Dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika.
Dalili za Ugonjwa wa kichaga cha mbwa.
1.Dalili ya kwanza ni kuwepo kwa maumivu makali kwenye kidonda,kwa kawaida utegemea na ukubwa wa kidonda kwa hiyo kuna tabia ya watu kuanza kutibu kidonda kwa njia za kawaida na kufunika bila kuchomwa dawa inayosababisha kuzuia kichaa cha mbwa hatimaye matokeo huwa mabaya kwa hiyo jamii inapaswa kuelimishwa kuhusu umuhimu wa kutibu tatizo la ugonjwa wa kichaa cha mbwa hospitalini.Na kama Maumivu ni makali kwenye kidonda dawa za kutibu maumivu zinaweza kutumika ili kupunguza maumivu kwenye kidonda.
2.pengine mtu akiumwa na mbwa huanza kuogopa sana akiamini kwamba labda atafariki ila tunapaswa kujua kuwa kama umengatwa nambwa na ukaenda hospitalini na kupewa dawa kuwa na matumizi ni lazima kwa sababu unakuwa umefuata masharit kwa hiyo tuachane na tabia za kuogopa ovyo ovyo, ila kuna woga mwingine utokea kwa sababu ya kuingia kwa wadufu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
3,Kuanza kuogopa maji na kuwa na tabia kama za mbwa, kama vijidudu havijatibiwa vizuri na vikisambaa sehemu mbalimbali za mwili usababisha mgonjwa kuwa na tabia mbwa mpaka kubweka na pengine uanza kuogopa maji ambapo kwa kitaalamu huitwa fear of water.
4. Kuwepo kwa maumivu hasa mgonjwa anapokuwa anameza wakati wa kula chakula.
Dalili mojawapo ya mgonjwa wa kichaa cha mbwa ni maumivu wakati wa kumeza chakula, hali hii utokea kwa sababu wadudu wanakuwa wamesambaa mwili mzima kwa hiyo kwa hatua hizi uponyaji ni kwa neema ya Mungu peke yake.
5. Kama Mgonjwa hajapewa dawa kwa kipindi chote tangia alipongatwa na mbwa dalili zikianza kujitokeza hasa kubweka kama mbwa, kuogopa maji na Dalili zinginezo mgonjwa ni vigumu kupona kwa hiyo anaweza kuishi kwa siku kumi tangu baada ya Dalili za hatari na kumgusa ila kufa ni lazima hasa kwa wagonjwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 kitabu cha Simulizi π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Bongolite - Game zone - Play free game π5 Madrasa kiganjani π6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Dalili ya pressure ya kupanda
Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya
Soma Zaidi...Dalili za saratani ya koo
Saratani ya Koo inarejelea Vivimbe vya Saratani vinavyotokea kwenye koo lako (koromeo), sanduku la sauti (larynx) au tonsils.
Soma Zaidi...Maambukizi ya VVU: Dalili za mwanzo na jinsi ya kuishi nayo.
βMakala hii inachunguza kwa kina virusi vya VVU (Virusi vya Upungufu wa Kinga Mwilini), ikianzia na utambuzi wa dalili za mwanzo (acute HIV infection), umuhimu wa upimaji wa mapema, na mikakati ya kisayansi ya kuishi maisha marefu na yenye tija kwa kutumia tiba ya kufubaza virusi (ART). Lengo ni kuondoa unyanyapaa na kutoa mwongozo wa kitaalamu kwa watu wanaoishi na VVU.
Soma Zaidi...AFYA NA MAGONJWA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Sababu za Ugonjwa wa pumu
Pumu ni ugonjwa wa njia ya upumuaji unaojulikana na kizuizi cha muda mrefu cha njia ya upumuaji. Inahusisha mfumo wa upumuaji unaobana njia ya hewa, Inaweza kuwa ya nje (hii hutokea kwa vijana kutokana na mizio) au ya ndani (hutokea kwa wazee)
Soma Zaidi...