picha

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 17: Hadithi ya Mtume Muhammad ﷺ kukutana na Bahira akiwa na miaka 12

Katikasomo hili utakwenda kujifunza stori maarufu ya Bahira kuhusu kukutana na Mtume Muhammad ﷺ na kumtambuwa utume wake.

KUKUTANA NA BAHIRA MWANAZUONI WA KIYAHUDI:

kuna historia stori maarufu ambayo inamuhusu Mtume Muhammad wakati ni mdogo. Hata hivyo wanahistria na baadhi ya maulamaa wamedhoofisha masimulizi haya na kusema kuwa ni stori za kutungwa kwani hazina ushahidi wa kutosheleza juu ya kutokea kwake. Stori yenyewe ni hiyo hapo chini:- 


Mzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Sikumoja wakati Mtume alipokuwa na umri wa miaka kumna mbili (12) alitoka yeye na kijana wake kuelekea Sham (Syria) kwa ajili ya kufanya biashra. Basi walipofika sehemu inayoitwa Busra walikutana na kuhani mmoja wa kiyahudi aliyeitwa Bahira na inasemekana jina lake halisi ni George (Joji kwa matamshi ya kiswahili). Mtu huyu aliwaonesha ukaribu mkubwa sana, a katu hajawahi kuonesha ukarimu huu kwao watu hawa kwani walikuwa ni wageni kwake.



Bahira aliushika mkono wa Mtume na akasema “huyu ndiye kiongozi wa watu wote, Allah atamtuma kwa kumpa ujumbe ambao utakuwa ni rehma kwa viumbe wote” hapa mzee Abu Talib akamuuliza “umejuaje jambo hili” Mzee huyu akajibu kwa kumwambia “mlipokuwa mnakuja alipotokea upade wa Aqabah niliona miti na majabali vyote vinamsujudia (yaani vinampa heshima) na huwa vitu hivi havifanyi hivi ila kwa mitume tu. Pia naweza kumjuwa kwa kuwa ana mhuri wa mitume chini ya bega lake kama tunda la tofaha (epo) yote haya tumeyasoma kwenye vitabu vya dini yetu”



Baada ya mazungumzo Bahira akamwambia mzee Abu Talib amrudishe kijana Makkah kwani Bahira alihofia kuwa watu wa huko wendako huenda wakamgunduwa kuwa huyu atakujakuwa mtume wa mwisho hivyo wakamfanyia hasadi na kumuua. Kwani Mayahudi walikuwa wakihubiri kuhusu Mtume wa Mwisho lakini walitarajia kuwa atatokea miongoni mwa kabila lao hivyo wakitambua kuwa Mtume wa Mwisho ni Muarabu wanaweza kumuuwa kama walivyowauwa mitume wao huko nyuma. Basi mzee Abu talib alitii na kumrudisha kijana wake Makkah. 



Wanazuoni wa sirah wanazungumza maelezo mengi kuhusu habari hii ya Bahirah na Kijana Muhammad. Wapo wanaoeleza kuwa Bahira baada ya kutamka maneno ya kuwa huyu kijana atakujakuwa ni mtume alitaka kujiridhisha zaidi hivyo akaanza mazungumzo na kijana ili aweze kubaini mengi zaidi. Basi katika mazungumzo yake Bahira alisema “Nakuapia kwa Mungu Lata na Uzza” bahira alitambuwa kuwa Lata na Uzza ni miungu wa washirikina wa Makkah hivyo Mtume hatavumilia maneno haya. Basi kijana Muhammad aliposikia maneno yake akamwambia “Usitaje Lata na Uza mbele yangu, ninawachukia” Kufika hapa Bahira akawa amejiridhisha kabisa kuwa huyu ndiye Mtume wa Mwisho.



Katika masimulizi mengine ni kuwa Bahira alikaribisha msafara mmoja wa kibiashara kwenye tafrija yake. Msafara huu ndio ulikuwa msafara wa Abu Talib na wenzie. Basi bahira akawaambia watu wote waingie ndani kwenye tafrija isipokuwa hyuy mtoto (Muhammad) abakie nje ili kulinda mizigo. Basi wakati tafrija inaendelea bahira akaanza kuona miujiza kama Kusujudi kwa mitu (kutoa heshima) na kufunikwa na mawingu wakati kwa ajili ya kivuli. Hapo ndipo Bahira akatambua kuwa huyu ni Mtume.



Na hapo ndipo alipomsahuri mzee Abu talib kuwa kijana huyu asiendenae huko Syria kwani mayahudi wakimjuwa watamuua. Mzee abu Talib alitii ushauri huu hivyo akauza bidhaa zake paleple kwa bei iliyo nafuu ili aweze kurudi zake Makkah. Abu Talib safari yake ya biashara ikaishia palepale bila ya kufika Syria.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-07-28 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 909

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 web hosting    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 6: Nasaba ya Mtume Muhammaﷺ

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Nasaba ya Mtume Muhammad ﷺ toka kwa wazazi wake Mpaka kwa Nabii Ibrahim

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 41: Mbinu za kukomesha kuenea kwa uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza mambo yaliyofanyika katika harakati za kukomesha kuenea kwa uislamu.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 29: Amri za kwanza alizopewa Mtume Muhammad ﷺ

Katika somo hili utajifunza amri ambazo alipewa Mtume Muhammad ﷺ mwanzoni kabisa mwa kazi yake ya Kulingania dini

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 27: Kushuka tena kwa Wahyi

Baada ya kukatika kwa Wahyi kwa muda wa masiku kadhaa hatimaye Jibril akaleta tena wahyi kwa mara nyingine.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 37: Amri ya kulingania watu wote kwenye Mlima As-Safa

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu amri ya kulingania wtu wote, yale yaliyojiri katika mkutano wa kwanza na laana ya Abu Lhab. TUkio hili lilianyika katika mlima As-safa

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 64: Ndoa ya Mtume Muhammad baada ya Khadija

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu Ndoa Mtume Muhammad baada ya Bi Khadija alimuoa Sauda kisha Aisha

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 44: Historia fupi ya Mke wa Abu Lahab - Arwā bint Ḥarb

Katika somo hili utakwenda kujifunza kwa ufupi historia ya mmoja katika maadui wakubwa wa Uislamu wakati Mtume alipokuwa analingania dini.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 51: Maquarish wanamuendea tena Mzee Abu Talib

Baada ya Maquraish kufeli mpango wao wa kuwarejesha Wahamiaji, wakaamuwa wafanye mbinu nyingine kwa ajili ya kuzuia harakati za Mtume Muhammad

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 40: Historia fupi ya Walib Ibn Al-Mughira

Katika somo hili utajifunza kuhusu mmoja katika maadui wakubwa wa Mtume Muhammad wakati akilingania watu.

Soma Zaidi...