Dawa ya fangasi kwenye mdomo na ulimi
Utajifunza dalili za fangasi mdomoni na ulimini, sababu za fangasi wa mdomoni na ulimini, matibabu yeke na njia za kukabiliana nao
Dawa ya fangasi kwenye mdomo na ulimi
Fangasi wanaweza kuathiri sehemu yeyote kwenye ngozi ya mtu. Kuanzia vidole, kichwa, kwapa, sehemu za siri na mapajani. Hutokea fangasi wakaathiri mdomo na ulimi. Hapa hali inaweza kuwa mbaya pale mtu akishindwa kula. Bila shaka ni maumivu, lakini leo nitakwenda kukutajia tiba yake.
Nini sababu ya fangasi wa mdomo na ulimi?
Fangasi hawa husababishwa na aina ya fangasi inayoitwa Candida albicans (C.albicans). hawa fangasi ni kawaida kupatikana kwenye mdomo. Kwa mtu ambaye kinga yake ipo imara hakuna shida yeyote anaweza kuipata kwa kuwa na fangasi hawa. Ila endapo watazidi kupitiliza ndipo inaweza kuleta shida.
Dalili za fangasi kwenye mdomo na ulimi
1.Vijidoma vyeupe au njano kwenye shavu kwa ndani, finzi, midomo na kwenye ulimi
2.Kuvuja kwa damu wa finzi
3.Vidonda kwenye mdomo
4.Kuhisi kama kuna pamba kwenye mdomo (vinyuzinyizi)
5.Ukavu wa kona za mdomo pamoja na mipasuko
6.Taabu katika kumeza
7.Mdomo kuwa na ladha mbaya
8.Kupotesa ladha ya unachokila.
Fangasi wa mdomoni wanaweza kuambukiza?
Yes wanaweza kuambukizwa kwa mfano ukimkisi (denda) mtu anaweza kupata fangasi hawa kama na wewe unao.
Dawa ya fanasi kwenye mdomo na ulimi
1.Fluconazole hiini ya kumeza
2.Clotrimazole (Mycelex Troche) ni kidonge pia cha kumumunyikia mdomoni
3.Nystatin (Nystop, Nyasta) ni ya kuosha mdomo
4.Itraconazole (Sporanox) ni ya kumeza, hupewa wale wenye usugu ama wenye HIV
5.Amphotericin B (AmBisome, Fungizone) hutumika kutibu hali mbaya zaidi ya fangasi wa mdomoni.
Nini ufanye ukiwa unatumia dawa hizi
1.Piga mswaki kwa mswaki ulio mlaini
2.Badili mswaki baada ya kumaliza dozi
3.Usitumie dawa za kuosha mdomo mpaka daktari akuambie.
4.Osha mdomo kwa maji ya chumvi
5.Changanya maji na juisi ya limao kisha knywa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 web hosting 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Chini ya Tumbo langu Kuna uchungu lakini si sana shinda ni ni?
Nini kinasababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu?
Soma Zaidi...Fahamau madhara ya flagyl (Metronidazole)
Flagyl ni nini? Flagyl (metronidazole) ni antibiotic. Inapigana na bakteria katika mwili wako. Flagyl hutumiwa kutibu maambukizo ya bakteria ya uke, tumbo, ngozi, viungo na njia ya upumuaji.
Soma Zaidi...Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya ALU au kwa lugha nyingine ni dawa ya mseto
Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin
Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa.
Soma Zaidi...Matumizi ya dawa ya vidonda vya tumbo
Posti hii inahusu zaidi matumizi ya dawa za vidonda vya tumbo, ili kuweza kutumia dawa hizi ni vizuri kabisa kufuata mashariti kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...