Njia za jumla za kujikinga na magonjwa mbalimbali


image


Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona kabisa Bali tunaishi nayo na kufuata mashart ya kupunguza makali ya ugonjwa.


Njia za kujikinga na magonjwa.

1. Njia ya kwanza ni kufanya usafi wa mazingira,kufanya usafi wa binafsi yaani kuoga, kufua nguo, kukata kucha, kusafisha meno, kunywa maji safi na salama na mambo hayo ya kuhakikisha mwili unakaa kwenye hali ya usafi kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa,na pia kwa upande wa mazingira, kukata nyasi zilizozunguka makazi , kumchoma takataka,kutunza uchafu sehemu Moja na kutoruhusu kuishi sehemu Moja na wanyama, yaani kuwatengea wanyama sehemu yao kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa.

 

 

2. Kupata kinga ya mwili.

Kwa upande wa kupata kinga ya mwili ni pamoja na kupata chanjo zote zinazohitajika mwilini hasa hasa kwa watoto kwa kufanya hivyo tunazuia magonjwa ambayo yanaweza kutokea hapo mbeleni,kwa mfano kupata chanjo ya kifua kikuuu, kupata chanjo ya kuzuia kupooza, kupata chanjo ya kuzuia kuharisha kupata chanjo ya pepo punda na chanjo zote za lazima kwa mtoto na kwa mabinti wanaotegemea kubeba mimba kupata chanjo zinazohitajika Ili kuepuka magonjwa mbeleni. Kwa kuweka mwili katika hali ya kinga ni vigumu kupata magonjwa.

 

 

3. Kula mlo kamili.

Kuna msemo usemao kwamba chakula Bora ni dawa, kwa sababu mlo ukiwa kamili na kutosha ni vigumu sana kupata magonjwa, kwa mfano aina zote za vyakula zikiwa sawia ni vigumu kupata magonjwa kwa mfano matumizi mazuri ya vyakula vya wanga, protein, mafuta kidogo na mboga za majani za kutosha na kunywa maji kulingana na uzito wako kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa, lakini Kuna tabia ambayo watu wanapendelea aina Moja ya vyakula hasa vyakula vya madukani vilivyojaa kemikali na mafuta kwa wingi sukari wakitegemea kupata afya njema kwa kufanya hivyo matokeo yake ni kinenepeana na kuwa na vitambi hatimaye magonjwa ya presha na mengine mengi tu. Kwa hiyo kula mlo kamili ni kujikinga na magonjwa.

 

 

4. Kuangalia afya Yako mara kwa mara.

Kitendo cha kuangalia afya mara kwa mara nayo ni hatua Moja kubwa kwa sababu unaweza kukuta Kuna ugonjwa upo na ujautibu au kwa wakati mwingine ukikutwa na presha labda inaelekea kuwa juu unarekebisha mtindo wa maisha au ukikuta sukari ni kubwa unapunguza kiwango cha sukari kwa kufanya hivyo ni vizuri kabisa kuepuka na magonjwa au kwa vijana ni vizuri kabisa kupima maambukizi na magonjwa ya zinaa ikitokea kuna ugonjwa ni kuanza dawa mapema Ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali ambayo ni pamoja na ugumba kama Kuna zinnia Kali au kuepuka kinga ya mwili kushuka kama Kuna maambukizi ya virus vya ukimwi.

 

 

5. Elimu kutolewa kila mara.

Kwa kupitia watu mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu ni jambo zuri na la busara kwa sababu pengine Kuna mlipuko Fulani wa magonjwa jamii ikijulishwa mapema na kuweza kujikinga na kufuata mashart au tiba kama ipo ni vigumu kupata magonjwa kwa hiyo viongozi wa jamii wawe tayari kutoa elimu kwa waliowazunguka Ili kuzuia kuongezeka kwa magonjwa.

 

 

6. Kutibu magonjwa kama yapo.

Njia nyingine ya kupunguza magonjwa ni pamoja na tiba kama Kuna ugonjwa Fulani kwenye jamii ni vizuri kutibu ugonjwa huo Ili kuepuka kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu Kuna watu wenye kinga ya hali ya juu ana ugonjwa ila haoneshi dalili ni vizuri kutoa ushauri na kuhakikisha kuwa ugonjwa unatibika kwa watu wenye hali ya hivyo.

