picha

Figo ni nini, ni yapi maradhi yake na nitajiepusha vipi na maradhi ya figo

Makala hii itakwenda kukueleza ni nini hasa hizi figo, na ni yapi maradhi yake na ni kwa namna ggani utaweza kujilinda na maradhi ya figo.

Figo ni nini, ni yapi maradhi yake na nitajiepusha vipi na maradhi ya figo

IJUWE FIGO NA MARADHI YAKE NA NAMNA YA KUJIKINGA NA MARADHI YA FIGO:

Figo ni katika viungo muhimu sana katika mwili wa mwanadamu. Ijapokuwa kila kiungo ni muhimu kwenye mwili wa binadamu, lakini katika mfumo wa kutoa mkojo na kuchuja damu figo ni muhimu zaidi. maradhi ya figo yamekuwa yakiongezeka kuliko ilivyokuwa hapo zmani, ijapokuwa kasi yake sio sawa na maradhi mengine. Makala hii itakwenda kukueleza ni nini hasa hizi figo, na ni yapi maradhi yake na ni kwa namna ggani utaweza kujilinda na maradhi ya figo.


Kila mtu ana figo mbili kwenye mwili wake, ukubwa wa figo unakadiriwa kufukia ukubwa wa ngumi yako. Katika mwili wako figo hupatikana karibia na katikati ya mgongo chini kidogo ya mbavu. Ndani ya kila figo kuna mamilioni ya vichujio vya kuchuja damu vinavyojulikana kama nephron. Kazi yake kubwa ni kuchuja damu, kuondoa uchafu kwenye damu na kuondoa maji ya ziada kwenye damu na kupata mkojo ambao ni mchanganyiko wa majina na uchafu uliotoka kwenye damu. Baadaye maji haya ya mchanganyko yanakwenda kwenye kibofu na kuhifadhiwa kama mkojo.



Kati ya maradhi mengi ya figo huanza kuathiri hizi nephone. Na endapo hizi nephrone zikiharibiwa zinapelekea figo kuathirika na kushindwa kufanya kazi vyema na kushindwa kuondoa uchau kwenye damu. Katika sababu za tatizo hili la kuathirika kwa nephone inaweza kuwa matatizo ya kurithi, majeraha, ama matumizi ya madawa ambayo athari yake yanaweza kuathiri figo.



Unaweza kuwa hatarini sana kama una maradhi ya kisukari, ama kama una shinikizo kubwa la damu ama una ukaribu wa kifamilia na watu ambao wana tatizo hili. Maradhi hatari ya figo ni yale ambayo huathiri nephone kipolepole na huwenda hii kuchukuwa miaka kadhaa hadi kuja kuumwa. Matatizo mengine yanayoweza kuathiri figo ni kama saratani ya figo na vijiwe vya kwenye figo.



Katika njia za kulinda figo yako dhidi ya maradhi ni pamoja na kunywa maji mengi angalau glasi 8 kwa siku. Fanya mazoezi na punguza kula vyakula vyenye chumvi sana. Nenda chooni kila unapohisi kukojoa wacha kubana mkojo kwa muda mrefu. Hizi ni baadhi tu ya njia ambazo zitakusaidia kulinda figo zako dhini ya maradhi.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1712

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Sababu za homa kwa watoto wachanga

Muhtasari (Executive Summary) ​Homa kwa mtoto mchanga si ugonjwa wenyewe, bali ni ishara kwamba mfumo wa kinga ya mwili unapambana na kitu kigeni. Ingawa homa inaweza kuwatia hofu wazazi wengi, mara nyingi husababishwa na maambukizi ya virusi, bakteria, mabadiliko ya mwili kama kuota meno, au matokeo ya kawaida ya chanjo. Makala haya yanachambua sababu hizi kwa kina na kutoa mwongozo wa lini unapaswa kukimbilia hospitali haraka.

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI kwa Mtu Aliyeambukizwa Karibuni

Makala hii inaelezea hatua ya awali ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU), inayojulikana kama hatua ya maambukizi makali (acute HIV infection). Inafafanua dalili za kawaida zinazoweza kujitokeza wiki chache baada ya mtu kupata maambukizi, umuhimu wa kupima mapema, na kuondoa dhana potofu kuhusu dalili hizi.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kupooza (Stroke): Dalili za mwanzo na kinga.

​Ugonjwa wa kupooza, unaojulikana kitabibu kama stroke au cerebrovascular accident (CVA), ni dharura kubwa ya kitabibu inayotokea wakati mtiririko wa damu kwenye sehemu ya ubongo unapoingiliwa au kukatika. Kila sekunde ni muhimu katika kuokoa tishu za ubongo na kupunguza ulemavu wa kudumu. Makala haya yanafafanua dalili za mwanzo, sababu za hatari, na mikakati madhubuti ya kuzuia ugonjwa huu kwa maisha yenye afya bora

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi ya sikio kwa watu wazima

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi ya sikio mara nyingi ni maambukizi ya bakteria au virusi ambayo huathiri sikio la kati, nafasi iliyojaa hewa nyuma ya ngoma ya sikio ambayo ina mifupa midogo ya sikio inayotetemeka. Maambukizi ya si

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa ngozi wa Scabies (Kupele): Tiba yake na usafi.

Kupele (Scabies) ni ugonjwa wa ngozi unaowasha sana unaosababishwa na wadudu wadogo sana wanaoitwa Sarcoptes scabiei. Wadudu hawa huchimba mahandaki chini ya ngozi ili kutaga mayai, jambo linalosababisha mwasho mkali ambao huwa mbaya zaidi nyakati za usiku. Scabies huambukiza kwa urahisi sana kupitia mguso wa ngozi na ngozi au kushirikiana nguo na matandiko. Makala haya yanakupa mwongozo wa tiba sahihi na jinsi ya kudumisha usafi ili kutokomeza ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI

KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI Fanya miadi na daktari wako wa kawaida ikiwa una ishara au dalili zinazokupa wasiwasi.

Soma Zaidi...