Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ambavyo mwili unapambana na maradhi
NAMNA AMBAVYO MWILI HUPAMBANA NA MARADHI
Tumeona huko juu kuhusu visababishi vya maradhi na namna ambavyo maradhi yanaweza kusambaa, sasa hapa tutaona namna ambavyo miili yetu unapambana na maradhi haya kwa ajili yetu. Mwili una njia nyingi tuu na namna ya kupambana na maradhi kama utakavyoona hapo chini
1.KA KUTUMIA KUTA ZUIZI (PHYSICAL BARRIERS
Itambulike kuwa ili mtu aumwe ni kwamba wadudu wa maradhi wanatakiwa waingie mwilini. Sasa mwili una vizuizi yaani kuna ukuta maalum ambao unakazi ya kuzuoa wadudu hawa wasipate njia ya kuingia ndani. Vizuizi hivyo ni;-
A).Ngozi:ngozi yenyewe ni ukuta wa kuzuia vijidudu hivi. Ngozi hutumia chemikali kama jasho na mafuta ili kuuwa vijidudu hivi.ngozi inatabia ya kujitibu kwa haraka zaidi kama itapata jeraha ili kuzuia wadudu wasiingie.
B).Utando wa utelezi: huu ni utando maalumu ambao unateleza na kunata. Utando huu unapatika na sehemu nyingi za mwili kama puani kwa ajili ya kunasa mavumbi na vijidudu hawa. Utando huu pia upo machoni kwa ajili ya kunasa vijidudu hivi na kuvitoa nje.
C)Vinyweleo: hivi ni njia nyingine ya kunasa wadudu wowote wanaoraka kuingia ndani. Kwa mfano ndani ya pua kuwa vinyweleo hivi kwa ajili ya kunasa wadudu na mavumbi kuingia ndani.
D)Kemikali: kwa mfano mwili huzalisha asidi ya hydrocloric ambayo husaidia kuuwa bakteria waliopo kwenye vyakula.
2.INFLAMATORY RESPONSE (YAANI KUVIMBA)
Inatokea wadudu hawa wanaingia mwilini kwa mfano mtu anpojikata. Hivyo inflammatory response hali ya mwili kupambana na ma majeraha ambapo sehemu husika huvimba, huwa njeundu na kuwa na maumivu. Kitendo hiki hufanya eneo hili liwe limoto na kusababisha vimishipa vidogo vinavyoleta damu vilete damu kwa wingi na hatimaye seli kutoka kwenye damu hupambana na wadudu walofanikiwa kuingia kwenye eneo lile.
3.IMMUNE SYATEM (MFUMO WA KINGA)
Njia zilizotajwa hapo juu pekee haziwezi kupambana na wadudu hawa. Hivyo kuna mfumo maalumu wa kuukinga mwili dhidi ya majambazi hawa (pathojens) mfumo huu huitwa immune system ambao unatengenezwa na seli hai nyeupe za damu na aina flani ya protin ambayo kitaalamu huitwa antibodies ambazo zipo kwenye mfumo wa lymph (lymphatic system).
Mfumo wa lymph huu umezunguka mwili mzima na unahusika katika kubeba majimaji mwilini. Katika kufanya hivi unafanya kazi ya kuwatowa bakteria na pathogen wengine nje ya mwili. Mfumo huu una seli hai nyeupe nyingi nna hizi ndizo ambazo zinapambana na pathogen na kuwauwa.
Seli nyeupe za damu, kazi yao kuu seli hizi ni kuulinda mwili dhidi ya wavamizi. Kuna aina fani ya seli hizi hutowa kemikali ziitwazo antibodies ambazo huwakamata pathogens na pitowa tahadhari kwa seli nyingine ili wawaue hawa pathogens. Pindi unapoumwa hutokea tezi za lymph zinauma kama mtoki ni kwa sababu seli hizi nyeupe zipo kwa wingi eneo lile kupambana na wadudu hawa.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 746
Sponsored links
👉1
Kitabu cha Afya
👉2
Kitau cha Fiqh
👉3
Madrasa kiganjani
👉4
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉5
Simulizi za Hadithi Audio
👉6
kitabu cha Simulizi
Utaratibu wa lishe kwa wagonjwa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wagonjwa Soma Zaidi...
Mambo yanayosababisha kupona kwa vidonda.
Posti hii inahusu mambo yanayochangia katika kupona kwa kidonda, ni mambo ambayo yapo kwa mgonjwa mwenyewe kama ifuayavyo. Soma Zaidi...
Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo
Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k Soma Zaidi...
Kwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?
Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe? Soma Zaidi...
Ukiwa unalima sana unaweza kukonda
Unadhanivkufanya kazi kunaweza kukusababishia maradhi ama mwili kudhoofu, ama kukonda. Umeshawahivkujiuliza wanao nenepa huwa hawafanyi kazi? Soma Zaidi...
Mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu, kama mtu amepoteza fahamu Kuna mambo muhimu yanapaswa kuangaliwa kwa makini kama ifuayavyo. Soma Zaidi...
Matokeo ya maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maambukizi kwenye milija na ovari, ni matokeo apatayo mtu mwenye maambukizi kwenye milija na ovari. Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fati na mafuta na kazi zake mwilini
Hata kama mtu atakuambbia usile vyakula yenye mafuta bado itahitajika kula tu. Kuna mafuta na fati je unajuwa utofauti wao. Ni zipi kazi zao mwilini? Endelea na makala hii Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha
Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha hii ni chanjo wanayopewa watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa lengo la kuzuia kuharisha chanjo hiyo kwa kitaalamu huitwa Rotarix. Soma Zaidi...
Dalili za unyanyasaji wa kimwili
Unyanyasaji wa kimwili. Unyanyasaji wa watoto kimwili hutokea wakati mtoto amejeruhiwa kimwili kimakusudi.
Unyanyasaji wa kijinsia. Unyanyasaji wa watoto kingono ni shughuli yoyote ya kingono na mtoto, kama vile kumpapasa, kushikana mdomo na sehemu Soma Zaidi...