HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)

MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.

Download Post hii hapa

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)


MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.A.W
Ilikuwa ni tamaduni kwa waarabu waishio mjini kuwapeleka watoto wao wachanga vijijini wakalelewe ili wapate ukakamavu, wajifunze lugha vyema na pia kuwaepusha na magonjwa ya miripuko yanayotokea mijini. Hivyo Mtume s.a.w alichukuliwa na Halima bint Dhuaib kutoka katika kabila la bani Sa’ad bin Bakar. Mume wake aliitwa Al-Harith bin ‘Abdul’Uzza pia alitambulia kwa jina la Abi Kabshah.

Halima anasimulia kuwa ulikuwa ni wakati wa ukame sana hususana sehemu ambay alikuwa akiishi yeye na watu wao. Mvua zilikata, wanyama hawakuweza kutoa maziwa kwa ukame uliopo. Wanyama hawakuweza kushiba. Shakula pia kilikuwa ni taabu, lakini tumaini lao lilikuwa ni kusubiria mvua inyeshe. Wakati huo walitoka watu waende mjini kwenda kutafuta watoto wa kuwalea ili waweze kupata kipato kama ujira wa kulea na kunyonyesha watoti hao kama ilivyokuwa ni kawaida yao. Alikuwepo kwenye msafara huu Halima na mume wake.

Bi Halima akiwa amepata punda wake aliyeonekana ni dhaifu sana na mumewe alikuwa amepanda ngamia ameye hakuwa ni mwenye kutoa maziwa. Walifika Maka na wakaanza kutafuta watoto wa kuwanyonyesha. Anaeleza bi halima kuwa katika msafara ule walotoka watu wote walifika kwa mama yake Mtume na kuelezwa kuwa mtoto huyu ni yatima, basi wote wakakataa kumchukuwa Muhammad kwenda kumlea kwa kuhofia wazazi wake hawataweza kulipa gharama kwani mtoto ni yatima.

Msafara huu uliendelea kuzungua Makkah kutafuta watoto wa kuwalea, halimaye bi Halima hakibahatika kupata mtoto, hivyo akashauriana na mumewe kuwa arudi kule kwa mtoto yatima kwani anaona vibaya kurudi mtupu pila ya kuwa na mtoto. Basi mumewe akakubali, na hapo bi Halia akarudi na kumchukuwa mtoto muhammad (s.a.w). na maajabu ndo yakaanza hapa kama vile bi Halima anavyotueleza, Nitataja kwa ufupi zaidi mambo haya yalotokea.

Anaeleza bi Halima kuwa alipombeba mtoto badi alipofika kwenye hema lao aloshangaa kuona maziwa yamejaa, kwa hakika hii ni ajabu kwake kwani hata mtoto wake alikuwa akikosa usingizi usiku kwa uchache wa maziwa. Lakini leo anakuwa na maziwa na kumtosha mtot muhammad pamoja na mtoto wake. Kwa hakika walinyonya watoto hawa wawili mpaka wakashiba na kulala.

Bi halima anasimulia kuwa mume wake alipotoka kwenda kumuangalia ngamia wake alishangaa kuona ngamia ana maziwa ya kutosha, alikamua maziwa kutoka kwenye ngamia wake wakanywa na kushiba. Hii pia ni ajabu aloishuhudia Bi halima baada ya kumchukuwa kijana Mhammad kwa ni hapo mwanzo ngamia wao hakuweza kutoa hata tone la maziwa ya kuweza kunywa, lakini leo ngamia huyu anatoa maziwa ya kuweza kushiba watu wa familia hii na kuyabakisha. Bi Halima anasimula kuwa asubuhi ya siku ilofata mume wangu aliniambia “ hakikahalima umechukuwa mtoto mwenye kubarikiwa” nikamjibu “nami natarajia iwe hivyo”.

Siku ilofata safari ya kurudi kutoka maka kwenda kwao ilianza. Katika msafara huu walishangaa kumuona punda wa halima amebadilika kwani amekuwa na nguvu na ameongeza uwezo wa kukimbia. Ilifikia wakati wnzie wakawa wanamwmbia nenda kipolepole ewe Halima kwa hakika huyu si yule pinda ulokuja ne. Ukweli ni kuwa punda ni yuleyule lakini Allah ameta miujiza yake hapa.

Walipofika nyumbani walishangaa kuona mifugo yao inarudi kutoka malishoni ikiwa imeshiba sana, wakati kulikuwa na ukame mkubwa sana. Mifugo yao iliweza kutoa maziwa mengi. Ilifikia wakati wamiliki wa mifugo wakawa wanawaambia wachungaji wao kuwa wachunge pale anapochungia mchungaji wa bi Halima. Ukweli ni kuwa majani ni yale yale isipokuwa Allah anaweza miujiza yake kwa bi Halima.

Kwa hakika bi Halima aliona miujiza mingi sana, na maisha yake yalibadilika na kuwa na raha na amani to ka amchukuwe mtoto Muhammad (s.a.w). bi Halima anasimulia kuwa mtoto Muhammad alikuwa anakuwa kwa haraka zaidi tofauti na alivyozoea. Bi Halima alimlea mtoto huyu kwa muda wa miaka miwili hata muda wa kumuachisha ziwa ukawadia. Ilikuwa anatakiwa ampeleke mtoto kwa mama yake.

Basi mtoto alipotimia miaka miwili kwa shingo upande bi Halima alimrudisha mtoto kwa mama yake. Huku akiwa haridhiki kwani ameona neema nyingi toka amchukuwe mtto huyu. Alipofika Makkah alimshawishi mamayake amruhusu aweze kurudi nae aendelee kumlea kwa kuhofia mtoto atpata maradhi ya mjini maradhi ya milipuko. Kwa sababu hii mama yake Mtume bi Amina alikubali hivyo bi Halima akaendelea kumlea mtoto huyu. Hvyo Mtume aliendelea kuishi kule na kuendelea kuimarika kimwili na kuwa na afya njema pamoja na kupata ufasaha katika lugha ya kiarabu.


                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1676

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...
Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume
Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume

Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.

Soma Zaidi...
Kuangamizwa kwa jeshi la tembo mwaka alizaliwa Mtume Muhammad s.a. w
Kuangamizwa kwa jeshi la tembo mwaka alizaliwa Mtume Muhammad s.a. w

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w sehemu ya 4. Hapa utajifunza kuhusu historia ya kuangamiza kwa jeshi la tembo.

Soma Zaidi...
tarekh 10
tarekh 10

KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah
Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake
Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake

Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake.

Soma Zaidi...