Historia ya Nabii Idrisa

Katika somohili utakwenda kujifunza historia ya Nabii Idrisa (amani iwe juu yake)

Katika Quran

Nabii Idris (a.s)

Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a.s) katika Mitume 25 waliotajwa katika Qur-an ni Idrisa(a.s).

Nabii Idrisa(a.s) ametajwa kwa ufupi katika Qur-an


 

“Na mtaje Idrisa katika Kitabu (hiki). Bila shaka yeye alikuwa mkweli sana (na) Nabii. Na tulimuinua daraja ya juu kabisa.” (19:56-57).


 

Na (mtaje) Ismail, na Idrisa na Dhul-kifli wote walikuwa miongoni mwa wanaosubiri.” (21:85)

Katika aya hizi Nabii Idrisa(a.s) ametajwa kuwa alikuwa Nabii wa Allah(s.w) aliyepea katika ukweli na subira na Allah akamnyanyua daraja ya juu kabisa kutokana na sifa zake hizo. Hatuna taarifa zaidi ya harakati za Nabii Idrisa(a.s) katika kuhuisha Uislamu na kuusimamisha katika jamii yake, bali itoshe tu kuwa mwanaharakati anayefanya kazi ya Mitume wa Allah ya kusimamisha Uislamu katika jamii hanabudi kujipamba na tabia ya ukweli na subira.


 

Inasemekana kuwa nabii Idrisa:-
1. Ndiye mtu wa kwanza kuandika
2. Ndiye mtume wa kwanza kutoa darsa
3. Ndiye mtu wa kwanza kushona nguo

 

Katika historia

Idris alizaliwa huko Babeli, mji ulioko katika eneo la sasa la Iraq. Kabla ya kupokea Ufunuo. Idris alipokuwa mkubwa, Mungu alimtunuku Unabii. Wakati wa maisha yake, watu wote hawakuwa bado Waislamu. Baadaye, Idris aliacha mji wake wa Babeli kwa sababu idadi kubwa ya watu walitenda dhambi nyingi hata baada ya kuwaonya. Baadhi ya watu wake waliondoka na Idris. Ilikuwa vigumu kwao kuacha makazi yao.

 

Wanahistora waslamu wanasimulia kuwa Idris alifanywa nabii akiwa na umri wa miaka 40, sawa na umri ambao Muhammad alianza kutoa unabii, na aliishi wakati ambapo watu walikuwa wameanza kuabudu moto. Tafsiri zinapanua juu ya maisha ya Idris, na kusema kwamba nabii aligawanya muda wake katika sehemu mbili. Kwa siku tatu za wiki, Idris angehubiri kwa watu wake na kwa siku nne angejishughulisha tu na ibada ya Mungu. Wanahistora  kama al-Tabari, walimpa Idris sifa ya kuwa na hekima na maarifa makubwa.

 

Tafsiri zinasimulia kwamba Idris alikuwa miongoni mwa "watu wa kwanza kutumia kalamu pamoja na kuwa mmoja wa watu wa kwanza kuangalia mwendo wa nyota na kuweka uzito na vipimo vya kisayansi."  Ibn Arabi alimuelezea Idris kama "nabii wa wanafalsafa" na kazi kadhaa zilihusishwa naye. Baadhi ya wanazuoni waliandika tafsiri juu ya kazi hizi zinazodaiwa kuwa zake, wakati huo huo Idris pia alipewa sifa ya uvumbuzi kadhaa, ikiwa ni pamoja na sanaa ya kutengeneza mavazi.

 

Mfasiri Ibn Ishaq alisimulia kwamba alikuwa mtu wa kwanza kuandika kwa kalamu.

 

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: visa vya Mitume Main: Dini File: Download PDF Views 628

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Historia ya Nabii Musa

atika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Musa

Soma Zaidi...
Hstora ya Nabii Ilyasa

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Ilyasa

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Ibrahimu

Katika post hii utakwenda kujifunza historia ya Mtume Ibrahim katika quran

Soma Zaidi...
hHistoria ya Nabii Dhul-kifl

Katika makala hii tutakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Dhul-kifl

Soma Zaidi...
Hstora ya Nabii Yunus

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Yunus

Soma Zaidi...
Historia ya Nabii Shu'aib

atika makala hii utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Shu'aib katika Quran

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) wa ufup

Huu n ufupisho wa Historia ya Mtume Muhammad s.a.w. Tumekuandalia histori hii kwa urefu zaidi kwenye Makala zetu zinazofuata

Soma Zaidi...
Hstoria ya Nabii Yusuf

Katika makala hii utakwenda ujfunzakuhusu historiaya Nabii Yufuf katika Quran

Soma Zaidi...
Hstora ya Nab Sulaman

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Sulaman

Soma Zaidi...
Hstora ya Nabii Yahya

Katika somo hili uatkwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Yahya

Soma Zaidi...