tangazo hapa ili kula mvuvi ajuwe kilichopo hapa nin nini. Na nitajenga na nyumba pia nitakaa hapa kuwaonya wavuvi.

 

Jini kusikia maneno haya akamwambia usinifanyie kama imma alivyomfanyia ateka. Mvuvi kwa shauku akauliza “kwani imma alinfanyia nini ateka?”. Jini likamjibu “unadhani nitakwambia wakati umenifungia humu?, nifungulie na nakuahidi nitakufanya tajiri maisha yako yote, nakuahidi”. Mvuvi kwa kupenda mali akakubali ahadi ya jini na akamfungulia, jini lilipotoka likapiga teke chupa ile na likacheka kwa sauti ya juu. Hali hii ilimuogopesha sana mvuvi. “usiogope rafiki yangu, nimefanya hivi kukutisha tuu, mimi naamini sana ahadi”. Ni maneno ya jini kumwambia mvuvi. Kisha akamwambia amfate na achuuwe na nyavu zake.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-09 13:19:06 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 56


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 1: Carmaralzamani prince pekee
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 15: Baba tajiri na kifo chake
Muendelezo....... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 9: Familia mpya
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 8: Harusi ya aladini kufanyika na binti wa mfalme
Muendelezo...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 20: Waliodhulumiwa kufanyiwa suluhisho
Ni mojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 18: Binti wa pili mwimba mashahiri mwenye makovu
Mwendelezo wa hadithi kutoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 5: Nani ni binti?
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 1: Aladini na taa ya mshumaa wa ajabu
Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 18: Hadithi ya fundi cherehani
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 4: Simulizi ya chongo wa kwanza mtoto wa Mfalme
Tusikilizie simulizii inahusu chongo wa kwanza wa mtoto wa mfalme iliyopo ndani ya kitabu cha kwanza cha Hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 5: Simulizi ya samaki wa ajabu
Simulizii hii inapatikana kwenye hadhithi za HALIF LELA U LELA katika kitabu cha kwanza.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Mtumwa wa mfalme na mawaziri
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha tatu..... Soma Zaidi...