NJIA ZA JUMLA ZA KUJIKINGA NA MAGONJWA MBALIMBALI


image


Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona kabisa Bali tunaishi nayo na kufuata mashart ya kupunguza makali ya ugonjwa.


Njia za kujikinga na magonjwa.

1. Njia ya kwanza ni kufanya usafi wa mazingira,kufanya usafi wa binafsi yaani kuoga, kufua nguo, kukata kucha, kusafisha meno, kunywa maji safi na salama na mambo hayo ya kuhakikisha mwili unakaa kwenye hali ya usafi kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa,na pia kwa upande wa mazingira, kukata nyasi zilizozunguka makazi , kumchoma takataka,kutunza uchafu sehemu Moja na kutoruhusu kuishi sehemu Moja na wanyama, yaani kuwatengea wanyama sehemu yao kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa.

 

 

2. Kupata kinga ya mwili.

Kwa upande wa kupata kinga ya mwili ni pamoja na kupata chanjo zote zinazohitajika mwilini hasa hasa kwa watoto kwa kufanya hivyo tunazuia magonjwa ambayo yanaweza kutokea hapo mbeleni,kwa mfano kupata chanjo ya kifua kikuuu, kupata chanjo ya kuzuia kupooza, kupata chanjo ya kuzuia kuharisha kupata chanjo ya pepo punda na chanjo zote za lazima kwa mtoto na kwa mabinti wanaotegemea kubeba mimba kupata chanjo zinazohitajika Ili kuepuka magonjwa mbeleni. Kwa kuweka mwili katika hali ya kinga ni vigumu kupata magonjwa.

 

 

3. Kula mlo kamili.

Kuna msemo usemao kwamba chakula Bora ni dawa, kwa sababu mlo ukiwa kamili na kutosha ni vigumu sana kupata magonjwa, kwa mfano aina zote za vyakula zikiwa sawia ni vigumu kupata magonjwa kwa mfano matumizi mazuri ya vyakula vya wanga, protein, mafuta kidogo na mboga za majani za kutosha na kunywa maji kulingana na uzito wako kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa, lakini Kuna tabia ambayo watu wanapendelea aina Moja ya vyakula hasa vyakula vya madukani vilivyojaa kemikali na mafuta kwa wingi sukari wakitegemea kupata afya njema kwa kufanya hivyo matokeo yake ni kinenepeana na kuwa na vitambi hatimaye magonjwa ya presha na mengine mengi tu. Kwa hiyo kula mlo kamili ni kujikinga na magonjwa.

 

 

4. Kuangalia afya Yako mara kwa mara.

Kitendo cha kuangalia afya mara kwa mara nayo ni hatua Moja kubwa kwa sababu unaweza kukuta Kuna ugonjwa upo na ujautibu au kwa wakati mwingine ukikutwa na presha labda inaelekea kuwa juu unarekebisha mtindo wa maisha au ukikuta sukari ni kubwa unapunguza kiwango cha sukari kwa kufanya hivyo ni vizuri kabisa kuepuka na magonjwa au kwa vijana ni vizuri kabisa kupima maambukizi na magonjwa ya zinaa ikitokea kuna ugonjwa ni kuanza dawa mapema Ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali ambayo ni pamoja na ugumba kama Kuna zinnia Kali au kuepuka kinga ya mwili kushuka kama Kuna maambukizi ya virus vya ukimwi.

 

 

5. Elimu kutolewa kila mara.

Kwa kupitia watu mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu ni jambo zuri na la busara kwa sababu pengine Kuna mlipuko Fulani wa magonjwa jamii ikijulishwa mapema na kuweza kujikinga na kufuata mashart au tiba kama ipo ni vigumu kupata magonjwa kwa hiyo viongozi wa jamii wawe tayari kutoa elimu kwa waliowazunguka Ili kuzuia kuongezeka kwa magonjwa.

 

 

6. Kutibu magonjwa kama yapo.

Njia nyingine ya kupunguza magonjwa ni pamoja na tiba kama Kuna ugonjwa Fulani kwenye jamii ni vizuri kutibu ugonjwa huo Ili kuepuka kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu Kuna watu wenye kinga ya hali ya juu ana ugonjwa ila haoneshi dalili ni vizuri kutoa ushauri na kuhakikisha kuwa ugonjwa unatibika kwa watu wenye hali ya hivyo.

