Hadithi Ya 38: Anayeonyesha Uadui Kwa Rafiki Yangu Mtiifu Ninatangaza Vita Dhidi Yake
Hadithi Ya 38: Anayeonyesha Uadui Kwa Rafiki Yangu Mtiifu Ninatangaza Vita Dhidi Yake
الحديث الثامن والثلاثون
"من عادى لي وليا فقد آذنته بالحرب"
عن أبي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه قال: قال رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : ((إنَّ الله تَعالَى قَال : مَنْ عَادَى لي وَلِيّاً فَقَدْ آذَنْتُهُ بِالْحَرْبِ، وَمَا تَقَرَّبَ إلَيَّ عَبْدِي بِشَيْءٍ أَحَبَّ إلَيَّ مِمَّا افْتَرَضْتُهُ عَلَيْهِ، وَلا يَزَالُ عَبْدِي يَتَقَرَّبُ إلَيَّ بِالنَّوَافِلٍ حَتَّى أُحِبَّهُ، فإذَا أَحْبَبْتُهُ كُنْتُ سَمْعَهُ الَّذِي يَسْمَعُ بهِ، وَبَصَرَهُ الَّذِي يُبْصِرُ بهِ، وَيَدَهُ الّتي يَبْطِشُ بهَا، وَرِجْلَهُ الّتي يَمْشي بِهَا، وَلَئِنْ سَأَلِني لأعْطِيَنَّهُ، ولَئِن اسْتَعَاذَنِي لأُعِيذَنَّهُ ))
رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ
HADITHI YA 38 ANAYEONYESHA UADUI KWA RAFIKI YANGU MTIIFU NINATANGAZA VITA DHIDI YAKE
Kutoka kwa Abu Hurayra رضي الله عنه ambaye amesema kuwa Mtume صلى الله عليه وسلم kasema: Allaah سبحانه وتعالى kasema: Anayeonyesha uadui kwa Walii Wangu (rafiki wa karibu, yaani mja mtiifu aliye karibu naye) , nitatangaza vita dhidi yake. Mja Wangu hanikaribii na kitu chochote ninachokipenda zaidi kama zile amali nilizomuwajibisha, na mja Wangu anazidi kukaribia Kwangu kwa amali njema zisizokuwa wajibu ili nimpende. Ninapompenda, Ninakuwa masikio yake anayosikilizia (yaani Allah atamjaalia asikie mazuri kama Qur’an, Dhikr, Mawaidha n.k. Na sio Muziki, Masengenyo, na Machafu mengine), macho yake anayoonea (yaani Allah atamfanya macho yake yawe yanatazama yale ya kheri), mikono yake ambayo anakamatia (Allah atafanya mikono yake ikamate vile vya halali na kufanya yale yanayomridhisha Allah), miguu yake anayoendea (na Allah ataifanya miguu yake isitembee kuyaendea ila yale mema, ya kheri na Atakayoridhika nayo Yeye Allah). Anaponiomba (kitu) bila shaka Ninampa, na anaponiomba ulinzi bila shaka Nitamlinda.
Imesimuliwa na Al-Bukhari
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Al-Arba-uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 5: kujiepusha na uzushi katika dini
Hadithi hii inakataza kuzusha mambo ambayo hayapo katika dini
Soma Zaidi...Maswali juu ya Sunnah na hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Dua za wakati wa shida na taabu
Hizi ni Dua ambazo unatakiwa uziombe wakati wa shida na taabu
Soma Zaidi...Ni siku zipo huitwa Aiyami tashriq?
Aiyami ni wingi wa neno yaumi kwa maana siku. Kwenye uislamu Kuna masimu matukufu kama vile masimu ya tashriq. Je ni yapi hayo? Endelea na makala hii.
Soma Zaidi...Mambo yaliyo sunnah siku za Idi ('iyd) siku ya sikukuu
Makala hii inaelezea mambo mbalimbali yaliyothibiti katika Sunnah kuhusu namna ya kuadhimisha siku ya ‘Iyd kwa mujibu wa mafundisho ya Kiislamu. Miongoni mwa mambo hayo ni kuvaa mavazi mazuri, kula kabla ya Swalaah ya ‘Iydul-Fitwr, kuleta Takbira, kuswali kwenye Muswallaa, pamoja na adabu nyingine zinazopaswa kufuatwa na Waislamu katika siku ya Sikukuu.
Soma Zaidi...