Jinsi ya kumuosha maiti wa kiislami mwanaume au mwanamke


image


Post hii inakwenda kukufundisha hatuwa kwa hatuwa jinsi ya kumuosha maiti wa kiislamu


Kumuosha Maiti

 

Kumuosha maiti ni Faradh Kifaya. Maiti hawezi kuswaliwa mpaka akoshwe kwanza kama vile ilivyo haramu kuswali bila ya kuwa twahara. Ni maiti ya Muislamu aliyekufa shahidi katika vita vya kupigania Uislamu tu ndiye anayezikwa hivyo hivyo na damu zake bila ya kuoshwa kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
“Ibn Abbas (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alipitisha amri juu ya watu waliokufa katika vita vya Uhud kuwa nguo zao za chuma na ngozi walizovalia zinaweza kuvuliwa bali wazikwe hivyo hivyo na damu pamoja na nguo zao nyingine za kawaida.” (Abu Daud, Ibn Majah).

 

1. Maiti ya kiume ioshwe na wanaume na maiti ya kike ioshwe na wanawake. Watoto wadogo wanaweza kuoshwa na wanaume au wanawake.Pia ni Sunnah mke kumuosha mumewe na mume kumuosha mkewe.
2. Ni mtu mmoja tu anayeosha na mwingine/wengine wa kumpa msaada pale atakapohitajia.
3. Ni muhimu muoshaji ayafahamu masharti ya kuosha maiti ya Muislamu yafutayo:
4. Muoshaji awe Muislamu.
5. Mahali pa kuoshea pawe faragha - panaweza kuwa bafuni, au sehemu ya ua uliojengwa maalumu kwa kazi hiyo au hata chumbani kama wafanyavyo watu wengi.
6. Maiti ioshwe huku imefunikwa gubi-gubi kwa nguo nyepesi inayoruhusu maji kupenyeza.
7. Muoshaji asiishike maiti bali aoshe akiwa amevaa gloves.
8. Kuchunga yale masharti yote yanayopaswa yatekelezwe na mwenye kukoga josho la wajibu kama vile kuwa na maji safi ya kutosha, pasiwe na kizuizi cha kuzuia maji kupenyeza mwili wa maiti.

 

Ni muhimu muoshaji afahamu nguzo na Sunnah za kuosha maiti. Nguzo za kuosha ni mbili:
(i)Nia.
(ii)Kueneza maji mwili mzima wa maiti.

 


Ni sunnah kumuosha maiti mara tatu au zaidi ya hivyo. Lakini katika idadi ya witri kama tunavyojifunza katika hadithi ifuatayo:

 


Ummu Atiyyah (r.a) amesimulia kuwa: Mtume wa Allah alitujia tulip okuwa tukimuosha (marehemu) binti yake (Zainab r.a). alisema: Muosheni mara tatu au mara tano au zaidi ya hapo kama mtaona hapana budi kufanya hivyo kwa maji ya mkunazi (lot tree) na w ekeni kafuri (karafuu maiti) au kitu kama hicho kwenye maungio (joints). Mtakapo maliza niiteni. Kwa

 

hiyo baada ya kumaliza tulimwita. Alitupa shuka yake ya kiunoni na kutuambia: Mfunikeni nayo. Katika maelezo mengine, Mtume (s.a.w) alisema: Muosheni katika witri mara tatu, au mara tano, au mara saba na anzeni na upande wake w a kulia na viungo vya kutaw adha. Akasema (Ummu Atiyah): Tulimuosha nywele zake mara tatu na kisha tukamlaza chali (kwa mgongo). (Bukhari na Muslim)

 


Namna ya Kuosha Maiti hatua kwa hatua
1.Maiti awekwe juu ya kitanda chenye tobo katikati la kupitishia uchafu utokao tumboni kama upo.

 


2.Lichimbwe shimo (ufuo) usawa wa tobo la kitanda, la kuhifadhi uchafu utakao toka kwa maiti. Iwapo hapana uwezekano wa kutengeneza ufuo, pawekwe kitu cha kukinga uchafu badala yake. Anaweza kuoshewa bafuni. Maiti ifunikwe nguo moja kubwa, iliyo nyepesi kiasi cha kuruhusu maji kupita.