 

 

7. Kutumia dawa endapo Kuna maambukizi.

Ni vizuri kabisa na jambo zuri kutumia dawa ikiwa umefanya vipimo na kugundulika una maambukizi kwa mfano watu wenye maambukizi ya virus vya ukimwi ni vizuri kabisa kutumia dawa na wasione aibu kabisa kwa sababu wasipotumia dawa wanaweza kuwa na magonjwa nyemelezi yanayosababisha afya zao kuyumba.

 

 

8. Kwa hiyo kuzuia kupatwa na magonjwa ni kazi inayoweza kufanikiwa zaidi kwa kuhakikisha mazalia ya wadudu wanaosambaza magonjwa kuharibiwa kwa mfano kujaribu mazalia ya mbu, nzi na wadudu wote ambao tnajua kazi zao ni kusambaza magonjwa tunaweza kutumia njia zozote pamoja na kutumia dawa za madukani za kuua wadudu.

 

 

9. Kwa hiyo kwa kufanya hayo yaliyojadiliwa magonjwa yanaweza kupungua au yasiwepo kabisa kwa sababu magonjwa yanakuwepo kwenye jamii kwa sababu ya kutozingatia tuliyoyajadili ambayo ni kutokula mlo kamili, tabia ya kutoangalia afya zetu, kushindwa kutumia dawa baada ya vipimo,kutofanya usafi kwenye mazingira yetu,kuishi na wadudu wanaosababisha ugonjwa na mambo mengine kama hayo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuziangatia hayo Ili tuwe mbali na magonjwa.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    2 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    3 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    4 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    5 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya html kwa kiswahili    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu ni madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mgonjwa pale ambapo matibabu yanapokuwa hayatolewi kwa mgonjwa wa maumivu chini ya kitovu. Soma Zaidi...

image Dalili za UKIMWI na VVU kutoka mwanzoni mwa siku za mwanzo
Je na wewe ni katika wanaosumbuka sana kujuwa dalili za kwanza za ukimwi toka siku ya kwanza, ama dalili za ukimwi kwenye ulimi, ama unatakakujuwa ni muda gani ukimwi huonekana, na je ukishiriki ngono zembe ndio utapata ukimwi? Basi makala hii ni kwa ajili yako, hapa utakwenda kujifunza hayo na mengineyo mengi kuhusu VVU na UKIMWI. Soma Zaidi...

image Heti kama mtu kafany mapenzi na mtu mwe ukimwi siku hihiyo akenda hospitali kapewa dawa kweli hataweza kuwabukizwa
Swali hili limeulizwa na mdau mmoja. Kuwa endapo mtu atafanya ngono zembe na akapata virusi je ataweza kuambukiza. Soma Zaidi...

image Njia za kushusha presha
Post hii inakwenda kukujulisha njia za kushusha presha iliyopanda. Soma Zaidi...

image YAJUE MARADHI YA KISUKARI
Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari Soma Zaidi...

image Dalili za ugonjwa wa vericose veini
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa vericose veini Soma Zaidi...

image Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID
Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa. Soma Zaidi...

image Nini husababisha kibofu cha mkojo kuuma na baadae kutoka damu
Katika post hii utajifunza sababu zinazowezabkuorlekea kibofu kuuma upande mmoja Soma Zaidi...

image Dalili za maambukizi kwenye magoti
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa Kuna maambukizi kwenye magoti, kwa sababu mbalimbali ambazo usababisha maumivu au maambukizi kwenye magoti Kuna dalili za mwanzo ambazo zinajitokeza kama tutakavyoona hapo chini Soma Zaidi...

image Athari za mkojo mwilini.
Posti hii inahusu zaidi athari za mkojo mwilini, kwa kawaida tunafahamu kwamba mkojo ni matokeo ya mkusanyiko wa uchafu wa maji maji yanayokusanyika kutoka mwilini ikiwa mkojo umebaki mwilini usababisha madhara mbalimbali kama tutakavyoona. Soma Zaidi...