Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 17: Hadithi ya Mtume Muhammad ﷺ kukutana na Bahira akiwa na miaka 12

Katikasomo hili utakwenda kujifunza stori maarufu ya Bahira kuhusu kukutana na Mtume Muhammad ﷺ na kumtambuwa utume wake.

KUKUTANA NA BAHIRA MWANAZUONI WA KIYAHUDI:

kuna historia stori maarufu ambayo inamuhusu Mtume Muhammad wakati ni mdogo. Hata hivyo wanahistria na baadhi ya maulamaa wamedhoofisha masimulizi haya na kusema kuwa ni stori za kutungwa kwani hazina ushahidi wa kutosheleza juu ya kutokea kwake. Stori yenyewe ni hiyo hapo chini:- 


Mzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Sikumoja wakati Mtume alipokuwa na umri wa miaka kumna mbili (12) alitoka yeye na kijana wake kuelekea Sham (Syria) kwa ajili ya kufanya biashra. Basi walipofika sehemu inayoitwa Busra walikutana na kuhani mmoja wa kiyahudi aliyeitwa Bahira na inasemekana jina lake halisi ni George (Joji kwa matamshi ya kiswahili). Mtu huyu aliwaonesha ukaribu mkubwa sana, a katu hajawahi kuonesha ukarimu huu kwao watu hawa kwani walikuwa ni wageni kwake.



Bahira aliushika mkono wa Mtume na akasema “huyu ndiye kiongozi wa watu wote, Allah atamtuma kwa kumpa ujumbe ambao utakuwa ni rehma kwa viumbe wote” hapa mzee Abu Talib akamuuliza “umejuaje jambo hili” Mzee huyu akajibu kwa kumwambia “mlipokuwa mnakuja alipotokea upade wa Aqabah niliona miti na majabali vyote vinamsujudia (yaani vinampa heshima) na huwa vitu hivi havifanyi hivi ila kwa mitume tu. Pia naweza kumjuwa kwa kuwa ana mhuri wa mitume chini ya bega lake kama tunda la tofaha (epo) yote haya tumeyasoma kwenye vitabu vya dini yetu”



Baada ya mazungumzo Bahira akamwambia mzee Abu Talib amrudishe kijana Makkah kwani Bahira alihofia kuwa watu wa huko wendako huenda wakamgunduwa kuwa huyu atakujakuwa mtume wa mwisho hivyo wakamfanyia hasadi na kumuua. Kwani Mayahudi walikuwa wakihubiri kuhusu Mtume wa Mwisho lakini walitarajia kuwa atatokea miongoni mwa kabila lao hivyo wakitambua kuwa Mtume wa Mwisho ni Muarabu wanaweza kumuuwa kama walivyowauwa mitume wao huko nyuma. Basi mzee Abu talib alitii na kumrudisha kijana wake Makkah. 



Wanazuoni wa sirah wanazungumza maelezo mengi kuhusu habari hii ya Bahirah na Kijana Muhammad. Wapo wanaoeleza kuwa Bahira baada ya kutamka maneno ya kuwa huyu kijana atakujakuwa ni mtume alitaka kujiridhisha zaidi hivyo akaanza mazungumzo na kijana ili aweze kubaini mengi zaidi. Basi katika mazungumzo yake Bahira alisema “Nakuapia kwa Mungu Lata na Uzza” bahira alitambuwa kuwa Lata na Uzza ni miungu wa washirikina wa Makkah hivyo Mtume hatavumilia maneno haya. Basi kijana Muhammad aliposikia maneno yake akamwambia “Usitaje Lata na Uza mbele yangu, ninawachukia” Kufika hapa Bahira akawa amejiridhisha kabisa kuwa huyu ndiye Mtume wa Mwisho.



Katika masimulizi mengine ni kuwa Bahira alikaribisha msafara mmoja wa kibiashara kwenye tafrija yake. Msafara huu ndio ulikuwa msafara wa Abu Talib na wenzie. Basi bahira akawaambia watu wote waingie ndani kwenye tafrija isipokuwa hyuy mtoto (Muhammad) abakie nje ili kulinda mizigo. Basi wakati tafrija inaendelea bahira akaanza kuona miujiza kama Kusujudi kwa mitu (kutoa heshima) na kufunikwa na mawingu wakati kwa ajili ya kivuli. Hapo ndipo Bahira akatambua kuwa huyu ni Mtume.



Na hapo ndipo alipomsahuri mzee Abu talib kuwa kijana huyu asiendenae huko Syria kwani mayahudi wakimjuwa watamuua. Mzee abu Talib alitii ushauri huu hivyo akauza bidhaa zake paleple kwa bei iliyo nafuu ili aweze kurudi zake Makkah. Abu Talib safari yake ya biashara ikaishia palepale bila ya kufika Syria.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 551

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) somo la 1: Asili ya Waarabu

Katika somo hili utakwenda kujifunza Asili ya waarabu na kusambaa kwao katika bara arab

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 45: Mkakati wa kuficha imani kwa Waslamu wapya

Katika somo hili utakwend akujifunza mkakati uliohusu kuficha imani ya uislamu kimatendo na kimaneno kwa kuhofia mateso ya Makafiri dhidi ya Waumini wapya

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 54: Kusilimu kwa Umar bin Al- Khattab

Hii ni historia fupi ya kuslimu kwa Umar na kuanza kwa taswira mpya ya waislamu na uislamu katika mji wa makkah

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 11: Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa

Katika somo hili utajifunza kuhusu Mtume MUhammad ﷺ kulelewa na Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa:

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 6: Nasaba ya Mtume Muhammaﷺ

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Nasaba ya Mtume Muhammad ﷺ toka kwa wazazi wake Mpaka kwa Nabii Ibrahim

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 7: Kuzaliwa kwa Mtume MUhammad ﷺ

katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Mazazi ya Mtume MUhammad ﷺ na kupewa jina.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 20: Kazi alizokuwa akifanya Mtume MUhammad kabla yautume

Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi ambazo alikuwa akifanya Mtume Muhammad ﷺ kabla ya kupewa utume

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 8: Kulelewa kwa Mtume Muhammad ﷺ na Halima

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuusu malezi na makuzi ya Mtume Muhammad ﷺ akiwa kwa bibi Halima

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 44: Historia fupi ya Mke wa Abu Lahab - Arwā bint Ḥarb

Katika somo hili utakwenda kujifunza kwa ufupi historia ya mmoja katika maadui wakubwa wa Uislamu wakati Mtume alipokuwa analingania dini.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 16: Historia ya Abu Talib

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya Abu Talib ibn Abd al-Muttalib ambaye ni baba yae mkubwa Mtume ﷺ

Soma Zaidi...