image

Namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

NAMNA AMBAVYO MWILI HUPAMBANA NA MARADHI

Tumeona huko juu kuhusu visababishi vya maradhi na namna ambavyo maradhi yanaweza kusambaa, sasa hapa tutaona namna ambavyo miili yetu unapambana na maradhi haya kwa ajili yetu. Mwili una njia nyingi tuu na namna ya kupambana na maradhi kama utakavyoona hapo chini

 

1.KA KUTUMIA KUTA ZUIZI (PHYSICAL BARRIERS

Itambulike kuwa ili mtu aumwe ni kwamba wadudu wa maradhi wanatakiwa waingie mwilini. Sasa mwili una vizuizi yaani kuna ukuta maalum ambao unakazi ya kuzuoa wadudu hawa wasipate njia ya kuingia ndani. Vizuizi hivyo ni;-

 

A).Ngozi:ngozi yenyewe ni ukuta wa kuzuia vijidudu hivi. Ngozi hutumia chemikali kama jasho na mafuta ili kuuwa vijidudu hivi.ngozi inatabia ya kujitibu kwa haraka zaidi kama itapata jeraha ili kuzuia wadudu wasiingie.

 

B).Utando wa utelezi: huu ni utando maalumu ambao unateleza na kunata. Utando huu unapatika na sehemu nyingi za mwili kama puani kwa ajili ya kunasa mavumbi na vijidudu hawa. Utando huu pia upo machoni kwa ajili ya kunasa vijidudu hivi na kuvitoa nje.

 

C)Vinyweleo: hivi ni njia nyingine ya kunasa wadudu wowote wanaoraka kuingia ndani. Kwa mfano ndani ya pua kuwa vinyweleo hivi kwa ajili ya kunasa wadudu na mavumbi kuingia ndani.

 

D)Kemikali: kwa mfano mwili huzalisha asidi ya hydrocloric ambayo husaidia kuuwa bakteria waliopo kwenye vyakula.

 

2.INFLAMATORY RESPONSE (YAANI KUVIMBA)

Inatokea wadudu hawa wanaingia mwilini kwa mfano mtu anpojikata. Hivyo inflammatory response hali ya mwili kupambana na ma majeraha ambapo sehemu husika huvimba, huwa njeundu na kuwa na maumivu. Kitendo hiki hufanya eneo hili liwe limoto na kusababisha vimishipa vidogo vinavyoleta damu vilete damu kwa wingi na hatimaye seli kutoka kwenye damu hupambana na wadudu walofanikiwa kuingia kwenye eneo lile.

 

3.IMMUNE SYATEM (MFUMO WA KINGA)

Njia zilizotajwa hapo juu pekee haziwezi kupambana na wadudu hawa. Hivyo kuna mfumo maalumu wa kuukinga mwili dhidi ya majambazi hawa (pathojens) mfumo huu huitwa immune system ambao unatengenezwa na seli hai nyeupe za damu na aina flani ya protin ambayo kitaalamu huitwa antibodies ambazo zipo kwenye mfumo wa lymph (lymphatic system).

 

Mfumo wa lymph huu umezunguka mwili mzima na unahusika katika kubeba majimaji mwilini. Katika kufanya hivi unafanya kazi ya kuwatowa bakteria na pathogen wengine nje ya mwili. Mfumo huu una seli hai nyeupe nyingi nna hizi ndizo ambazo zinapambana na pathogen na kuwauwa.

 

Seli nyeupe za damu, kazi yao kuu seli hizi ni kuulinda mwili dhidi ya wavamizi. Kuna aina fani ya seli hizi hutowa kemikali ziitwazo antibodies ambazo huwakamata pathogens na pitowa tahadhari kwa seli nyingine ili wawaue hawa pathogens. Pindi unapoumwa hutokea tezi za lymph zinauma kama mtoki ni kwa sababu seli hizi nyeupe zipo kwa wingi eneo lile kupambana na wadudu hawa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 641


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Umuhimu wa pua kama mojawapo ya mlango wa fahamu
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa pua kama mojawapo ya mlango wa fahamu.pua ni mlango wa fahamu ambao uhusika na kupumua. Soma Zaidi...

Zijue kazi za ovari
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa ovari kwenye mwili wa mwanamke. ovari ni sehemu ambapo mayai ya mwanamke hutunza, kwa hiyo kila mwanamke huwa na ovari ambayo husaidia kutunza mayai. Soma Zaidi...

Njia za kujikinga na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari Soma Zaidi...

Choo kisichokuwa cha kawaida
Posti hii inahusu zaidi Aina ya choo kisichokuwa cha kawaida, ni dalili za choo ambacho siyo Cha kawaida, Ina maana ukiona dalili za choo Cha Aina hii ni vizuri kwenda hospitalini Ili kupata matibabu. Soma Zaidi...

Nna swali mimi nimefanya Romance na mtu ambaye sijampima kbsa sasa naogopa anaeza kuwa mgonjwa na mm nkaupata
Muulizaji anauliza he kula denda, ama kumbusu ama kufanya romance na muathirika was HIV na wewe uta ambukizwa? Soma Zaidi...

Imani potofu kuhusu kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi imani potofu waliyonayo Watu kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu, hizi ni imani ambazo uwepo kwenye jamii na pengine uweza kuaminika lakini si za ukweli. Soma Zaidi...

Madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo, ni hatari inayotokea kwa mtu ambaye haujatibiwa vidonda vya tumbo. Soma Zaidi...

Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure
Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili Soma Zaidi...

Kwanini mdomo unakuwa mchungu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za mdomo kuwa mchungu Soma Zaidi...

Athari ya kutotibu maambukizi ya kwenye kibofu cha mkojo
Post hii inahusu zaidi athari za kutotibu maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo, nimatazito yanayoweza kutokea iwapo ugonjwa huu hautatibika. Soma Zaidi...

Mkojo mchafu na Rangi za mikojo na maana zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Rangi za mkojo na maana zake na mkojo mchafu Soma Zaidi...

Njia za kuongeza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya njia za kuongeza nguvu za kiume Soma Zaidi...