 


3.Maiti ikalishwe kitako juu ya hicho kitanda na makalio yake yawe sawa sawa na hilo tobo la kitanda na ufuo chini yake na iinamishwe kidogo nyuma. Kama ni maiti ya mtu mzima ni vyema msaidizi wa mwoshaji amuegemeze maiti kwa goti lake.

 


4.Mwoshaji apitishe mkono wake wa kushoto juu ya tumbo la maiti aliminyeminye kwa taratibu ili utoke uchafu uliomo humo ndani.

 


5.Amlaze chali na amminyeminye tumbo lake kama hapo awali.

 


6.Aikalishe tena kisha apitishe mkono wake wa kushoto chini, ukiwa umevalishwa gloves asafishe tupu mbili huku anajimiminia maji kwa mkono wa kulia mpaka atakate.

 

7.Muoshaji, baada ya hapo, azungurushe kitambaa kwenye kidole cha shahada cha mkono wa kushoto, akichovye majini, kisha amswakishe maiti vizuri meno ya juu na ya chini, kisha akitupe ufuoni.

 


8.Azungurushe kitambaa kingine kwenye kidole kidogo cha mkono wa kushoto, akichovye majini, kisha amsafishe kwacho tundu za pua, kisha akitupe ufuoni.

 


9.Achukue kijiti laini achokonoe kucha zake maiti, iwapo ni ndefu na chafu.

 


10.Akiwa pia amemkalisha, amtawadhishe maiti kwa kufuata utaratibu wa kawaida wa kutawadha. Lakini wakati wa kumwosha uso, amuinamishe mbele kidogo ili maji yasimwingie ndani.

 

11.Maiti akiwa katika hali hiyo hiyo ya kukaa, mwoshaji ataanza kumwosha kichwa huku akiwa amemuinamisha kwa mbele. Kama nywele ni nyingi zichanwe panapo uwezekano na zioshwe kwa sabuni. Kisha maji yamiminwe mpaka povu la sabuni liishe. Nywele na ndevu zichanwe vizuri na mwanamke mwenye nywele nyingi asukwe mikia.

 

12. Nywele zitakazong’oka ziambatanishwe na sanda.

 


13.Baada ya kuoshwa kichwa, maiti alazwe kwa ubavu wa kushoto, kisha kuanza kumwosha ubavu wa kulia kwa kumiminia maji mbele na nyuma pamoja na kusugua kwa sabuni. Kisha kummiminia maji mengi mpaka povu liishe.

 


14.Kisha maiti atalazwa kwa ubavu wa kulia na kuoshwa ubavu wa kushoto kama ilivyofanyika kwa ubavu wa kulia.

 


15.Baada ya makosho haya mawili - la maji na sabuni na la kuondoa sabuni, pawe na kosho la tatu la maji yaliyowekwa karafuu maiti na marashi kidogo. Karafuu maiti inasaidia kulegeza maungio na kufanya mwili wa maiti usitepete.

 


16.Baada ya makosho haya matatu, mwoshaji anyooshe viungo vya maiti na kumlaza sawasawa kama alivyolazwa mara baada ya kufa, kisha achukue nguo kavu na kumfuta maiti kama mtu anavyojifuta kwa taulo baada ya kukoga. Kisha maiti awekwe juu ya mkeka mkavu na afunikwe nguo kubwa kavu tayari kwa kupambwa na kuvalishwa sanda.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Zijuwe nguzo 17 za swala.
Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala. Soma Zaidi...

image Utaratibu wa kuzuru makaburi na dua zinazosomwa wakati wa kuzuru kaburi
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika katika kuzuru kaburi la muislamu. Soma Zaidi...

image Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja. Soma Zaidi...

image Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu. Soma Zaidi...

image Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini
Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Sera ya uchumi katika uislamu
Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu. Soma Zaidi...

image Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi
Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki. Soma Zaidi...

image Faida na umuhimu wa nfoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...

image Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

image Vipi utapata uchamungu kupitia funga
Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu. Soma Zaidi...