Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa
1. Maumivu makali wakati wa kujamiiana.
Kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo bakteria tayari wameshambulia sehemu mbalimbali kwenye kibofu Cha mkojo na sehemu zinazozunguka kama vile via vya uzazi kwa hiyo wakati wa kujamiiana mtu anapata maumivu hali hii uwatokea hasa watu wale ambao maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo yanapokuwa yamesambaa sana na yamekaa mda mrefu.kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa tunaangalia afya zetu mara kwa mara Ili kuepusha matatizo makubwa yanayoweza kujitokeza.
2.Mtu mwenye uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo anasikia maumivu wakati wa kukojoa.
Hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria ambao uingia kwenye kibofu Cha mkojo na kusababisha maambukizi na pengine kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe na uharibifu wowote ambao umeshafanyika kwenye kibofu Cha mkojo kwa hiyo wakati wa kukojoa mkojo ugusa sehemu ya majeraha na kusababisha maumivu wakati wa kukojoa kwa hiyo basi baada ya kujua hayo yote tunapaswa kutumia madawa ambayo yanatibu ugonjwa huu kwa sababu yapo na wengi wamepona na tusiyameze bila ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya.
3. Kuwepo kwa damu kwenye mkojo.
Hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na Maambukizi hayo yamekuwa makubwa zaidi na kusababisha kuvuja damu kwenye sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo ndio maana mkojo utoka n damu au uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo inakuwa unavuja damu ndo maana mkojo utoka pamoja na damu, hali hii sio nzuri inaweza kuleta madhara makubwa zaidi kwa hiyo mgonjwa anapaswa kuwaona wataalamu wa afya kwa msaada zaidi kwa sababu magonjwa haya yanatibika na dawa zipo hospitalini.
4. Maumivu makali kwenye Tumbo la chini.
Kwa wakati mwingine Kunakuwepo na maumivu kwenye sehemu ya tumbo la chini , hali hii usababishwa na Maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo ambapo kibofu Cha mkojo kinakuwa kimeshambuliwa na bakteria ambapo maumivu huwa mengi kwenye tumbo la chini.
5. Mkojo kutoa harufu mbaya.
Watu wenye matatizo ya uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, mkojo wao utoa harufu mbaya hali hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo ambayo usababisha harufu ya mkojo kubadilika na kuwa mbaya kwa hiyo pengine mkojo unaweza kuwa na usaha ambao usababisha mkojo kutoa harufu mbaya. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi mgonjwa inabidi kwenda hospitalini kwa matibabu zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Nimonia ni Hali ya kuvimba pafu inayoathiri hasa vifuko vya hewa viitwavyo Alveoli, husababishwa na Maambukizi ya virusi
Soma Zaidi...Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Njia za kufanya Ili kupunguza maumivu ya tatizo la uti wa mgongo, ni njia unazopaswa kufanya pale unapokuwa na tatizo la uti wa Mgongo.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...Hepatitis C ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoshambulia ini na kusababisha kuvimba. Watu wengi walioambukizwa na virusi vya Hepatitis C (HCV) hawana dalili. Kwa kweli, watu wengi hawajui kuwa wana maambukizi ya Hepatitis C hadi uharibifu wa ini
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi,ni kutokana na kazi zao pamoja na mazingira yao kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata Ugonjwa wa ukimwi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kufanya usafi wa sikio, sikio ni mojawapo ya ogani ambayo usaidia kusikia,kwa hiyo sikio linapaswa kusafishwa kwa uangalifu kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...