Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ
Amina bint Wahb ibn Abd Manaf al-Zuhriyya
Amina bint Wahb ibn Abd Manaf al-Zuhriyya (Kiarabu: آمِنَة بِنْت وَهْب, kwa kilatini: ʾĀmina bint Wahb, takriban 549–577) alikuwa mama wa Mtume wa Kiislamu Muhammad. Alitoka katika kabila la Banu Zuhra.
Maisha ya Awali na Ndoa:
Aminah alizaliwa kwa Wahb ibn Abd Manaf na Barrah bint 'Abd al-'Uzzā ibn 'Uthmān ibn 'Abd al-Dār huko Maka. Kabila lake, Quraysh, linasemekana kuwa wazao wa Ibrahim (Abraham) kupitia mwanawe Isma'il (Ishmael). Mwana wao Zuhrah alikuwa kaka mkubwa wa Qusayy ibn Kilab, babu wa Abdullah ibn Abdul-Muttalib, na msimamizi wa kwanza wa Qurayshi wa Kaaba. Abd al-Muttalib alipendekeza ndoa ya mtoto wake mdogo Abdullah na Aminah. Vyanzo vingine vinasema kuwa baba wa Aminah alikubali pendekezo (posa) hilo; vingine vinasema kuwa alikuwa ni mjomba wa Aminah, Wuhaib, ambaye alikuwa mlezi wake. Wawili hao walifunga ndoa muda mfupi baadaye. Abdullah alitumia muda mwingi wa ujauzito wa Aminah akiwa mbali nyumbani kama sehemu ya msafara wa wafanyabiashara na alikufa kwa ugonjwa kabla ya kuzaliwa kwa mwanawe huko Medina.
Kuzaliwa kwa Muhammad na Miaka ya Baadaye:
Miezi mitatu baada ya kifo cha Abdullah, mwaka 570–571 BK, Muhammad alizaliwa. Kama ilivyokuwa desturi miongoni mwa familia zote kubwa wakati huo kutafuta wanyonyeshaji na waleaji wa watoto wao kutoka mashambani, ili wapate kujuwa lugha kwa ufasaha, waepuke na magonjwa yanayozuka mijini, wawe na ukakamavu, na wajifunze tabia njema. Aminah Hivyo Muhammad alichukuliwa na Halima kwa ajili ya kulelewa. Imani ilikuwa kwamba jangwani, mtu angejifunza nidhamu binafsi, heshima, na uhuru. Wakati huu, Muhammad alinyonyeshwa na Halimah bint Abi Dhuayb, mwanamke maskini wa Bedouin kutoka kabila la Banu Sa'ad, tawi la Hawāzin.
Muhammad alipokuwa na umri wa miaka sita, alikutanishwa tena na Aminah, ambaye alimpeleka kumtembelea jamaa zake huko Yathrib (baadaye Medina). Waliporudi Maka mwezi mmoja baadaye, wakiwa na mtumishi wake, Umm Ayman, Aminah aliugua. Alikufa karibu mwaka 577 au 578, na alizikwa katika kijiji cha Al-Abwa'. Kaburi lake lilivunjwa mwaka 1998. Sababu ya kuvunjwa kwa makaburi mengi ni imani ya kuwa kuna watu walikuwa wanafanya ibada kwenye makaburi haya ama wengine walikuwa wakiyaomba. Hivyo fatuwa iliyotolewa na wanazuoni wa Sudia ni kuwa haya yote yanayofanywa ni bidaa na ni shirk. Hivyo makaburi mengi yalivunjwa na kuwa katika hali ya kawaida. Muhammad alichukuliwa kwanza na babu yake wa upande wa baba, Abd al-Muttalib, mwaka 577, na baadaye na baba yake mkubwa Abu Talib ibn Abd al-Muttalib.
Hatima katika Akhera:
Wanazuini wengi wa kiislamu bado wana hitilafu juu ya kuwa wazazi wa Mtume ni watu wa peponi ama wa motoni. Kuna hadithi nyingi zinanukuliwa hata hivyo wachambuwa wa hadithi wamedhoofisha nyingi katika hadithi hizo. na Nyinine zimepewa sifa ya kuwa ni za uwongo kabisa. Hivyo basi jambo hili tumuachie Allah.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Hatimaye Mtume Muhammad ﷺ anarejea Makkah na kuendelea na kazi yake
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza mambo yaliojiri katika kikao kilicho andaliwa kwa ajili ya kumuuwa Mtue Muhammad s.a.w. Katika kikao hiki mpaka Iblis alihudhuria
Soma Zaidi...Katikasomo hili utakwenda kujifunza stori maarufu ya Bahira kuhusu kukutana na Mtume Muhammad ﷺ na kumtambuwa utume wake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu yaliyotokea baada ya watu wa Mkkah kulinganiwa kwenye dini kwa mara ya kwanza
Soma Zaidi...Baada ya kukatika kwa Wahyi kwa muda wa masiku kadhaa hatimaye Jibril akaleta tena wahyi kwa mara nyingine.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuusu historia ya mmoja katika maswahaba wa mwanzoni na mwenye mchango mkubwa sana katika uislamu ambaye ni Al-Arqam ibn Abi al-Arqam
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza mkakati uliohusu kuficha imani ya uislamu kimatendo na kimaneno kwa kuhofia mateso ya Makafiri dhidi ya Waumini wapya
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya wazazi wa Mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza mchango mkubwa wa nyumba ya Arqam Ibn Abi AL Arqam katika historia nzima ya Uislamu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya Abu Talib ibn Abd al-Muttalib ambaye ni baba yae mkubwa Mtume ﷺ
Soma Zaidi...