Historia ya Nabii Idrisa
Katika somohili utakwenda kujifunza historia ya Nabii Idrisa (amani iwe juu yake)
Katika Quran
Nabii Idris (a.s)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a.s) katika Mitume 25 waliotajwa katika Qur-an ni Idrisa(a.s).
Nabii Idrisa(a.s) ametajwa kwa ufupi katika Qur-an
“Na mtaje Idrisa katika Kitabu (hiki). Bila shaka yeye alikuwa mkweli sana (na) Nabii. Na tulimuinua daraja ya juu kabisa.” (19:56-57).
Na (mtaje) Ismail, na Idrisa na Dhul-kifli wote walikuwa miongoni mwa wanaosubiri.” (21:85)
Katika aya hizi Nabii Idrisa(a.s) ametajwa kuwa alikuwa Nabii wa Allah(s.w) aliyepea katika ukweli na subira na Allah akamnyanyua daraja ya juu kabisa kutokana na sifa zake hizo. Hatuna taarifa zaidi ya harakati za Nabii Idrisa(a.s) katika kuhuisha Uislamu na kuusimamisha katika jamii yake, bali itoshe tu kuwa mwanaharakati anayefanya kazi ya Mitume wa Allah ya kusimamisha Uislamu katika jamii hanabudi kujipamba na tabia ya ukweli na subira.
Inasemekana kuwa nabii Idrisa:-
1. Ndiye mtu wa kwanza kuandika
2. Ndiye mtume wa kwanza kutoa darsa
3. Ndiye mtu wa kwanza kushona nguo
Katika historia
Idris alizaliwa huko Babeli, mji ulioko katika eneo la sasa la Iraq. Kabla ya kupokea Ufunuo. Idris alipokuwa mkubwa, Mungu alimtunuku Unabii. Wakati wa maisha yake, watu wote hawakuwa bado Waislamu. Baadaye, Idris aliacha mji wake wa Babeli kwa sababu idadi kubwa ya watu walitenda dhambi nyingi hata baada ya kuwaonya. Baadhi ya watu wake waliondoka na Idris. Ilikuwa vigumu kwao kuacha makazi yao.
Wanahistora waslamu wanasimulia kuwa Idris alifanywa nabii akiwa na umri wa miaka 40, sawa na umri ambao Muhammad alianza kutoa unabii, na aliishi wakati ambapo watu walikuwa wameanza kuabudu moto. Tafsiri zinapanua juu ya maisha ya Idris, na kusema kwamba nabii aligawanya muda wake katika sehemu mbili. Kwa siku tatu za wiki, Idris angehubiri kwa watu wake na kwa siku nne angejishughulisha tu na ibada ya Mungu. Wanahistora kama al-Tabari, walimpa Idris sifa ya kuwa na hekima na maarifa makubwa.
Tafsiri zinasimulia kwamba Idris alikuwa miongoni mwa "watu wa kwanza kutumia kalamu pamoja na kuwa mmoja wa watu wa kwanza kuangalia mwendo wa nyota na kuweka uzito na vipimo vya kisayansi." Ibn Arabi alimuelezea Idris kama "nabii wa wanafalsafa" na kazi kadhaa zilihusishwa naye. Baadhi ya wanazuoni waliandika tafsiri juu ya kazi hizi zinazodaiwa kuwa zake, wakati huo huo Idris pia alipewa sifa ya uvumbuzi kadhaa, ikiwa ni pamoja na sanaa ya kutengeneza mavazi.
Mfasiri Ibn Ishaq alisimulia kwamba alikuwa mtu wa kwanza kuandika kwa kalamu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Historia ya Nabii Shu'aib
atika makala hii utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Shu'aib katika Quran
Soma Zaidi...Hstora ya Nab Ishaqa katika quran
Katika post hii tutakwenda kujifunza historia ya Mtume Ishaqa
Soma Zaidi...Hstora ya Nabii Yunus
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Yunus
Soma Zaidi...Historia ya Nabii Nuhu katika Quran
Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya Mtume Nuhu kulingana na melezo yaliyo kwenye Quran
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Al-yasa’a
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Mtume Al-yasa'a
Soma Zaidi...Hstoria ya Nabii Yusuf
Katika makala hii utakwenda ujfunzakuhusu historiaya Nabii Yufuf katika Quran
Soma Zaidi...