Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 17: Hadithi ya Mtume Muhammad ﷺ kukutana na Bahira akiwa na miaka 12

Katikasomo hili utakwenda kujifunza stori maarufu ya Bahira kuhusu kukutana na Mtume Muhammad ﷺ na kumtambuwa utume wake.

KUKUTANA NA BAHIRA MWANAZUONI WA KIYAHUDI:

kuna historia stori maarufu ambayo inamuhusu Mtume Muhammad wakati ni mdogo. Hata hivyo wanahistria na baadhi ya maulamaa wamedhoofisha masimulizi haya na kusema kuwa ni stori za kutungwa kwani hazina ushahidi wa kutosheleza juu ya kutokea kwake. Stori yenyewe ni hiyo hapo chini:- 


Mzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Sikumoja wakati Mtume alipokuwa na umri wa miaka kumna mbili (12) alitoka yeye na kijana wake kuelekea Sham (Syria) kwa ajili ya kufanya biashra. Basi walipofika sehemu inayoitwa Busra walikutana na kuhani mmoja wa kiyahudi aliyeitwa Bahira na inasemekana jina lake halisi ni George (Joji kwa matamshi ya kiswahili). Mtu huyu aliwaonesha ukaribu mkubwa sana, a katu hajawahi kuonesha ukarimu huu kwao watu hawa kwani walikuwa ni wageni kwake.



Bahira aliushika mkono wa Mtume na akasema “huyu ndiye kiongozi wa watu wote, Allah atamtuma kwa kumpa ujumbe ambao utakuwa ni rehma kwa viumbe wote” hapa mzee Abu Talib akamuuliza “umejuaje jambo hili” Mzee huyu akajibu kwa kumwambia “mlipokuwa mnakuja alipotokea upade wa Aqabah niliona miti na majabali vyote vinamsujudia (yaani vinampa heshima) na huwa vitu hivi havifanyi hivi ila kwa mitume tu. Pia naweza kumjuwa kwa kuwa ana mhuri wa mitume chini ya bega lake kama tunda la tofaha (epo) yote haya tumeyasoma kwenye vitabu vya dini yetu”



Baada ya mazungumzo Bahira akamwambia mzee Abu Talib amrudishe kijana Makkah kwani Bahira alihofia kuwa watu wa huko wendako huenda wakamgunduwa kuwa huyu atakujakuwa mtume wa mwisho hivyo wakamfanyia hasadi na kumuua. Kwani Mayahudi walikuwa wakihubiri kuhusu Mtume wa Mwisho lakini walitarajia kuwa atatokea miongoni mwa kabila lao hivyo wakitambua kuwa Mtume wa Mwisho ni Muarabu wanaweza kumuuwa kama walivyowauwa mitume wao huko nyuma. Basi mzee Abu talib alitii na kumrudisha kijana wake Makkah. 



Wanazuoni wa sirah wanazungumza maelezo mengi kuhusu habari hii ya Bahirah na Kijana Muhammad. Wapo wanaoeleza kuwa Bahira baada ya kutamka maneno ya kuwa huyu kijana atakujakuwa ni mtume alitaka kujiridhisha zaidi hivyo akaanza mazungumzo na kijana ili aweze kubaini mengi zaidi. Basi katika mazungumzo yake Bahira alisema “Nakuapia kwa Mungu Lata na Uzza” bahira alitambuwa kuwa Lata na Uzza ni miungu wa washirikina wa Makkah hivyo Mtume hatavumilia maneno haya. Basi kijana Muhammad aliposikia maneno yake akamwambia “Usitaje Lata na Uza mbele yangu, ninawachukia” Kufika hapa Bahira akawa amejiridhisha kabisa kuwa huyu ndiye Mtume wa Mwisho.



Katika masimulizi mengine ni kuwa Bahira alikaribisha msafara mmoja wa kibiashara kwenye tafrija yake. Msafara huu ndio ulikuwa msafara wa Abu Talib na wenzie. Basi bahira akawaambia watu wote waingie ndani kwenye tafrija isipokuwa hyuy mtoto (Muhammad) abakie nje ili kulinda mizigo. Basi wakati tafrija inaendelea bahira akaanza kuona miujiza kama Kusujudi kwa mitu (kutoa heshima) na kufunikwa na mawingu wakati kwa ajili ya kivuli. Hapo ndipo Bahira akatambua kuwa huyu ni Mtume.



Na hapo ndipo alipomsahuri mzee Abu talib kuwa kijana huyu asiendenae huko Syria kwani mayahudi wakimjuwa watamuua. Mzee abu Talib alitii ushauri huu hivyo akauza bidhaa zake paleple kwa bei iliyo nafuu ili aweze kurudi zake Makkah. Abu Talib safari yake ya biashara ikaishia palepale bila ya kufika Syria.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 725

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 19: Hilf al-Fudul - makataba wa haki

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya mkataba wa al-Fudhul na matokeo yake katika kusimamaia haki za wafanyabiashara.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 56: Abu Talib Awaunganisha Bani Hashim na Bani Al-Muttalib kwa Ulinzi wa Mtume (SAW)

Wana wa Abd Manaf wanaungana kumlinda Mtume Muhammad isipokuwa Abu Lahab yeye amekataa kuungana na ndugu zake.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 41: Mbinu za kukomesha kuenea kwa uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza mambo yaliyofanyika katika harakati za kukomesha kuenea kwa uislamu.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 38: Taharuki yaingia Mjini Mkkah

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu yaliyotokea baada ya watu wa Mkkah kulinganiwa kwenye dini kwa mara ya kwanza

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 14: Historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 34: Amri ya kulingnia dini kwa uwazi

Katika somo hili utajifunz akuhusu amri ya kulingania dini bila ya kificho, baada ya kulingania kwa siri kwa miaka mitatu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 16: Historia ya Abu Talib

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya Abu Talib ibn Abd al-Muttalib ambaye ni baba yae mkubwa Mtume ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 20: Kazi alizokuwa akifanya Mtume MUhammad kabla yautume

Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi ambazo alikuwa akifanya Mtume Muhammad ﷺ kabla ya kupewa utume

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 33: Mquraishi wanagunduwa kuhusu dini Mpya

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo wito wa ulingano ulipoenea na kuwafikia maquraish na washirikina

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 45: Mkakati wa kuficha imani kwa Waslamu wapya

Katika somo hili utakwend akujifunza mkakati uliohusu kuficha imani ya uislamu kimatendo na kimaneno kwa kuhofia mateso ya Makafiri dhidi ya Waumini wapya

Soma Zaidi...