picha

Kichaa cha mbwa.

Post hii inahusu zaidi kichaa cha mbwa,au kwa kitaalamu huitwa rabies, utokea pale mtu anapongatwa na mnyama ambaye ni jamii ya mtu au mbwa mwenyewe

Kichaa cha mbwa.

1.kichaa cha mbwa utokea pale mbwa anapomngata mtu  inawezekana akangata sehemu yoyote ya mwili inawezekana ukawa mkono , mguu yaani sehemu hiyo mbwa wanaachia virusi na ukaa kwenye kidonda kwa mda.

 

2. Baadae virus hao wanapitia kwenye mfumo wa Neva system, hasa hasa Neva zinazoelekea kwenye ubongo na virus wakishafika kwenye ubongo uhakikisha wameshambulia ubongo na hapo mtu ufanana kama amechanganyikiwa hivi na kuweza kuongea mambo yasiyofaa kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye ubongo.na hapo mgonjwa uweza kubwaka kama mbwa na pengine kuanza kuogopa vitu mbalimbali kwa mfano kuogopa maji.

 

3. Pia virus vikisha shambulia kwenye ubongo uendelea kuzaliana na kuongezeka na kuendelea kushambulia sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha mgonjwa kuwa na tabia kama za mbwa kabisa, pamoja na kubweka na mlio uweza kubadilika kuwa kama wa mbwa hapo mgonjwa hawezi kumaliza mda mrefu na kwa kawaida ufariki.

 

4. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kufahamu namna ya kichaa cha mbwa kinavyotokea na kuweza kutibu mapema au ikitokea mtu akangatwa na mbwa hata kama haujui kama mbwa ana kichaa au Hana ni lazima kuanza chanjo mara Moja kwa sababu chanjo zipo na zinapatikana kwenye hospital nyingi sana, kwa sababu ugonjwa huu unaua.

 

5. Na pia ni vizuri kabisa kuweza kuchanja mbwa mara kwa mara Ili kuweza kuepukana na tatizo hili linalopelekea kuhatarisha maisha ya watu, na pia chanjo ya kichaa cha mbwa ni ya gharama kweli ambapo kila chanjo ni sh elfu ishilini na tano na udungwa kwa mfululizo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2484

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k

Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.

Soma Zaidi...
Kivimba kwa utando wa pua

post hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa utando wa pua unaoonyeshwa na mchanganyiko wa dalili zifuatazo: Kupiga chafya Msongamano wa pua Muwasho wa kiwambo cha sikio Kuwasha kwa pua na koromeo Uvimbe huu hutokea ikiwa mashambulizi ya kupiga chafya,

Soma Zaidi...
Dalili, chanzo, sababu na vmambo hatari kuhusu kifua kikuu

Katika makala hii utajifunza kuhusu kifua kikuu, dalili zake, sababu zake, chanzo chake na mambo hatari kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
Athari za kutotibu fangasi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu athari za kutokutibu fangasi

Soma Zaidi...
Je wiki 1 dalili zinaonyesha za maambukizi ya ukimwi na wiki 3 vipimo vinaweza kuonyesha Kama umeasilika

Muda ambao maambukizi ya virusi vya ukimwi kuonyesha dalili unaweza kutofautiana kutika mtu hadi mwingine.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa fungusi uken

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa fungusi uken, ni ugonjwa unaoshambulia sana sehemu za Siri ambao huwa na dalili kama zifuatazo.

Soma Zaidi...