Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kazi za vitamin B na makundi take
KAZI ZA VITAMINI B NA MAKUNDI YAKE
Vitamini B ni moja kati ya vitamini ambavyo vinahitajika sana mwilini. Athari yeyote ya upungufu wa vitamini hivi inaweza kuonekana moja kwa moja kwenye miili yetu. vitamini B vimegawanyika katika makundi mengi sana ikiwemo B1, B2, B3, B5, B6, B7, B9 na B12. je ungependa kujuwa kazi za vitamini hivi kulingana na aina zake. Endelea na makala hii upate kujifunza kazi za vitamini B.
Kazi za vitamini B kulingana na kila kundi la vitamini B
Basi tambuwa kuwa kuwa kazi za vitamini B ni kuhakikishha kuwa mipambano ya kikemikali inafanyika ndani ya seli. Sasa hapa tutaona kazi za vitamini hivi kulingana na makundi yake:-
1. B1 hii husaidia mfumo wa fahamu (mfumo wa neva) kufanya kazi vyema. Upungufu wa vitamini hivi B1 huweza kuleta maatizo kwenye mfumo wa fahamu, moyo na mupotea kwa misuli.
2. B2 huhitajika kwa ajili ya uzalishwaji wa nishati, lipi, vitamini, madini na husaidia katika utengenezwaji wa antioxidant. Upungufu wa vitamini hivi huweza kusababisha kuvimba (imflamation) kwenye ngozi, ulimi, midomo, na matatizo kwenye mfumo wa fahamu.
3. B3 hii huhitajika katika kufanyika mchakato wa metabolism kwenye seli. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea ngozi kuwa na matatizo kama miwasho, mapele, ukurutu na kadhalika. Pia upungufu wa vitamini hivi huweza kusababisha tumbo kuvurugika na kuleta misongo ya mawazo
4. B6 hii hufanya kazi ya kuhakikisha metabolisma inayohusima katika kuchakata hamirojo asidi za amino, kuchakata hemoglobin hizi ni chembechembe za kwenye seli nyekundu za damu zinazo saidia katika kusafirisha hewa mwilini, pia katika kuthibiti kiwango cha sukari kwenye damu. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea madhara kwenye ubongo, shida kwenye fahamu ya mtu na pia ugonjwa wa anemia unaonasibiana na upungufu wa hewa ya oksijeni mwilini.
5. B9 huhusika katika kuchakata DNA, kuchakata amino acid, katika kukua na kukomaa kwa seli mwilini hasa hasa seli hai nyekundu. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea matatizo katika ukuaji, utengenezwaji na ukomaaji wa seli hai nyekundu za damu, uchovu, maumivu ya kichwa, kutokea uvimbe kwenye mdomo na hata kuathiri mtoto aliyepo tumboni.
6. B12 huhitajika kwa ajili ya utengenezwaji wa seli mpya, utengenezwaji wa damu na pia kwa ajili ya mfumo wa fahamu kufanya kazi vyema. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea kuvurugika kwa tumbo, shida kwenye mfumo wa fahamu pamoja na matatizo kwenye ulimi.
Kazi za vitamini B kwa ujumla
Kwa ujumla vitamini B vina kazi nyingi kama ulivyojifunza hapo juu. Kazi hizi tunaweza pia kuziweka katika ufupisho ufuatao. Lengo la kufupisha ni kukuwezesha msomaji kukumbuka kwa wepesi kazi za vitamini B. Kazi hizo ni kama zifuatazo:-
1. Husaidia mfumo wa fahamu kufanya kazi vyema
2. Huhitajika kwa ajili ya uzalishaji wa nishati (nguvu) mwilini
3. Husaidia katika utengenezwaji wa seli mwilini
4. Husauidia katika utengenezwaji wa hemoglobin hizi ni chembechembe katika seli nyekundu za damu
5. Husaidia katika kuchakata DNA
6. Husaidia katika utengenezwaji wa seli mpya na kukomaa kwa seli
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu, tunajua kubwa kifua kikuu ni Ugonjwa ambao utumia mda mrefu kidogo katika matibabu kwa hiyo mgawanyiko wake uko kwenye sehemu mbili muhimu kama tutajavyoona
Soma Zaidi...Kama mtu anatokwa na damu za pua, basi juwa kuwa anahitaji huduma ya kwanza.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi chanjo ya pentavalent ni aina ya chanjo ambayo inazuia Magonjwa matano ambayo ni kifadulo, pepopunda, homa ya ini na magonjwa yanayohusiana na upumuaji.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa maji mwilini
Soma Zaidi...Kushambuliwa kwa moyo na kupumua ni kitendo Cha moyo kusimama ghafla, Hali hii unapaswa kutolewa huduma ya kwanza Ili moyo ufanye kazi tena,
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi michubuko ambayo mara nyingi utokea kwa watoto wakati wa kuzaliwa,na mara nyingi uweza kupona baada ya masaa ishilini na manne au ndani ya masaa ishilini na manne.
Soma Zaidi...Nimeambiwa presha yangu umeshuka iko 90/60 na Nina umri wa miaka 26 KawaidaMtu anatakiwa na kiwango gani Cha presha
Soma Zaidi...Ajali ya kichwa na ajali inayotolewa kwenye sehemu mbalimbali za kichwa, ambavyo husababishwa madhara kwa aliyepata ajali hiyo
Soma Zaidi...Kungโatwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.
Soma Zaidi...