picha

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 14: Historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ

Amina bint Wahb ibn Abd Manaf al-Zuhriyya

Amina bint Wahb ibn Abd Manaf al-Zuhriyya (Kiarabu: آمِنَة بِنْت وَهْب, kwa kilatini: ʾĀmina bint Wahb, takriban 549–577) alikuwa mama wa Mtume wa Kiislamu Muhammad. Alitoka katika kabila la Banu Zuhra.

 

Maisha ya Awali na Ndoa:

Aminah alizaliwa kwa Wahb ibn Abd Manaf na Barrah bint 'Abd al-'Uzzā ibn 'Uthmān ibn 'Abd al-Dār huko Maka. Kabila lake, Quraysh, linasemekana kuwa wazao wa Ibrahim (Abraham) kupitia mwanawe Isma'il (Ishmael). Mwana wao Zuhrah alikuwa kaka mkubwa wa Qusayy ibn Kilab, babu wa Abdullah ibn Abdul-Muttalib, na msimamizi wa kwanza wa Qurayshi wa Kaaba. Abd al-Muttalib alipendekeza ndoa ya mtoto wake mdogo Abdullah na Aminah. Vyanzo vingine vinasema kuwa baba wa Aminah alikubali pendekezo (posa) hilo; vingine vinasema kuwa alikuwa ni mjomba wa Aminah, Wuhaib, ambaye alikuwa mlezi wake. Wawili hao walifunga ndoa muda mfupi baadaye. Abdullah alitumia muda mwingi wa ujauzito wa Aminah akiwa mbali nyumbani kama sehemu ya msafara wa wafanyabiashara na alikufa kwa ugonjwa kabla ya kuzaliwa kwa mwanawe huko Medina.

 

Kuzaliwa kwa Muhammad na Miaka ya Baadaye:

Miezi mitatu baada ya kifo cha Abdullah, mwaka 570–571 BK, Muhammad alizaliwa. Kama ilivyokuwa desturi miongoni mwa familia zote kubwa wakati huo kutafuta wanyonyeshaji na waleaji wa watoto wao kutoka mashambani, ili wapate kujuwa lugha kwa ufasaha, waepuke na magonjwa yanayozuka mijini, wawe na ukakamavu, na wajifunze tabia njema. Aminah Hivyo Muhammad alichukuliwa na Halima kwa ajili ya kulelewa. Imani ilikuwa kwamba jangwani, mtu angejifunza nidhamu binafsi, heshima, na uhuru. Wakati huu, Muhammad alinyonyeshwa na Halimah bint Abi Dhuayb, mwanamke maskini wa Bedouin kutoka kabila la Banu Sa'ad, tawi la Hawāzin.

 

Muhammad alipokuwa na umri wa miaka sita, alikutanishwa tena na Aminah, ambaye alimpeleka kumtembelea jamaa zake huko Yathrib (baadaye Medina). Waliporudi Maka mwezi mmoja baadaye, wakiwa na mtumishi wake, Umm Ayman, Aminah aliugua. Alikufa karibu mwaka 577 au 578, na alizikwa katika kijiji cha Al-Abwa'. Kaburi lake lilivunjwa mwaka 1998. Sababu ya kuvunjwa kwa makaburi mengi ni imani ya kuwa kuna watu walikuwa wanafanya ibada kwenye makaburi haya ama wengine walikuwa wakiyaomba. Hivyo fatuwa iliyotolewa na wanazuoni wa Sudia ni kuwa haya yote yanayofanywa ni bidaa na ni shirk. Hivyo makaburi mengi yalivunjwa na kuwa katika hali ya kawaida. Muhammad  alichukuliwa kwanza na babu yake wa upande wa baba, Abd al-Muttalib, mwaka 577, na baadaye na baba yake mkubwa Abu Talib ibn Abd al-Muttalib.

 

Hatima katika Akhera:

 Wanazuini wengi wa kiislamu bado wana hitilafu juu ya kuwa wazazi wa Mtume ni watu wa peponi ama wa motoni. Kuna hadithi nyingi zinanukuliwa hata hivyo wachambuwa wa hadithi wamedhoofisha nyingi katika hadithi hizo. na Nyinine zimepewa sifa ya kuwa ni za uwongo kabisa. Hivyo basi jambo hili tumuachie Allah.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-08-02 12:23:32 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Masomo File: Download PDF Views 1505

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 53: Kuslimu kwa Hamza bin Abdul-Muttalib

Hapa utajifunza historia ya kuslimu kwa Hamzah bin Abdul-Muttalib.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 60: Kulingania Uislamu nje ya Makkah

Mwaka wa 10 toka kupata utume, Mtume Muhammad (S.A.W) anaanza kulingania dini nje ya Mji wa Makkah

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 48: Hijra ya kwanza kuelekea Ethiopia

Katika somo hiliutajifunza kuhusu Hijra ya Kwanz ana ya Pili kuelekea Ethiopia na mambo yaliyojitokeza.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 2: Historia ya watu wa kabila la Quraysh na familia ya Mtume Muhammad (s.a.w)

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya kabila la Quraysh Mka na Familia ya Mtume MUhammad (s.a.w)

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 19: Hilf al-Fudul - makataba wa haki

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya mkataba wa al-Fudhul na matokeo yake katika kusimamaia haki za wafanyabiashara.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 12: Historia fupi ya Salma bint Amir mama Abdul Muttalib

Katika somo hili utawenda kujifunza Historia fupi ya Salma bint Amir mama wa babu yake Mtume Muhammad kwa upande wa baba

Soma Zaidi...