image

Huduma ya Kwanza kwa mwenye kizunguzungu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu mwenye kizunguzungu

HUDUMA YA KWANZA KWA MWENYE KIZUNGUZUNGU

Unapokuwa na kizunguzungu unashindwa kuudhibiti mwili wako, unaweza kuanguka kabisa. Kizunguzungu kinaweza kuwa ni dalili ya tatizo flani kwenye afya ya mtu. Maradhi mengi yanahusiana na kizunguzungu, hivyo baada ya huduma ya kwanza na mgonjwa akawa hajambo ni vyema aende kituo cha afya akajuwe chanzo cha kizunguzungu:

 

Mtu mwenye kizunguzungu anaweza kujipa huduma ya kwanza mwenyewe. Vinginevyo anaweza pia kupata maelekezo kutoka kwa mtu aliye karibu naye kwani siku zote mgonjwa anakosa uwezo wa kujimilikia hasa kujipa huduma ya kwanza.

1.Kwanza mwenye kizunguzungu anatakiwa akae chini

2.Kama alikuwa akitembea ama alikuwa akifanya shuhuli yeyote anatakiwa aache na akae chini kabisa na wala asichchumae.

3.Akaechini kipolepole na katu asiharakishe

4.Kama kukaa chini hakutoshi ni vyema alale, kama anaona kama dunia inazunguka asilale kichalichali.

5.Kama anakiu mpe maji ya kutosha anywe

6.Akae sehemu iliyotuia, isiyo na fujo wala mwanga mkali wa taa ama jua

7.Ni vyema kama atapata usingizi walau kidogo

8.Kizunguzungu kikiondoka kwanza akae chini kipolepole na anapotaka kusimama asimame kipolepole na katu asitumie kitu ili kimsaidie kusimama kama fimbo





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1745


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Huduma kwa watu waliodhani wamepatwa na maambukizi.
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo utolewa kwa watu wanaodhani wamepatwa na maambukizi ya virus vya ukimwi. Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za vyakula vya vitamini Soma Zaidi...

Huduma ya kwanza kwa mwenye uchafu kwenye sikio.
Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kqa mgonjwa aliyeingiliwa na kitu au uchafu kwenye sikio. Soma Zaidi...

Namna ya kusaidia mwili kupambana na maradhi
Somo hili linakwenda kukuletea namna ambavyo mwili unapambana na maradhi Soma Zaidi...

Utaratibu wa lishe kwa wazee
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wazee Soma Zaidi...

Nna swali mimi nimefanya Romance na mtu ambaye sijampima kbsa sasa naogopa anaeza kuwa mgonjwa na mm nkaupata
Muulizaji anauliza he kula denda, ama kumbusu ama kufanya romance na muathirika was HIV na wewe uta ambukizwa? Soma Zaidi...

viapo
20. Soma Zaidi...

Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeshambuliwa na moyo na kushindwa kupumua
Kushambuliwa kwa moyo na kupumua ni kitendo Cha moyo kusimama ghafla, Hali hii unapaswa kutolewa huduma ya kwanza Ili moyo ufanye kazi tena, Soma Zaidi...

Hizi ni kazi za mapafu mwilini
Makala hii itakwenda kukufundisha kazi 5 za maafu mwilimi. Wengi tunajuwa tu kuwa mapafu yanafanya kazi ya kupumuwa. ila si hivyo tu yapo mengi zaidi. Soma Zaidi...

Faida za minyoo
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za minyoo Soma Zaidi...

Zijue kazi za ini
Post hii inahusu zaidi kazi za ini, ni kiungo muhimu kwenye mwili ambacho Kina umuhimu sana, bila ini maisha ya mwanadamu yanaweza kuishia pabaya Soma Zaidi...

Msaada kwa wenye tonsils
Posti hii inahusu zaidi msaada kwa wenye tonsils, kwa wale wenye tonsils wanapaswa kufanya yafuatayo ili kuweza kupambana na ugonjwa huu. Soma Zaidi...