image

Njia za jumla za kujikinga na magonjwa mbalimbali

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona

Njia za kujikinga na magonjwa.

1. Njia ya kwanza ni kufanya usafi wa mazingira,kufanya usafi wa binafsi yaani kuoga, kufua nguo, kukata kucha, kusafisha meno, kunywa maji safi na salama na mambo hayo ya kuhakikisha mwili unakaa kwenye hali ya usafi kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa,na pia kwa upande wa mazingira, kukata nyasi zilizozunguka makazi , kumchoma takataka,kutunza uchafu sehemu Moja na kutoruhusu kuishi sehemu Moja na wanyama, yaani kuwatengea wanyama sehemu yao kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa.

 

 

2. Kupata kinga ya mwili.

Kwa upande wa kupata kinga ya mwili ni pamoja na kupata chanjo zote zinazohitajika mwilini hasa hasa kwa watoto kwa kufanya hivyo tunazuia magonjwa ambayo yanaweza kutokea hapo mbeleni,kwa mfano kupata chanjo ya kifua kikuuu, kupata chanjo ya kuzuia kupooza, kupata chanjo ya kuzuia kuharisha kupata chanjo ya pepo punda na chanjo zote za lazima kwa mtoto na kwa mabinti wanaotegemea kubeba mimba kupata chanjo zinazohitajika Ili kuepuka magonjwa mbeleni. Kwa kuweka mwili katika hali ya kinga ni vigumu kupata magonjwa.

 

 

3. Kula mlo kamili.

Kuna msemo usemao kwamba chakula Bora ni dawa, kwa sababu mlo ukiwa kamili na kutosha ni vigumu sana kupata magonjwa, kwa mfano aina zote za vyakula zikiwa sawia ni vigumu kupata magonjwa kwa mfano matumizi mazuri ya vyakula vya wanga, protein, mafuta kidogo na mboga za majani za kutosha na kunywa maji kulingana na uzito wako kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa, lakini Kuna tabia ambayo watu wanapendelea aina Moja ya vyakula hasa vyakula vya madukani vilivyojaa kemikali na mafuta kwa wingi sukari wakitegemea kupata afya njema kwa kufanya hivyo matokeo yake ni kinenepeana na kuwa na vitambi hatimaye magonjwa ya presha na mengine mengi tu. Kwa hiyo kula mlo kamili ni kujikinga na magonjwa.

 

 

4. Kuangalia afya Yako mara kwa mara.

Kitendo cha kuangalia afya mara kwa mara nayo ni hatua Moja kubwa kwa sababu unaweza kukuta Kuna ugonjwa upo na ujautibu au kwa wakati mwingine ukikutwa na presha labda inaelekea kuwa juu unarekebisha mtindo wa maisha au ukikuta sukari ni kubwa unapunguza kiwango cha sukari kwa kufanya hivyo ni vizuri kabisa kuepuka na magonjwa au kwa vijana ni vizuri kabisa kupima maambukizi na magonjwa ya zinaa ikitokea kuna ugonjwa ni kuanza dawa mapema Ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali ambayo ni pamoja na ugumba kama Kuna zinnia Kali au kuepuka kinga ya mwili kushuka kama Kuna maambukizi ya virus vya ukimwi.

 

 

5. Elimu kutolewa kila mara.

Kwa kupitia watu mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu ni jambo zuri na la busara kwa sababu pengine Kuna mlipuko Fulani wa magonjwa jamii ikijulishwa mapema na kuweza kujikinga na kufuata mashart au tiba kama ipo ni vigumu kupata magonjwa kwa hiyo viongozi wa jamii wawe tayari kutoa elimu kwa waliowazunguka Ili kuzuia kuongezeka kwa magonjwa.

 

 

6. Kutibu magonjwa kama yapo.

Njia nyingine ya kupunguza magonjwa ni pamoja na tiba kama Kuna ugonjwa Fulani kwenye jamii ni vizuri kutibu ugonjwa huo Ili kuepuka kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu Kuna watu wenye kinga ya hali ya juu ana ugonjwa ila haoneshi dalili ni vizuri kutoa ushauri na kuhakikisha kuwa ugonjwa unatibika kwa watu wenye hali ya hivyo.

 

 

7. Kutumia dawa endapo Kuna maambukizi.

Ni vizuri kabisa na jambo zuri kutumia dawa ikiwa umefanya vipimo na kugundulika una maambukizi kwa mfano watu wenye maambukizi ya virus vya ukimwi ni vizuri kabisa kutumia dawa na wasione aibu kabisa kwa sababu wasipotumia dawa wanaweza kuwa na magonjwa nyemelezi yanayosababisha afya zao kuyumba.

 

 

8. Kwa hiyo kuzuia kupatwa na magonjwa ni kazi inayoweza kufanikiwa zaidi kwa kuhakikisha mazalia ya wadudu wanaosambaza magonjwa kuharibiwa kwa mfano kujaribu mazalia ya mbu, nzi na wadudu wote ambao tnajua kazi zao ni kusambaza magonjwa tunaweza kutumia njia zozote pamoja na kutumia dawa za madukani za kuua wadudu.

 

 

9. Kwa hiyo kwa kufanya hayo yaliyojadiliwa magonjwa yanaweza kupungua au yasiwepo kabisa kwa sababu magonjwa yanakuwepo kwenye jamii kwa sababu ya kutozingatia tuliyoyajadili ambayo ni kutokula mlo kamili, tabia ya kutoangalia afya zetu, kushindwa kutumia dawa baada ya vipimo,kutofanya usafi kwenye mazingira yetu,kuishi na wadudu wanaosababisha ugonjwa na mambo mengine kama hayo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuziangatia hayo Ili tuwe mbali na magonjwa.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1074


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu
kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako Soma Zaidi...

Ugonjwa wa coma
Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la Kichwa, Kiharusi, Uvimbe kwenye ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi, Soma Zaidi...

Matatizo yanayoweza kusababisha Saratani.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na matatizo yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa Saratani. Soma Zaidi...

Bawasili usababishwa na nini?
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili. Soma Zaidi...

Nini kinasababisha kizunguzungu?
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu Soma Zaidi...

Namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni njia ambazo mtu anaweza kutumia Ili kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.zifuatazo ni njia zinazoweza kutumika kama mtu amepata uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo. Soma Zaidi...

dalili za mimba changa ndani ya wiki moja
Je na wewe ni katika ambao wanahitaji kujuwa dalili za mimba ndani ya wiki moja? kama ndio makala hii ni kwa ajili yako. Utakwenda kuona dalili za mwanzo sana za ujauzito toka siku za mwanzoni. Soma Zaidi...

Ni nini husababisha kuziba kwa Njia ya machozi
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa kuziba kwa Njia ya machozi yaani kukosa machozi ambayo husababishwa na maambukizi. Soma Zaidi...

Aina za kifua kikuu.
Posti hii inahusu zaidi aina mbili za kifua kikuu, aina ya kwanza ni ile ya kawaida ambayo ushambulia mapafu na aina ya pili ni ile ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye limfu node, kwenye sehemu za moyo, kwenye uti wa mgongo, kwen Soma Zaidi...

Ninashida Kuna mtu anaumwa pressure Kila anap pima Iko juu il mwil aumuumi at kidg n dawa anatumia unawez kunisaidiaj
Kama unasumbuliwa na presha post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakuoatia ushauri kutokana na swali alilouliza mdau wetu. Soma Zaidi...

Minyoo na athari zao kiafya
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu minyoo na athari zao kiafya Soma Zaidi...

Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt Soma Zaidi...