image

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 14: Hadithi ya kifo cha kujionea

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza Muendelezo wa safari ya Sinbad

SAFARI YA SITA YA SINBAD.

 

Walipokusanyika watu wote akaanza kusimulia kuhusu safari yake ya sita. Nilipookoka na safari ya tano sikutamani tena kusafiri kwa njia ile. Hali hii haikudumu kwa muda mpaka nilipoamua kufanya safari ya mwisho kwani nilikuwa uymri umeshakwenda sana. Nikaamini kuwa faida nitakayoipata safari hii sitafanya safari nyingine yeyote ya majini. Basi nilianza kujiandaa kwa ajili ya safari hii. Hata hivyo maandalizi yalichukuwa muda kwani umri ulikuwa umeshakuwa mkubwa. Baada ya maandalizi safari ikaanza.

 

Safari hii ilikuwa mbaya sana, maana hata hatukuweza kupata siku mzima iliyo salama. Mara tuu baada ya kuanza safari kwa muda wa masaa kama nane kwa makadirio upepo uliharibika na kuwa mkali sana. Jahazi lilikuwa likipelekwa tusukokujuwa kwa muda wa siku tano. Siku ya sita upepo ulitulia katika sehemu ambayo hata hatuijui kabisa. Nahodha baada ya kuangalia zaidi eneo hili alilitukusanya karibu na akatuambia kuwa hapa tulipo tupo katika mkondo hatari sana baharini na hakuna jahazi lililokuja mkondo huu na kupona. Ghafla maji yaendayo kwa kasi yakatuchukuwa na kutupeleka kwenye ufukwe wa kisiwa tusichokijua. Tulipofika pale nahodha akatuambia tuchuke sisi na mizigo yetu kisha akagawa chakula tulicho nacho sawa kwa sawa kwa kila mtu. Kisha akatuambia kuwa hapa tulipo hakuna upepo unaotoka kuelekea kokote. Maji yote yanavutwa kuelekea hapa. Na eneo hili kama mnavyoona lina mlima huu ambapo hata ukipanda sauti haitafika popote wala kusikiwa na mtu.

 

Kisha akatuambia kuwa hakuna yeyote atakuja kutuakoaa hapa hivyo maisha ya mtu kuishi yatategemea kuisha kwa chakula chake. Wakati anazungumza maneno yale mimi nilikuwa nawaza yalonikuta kule kwenye mapango. Basi hali ikawa hivyo kwa hakika hakuna pa kutokea. Nilizunguka kuangalia eneo li;le nikagunguwa kuwa kuna mto ambao umetokea mlimani kisha ukakunja bila ya kuingua baharini ukarudi upande wa bondeni kudogo pembeni mwa ufukwe na ukapotelea kwenye pango ililo jembaba.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 10:15:00 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 30


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 2: Ni ndoto ama kweli???
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 14: Jaribio la pili kwa Aladini
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 16: Usaliti
Hadithi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na zinavutia na zinasomwa na kusikilizwa kwa wakubwa na wadogo na hii simulizi inatoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nudhini na mtumwa
Muendelezo....... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 20: Kinyozi maishani mwangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 4: Sehemu ya pili ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 2:  Simulizi ya tabibu wa mfalme
Simulizi ni nzuri sana maana zinafundisha na hazibagui mkubwa wala mdogo... tusikilize na kusoma kisa cha tabibu wa mfalme....kutoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 16: Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 3: Uokozi kwenye kisiwa
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 18: Binti wa pili mwimba mashahiri mwenye makovu
Mwendelezo wa hadithi kutoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 7: Hadithi ya safari ya majibu juu ya maswali mawili
Wapendwa wasomaji na wasikilizaji wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tuendelee kusikiliza hadithi zetu mzuri na za kusisimua.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part24 : Kaka wa tatu wa kinyozi
Muendelezo Soma Zaidi...