 

 

7. Kutumia dawa endapo Kuna maambukizi.

Ni vizuri kabisa na jambo zuri kutumia dawa ikiwa umefanya vipimo na kugundulika una maambukizi kwa mfano watu wenye maambukizi ya virus vya ukimwi ni vizuri kabisa kutumia dawa na wasione aibu kabisa kwa sababu wasipotumia dawa wanaweza kuwa na magonjwa nyemelezi yanayosababisha afya zao kuyumba.

 

 

8. Kwa hiyo kuzuia kupatwa na magonjwa ni kazi inayoweza kufanikiwa zaidi kwa kuhakikisha mazalia ya wadudu wanaosambaza magonjwa kuharibiwa kwa mfano kujaribu mazalia ya mbu, nzi na wadudu wote ambao tnajua kazi zao ni kusambaza magonjwa tunaweza kutumia njia zozote pamoja na kutumia dawa za madukani za kuua wadudu.

 

 

9. Kwa hiyo kwa kufanya hayo yaliyojadiliwa magonjwa yanaweza kupungua au yasiwepo kabisa kwa sababu magonjwa yanakuwepo kwenye jamii kwa sababu ya kutozingatia tuliyoyajadili ambayo ni kutokula mlo kamili, tabia ya kutoangalia afya zetu, kushindwa kutumia dawa baada ya vipimo,kutofanya usafi kwenye mazingira yetu,kuishi na wadudu wanaosababisha ugonjwa na mambo mengine kama hayo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuziangatia hayo Ili tuwe mbali na magonjwa.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Madhara ya kichaa cha mbwa
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtu hajatibiwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa. Soma Zaidi...

image Dalili za miguu kufa ganzi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo Uweza kujitokeza na kuona kwamba ni Dalili za miguu kufa ganzi, pengine utokea kwa watu wote na pengine huwa ni kwa ghafla Soma Zaidi...

image Sababu ya maumivu ya magoti.
Posti hii inahusu zaidi sababu za maumivu ambayo yanasikika kwenye magoti, huu ni ugonjwa ambao umewapata walio wengi na bado ni kilio kwa walio wengi kwa vijana na kwa wazee, Kuna wataalamu mbalimbali ambao wameweza kugundua sababu za maumivu kwenye magoti kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?
Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mwanzo hadi kufikia miezi mitatu. Mwisho wa makala hii utaweza kujifunza mambo yafuatayo:- Soma Zaidi...

image Sababu za mwanamke kuumwa tumbo y chini ya kitovu.
Posti hii inahusu sababu za mwanamke kuumwa tumbo chini ya kitovu, ni tatizo ambalo limewapata wanawake wengi na pengine sababu ni vigumu kupata au pengine zinapatikana lakini kwa kuchelewa hali ambayo usababisha madhara mbalimbali kwenye mwili. Soma Zaidi...

image Madhara ya fangasi.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi za ukeni kwa kawaida tunajua kubwa fangasi zikiingia kwenye uke usababisha madhara mbalimbali ambayo mengine yanaweza ya kudumu na mengine ya mda kama yametibiwa mapema. Soma Zaidi...

image Vipimo vya kuchunguza kama una asidi nyingi tumboni
Posti hii inahusu zaidi vipimo vya kuchunguza kama una kiwango kikubwa cha asidi au tindikali tumboni Soma Zaidi...

image Madhara ya maumivu kwenye nyonga na kiuno.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa matibabu kwenye nyonga na kiuno hayatafanyika. Soma Zaidi...

image NI WATU GANI WALIO HATARINI ZAIDI KUPATA UKIMWI?
Post hii itakwena kukufundisha kuhusu historia fupi ya Ukimwi na matibabu yake. Ni wapi wapo hatarini kupata maambukizi na ni kitu gani wafanye? Soma Zaidi...

image Dalili za kasoro ya moyo ya kuzaliwa kwa watu wazima
Ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao (kasoro ya moyo ya kuzaliwa) ni hali isiyo ya kawaida katika muundo wa moyo wako unaozaliwa nao. utu uzima. Ingawa maendeleo ya kimatibabu yameboreshwa, watu wazima wengi walio na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa wanaweza wasipate uangalizi ufaao wa ufuatiliaji.Iwapo ulikuwa na kasoro ya kuzaliwa iliyorekebishwa ukiwa mtoto mchanga, kuna uwezekano bado unahitaji utunzaji ukiwa mtu mzima.Inapaswa kushauriana na dactari ikiwa kuna uwezekano wa kuwa na matatizo, au ikiwa uko katika hatari kubwa ya matatizo mengine ya moyo kama mtu mzima. Soma Zaidi...