Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa
1. Maumivu makali wakati wa kujamiiana.
Kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo bakteria tayari wameshambulia sehemu mbalimbali kwenye kibofu Cha mkojo na sehemu zinazozunguka kama vile via vya uzazi kwa hiyo wakati wa kujamiiana mtu anapata maumivu hali hii uwatokea hasa watu wale ambao maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo yanapokuwa yamesambaa sana na yamekaa mda mrefu.kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa tunaangalia afya zetu mara kwa mara Ili kuepusha matatizo makubwa yanayoweza kujitokeza.
2.Mtu mwenye uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo anasikia maumivu wakati wa kukojoa.
Hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria ambao uingia kwenye kibofu Cha mkojo na kusababisha maambukizi na pengine kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe na uharibifu wowote ambao umeshafanyika kwenye kibofu Cha mkojo kwa hiyo wakati wa kukojoa mkojo ugusa sehemu ya majeraha na kusababisha maumivu wakati wa kukojoa kwa hiyo basi baada ya kujua hayo yote tunapaswa kutumia madawa ambayo yanatibu ugonjwa huu kwa sababu yapo na wengi wamepona na tusiyameze bila ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya.
3. Kuwepo kwa damu kwenye mkojo.
Hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na Maambukizi hayo yamekuwa makubwa zaidi na kusababisha kuvuja damu kwenye sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo ndio maana mkojo utoka n damu au uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo inakuwa unavuja damu ndo maana mkojo utoka pamoja na damu, hali hii sio nzuri inaweza kuleta madhara makubwa zaidi kwa hiyo mgonjwa anapaswa kuwaona wataalamu wa afya kwa msaada zaidi kwa sababu magonjwa haya yanatibika na dawa zipo hospitalini.
4. Maumivu makali kwenye Tumbo la chini.
Kwa wakati mwingine Kunakuwepo na maumivu kwenye sehemu ya tumbo la chini , hali hii usababishwa na Maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo ambapo kibofu Cha mkojo kinakuwa kimeshambuliwa na bakteria ambapo maumivu huwa mengi kwenye tumbo la chini.
5. Mkojo kutoa harufu mbaya.
Watu wenye matatizo ya uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, mkojo wao utoa harufu mbaya hali hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo ambayo usababisha harufu ya mkojo kubadilika na kuwa mbaya kwa hiyo pengine mkojo unaweza kuwa na usaha ambao usababisha mkojo kutoa harufu mbaya. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi mgonjwa inabidi kwenda hospitalini kwa matibabu zaidi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Ugonjwa wa kuharibika kwa mwili ni aina ya ugonjwa sugu wa Akili ambao huwezi kuacha kufikiria kuhusu kasoro katika mwonekano wako au ya kuwaziwa. Lakini kwako, mwonekano wako unaonekana kuwa wa aibu sana hivi kwamba hutaki kuonekana na mtu yeyote
Soma Zaidi...Kuharisha ni Hali ya kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisicho na damu
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na maumivuvya tumbo chini ya kitovu upande wa kushito. Post hii itakuletea sababu za maukivubhayo na nini ufanye.
Soma Zaidi...Swali hili limeulizwa na mdau mmoja. Kuwa endapo mtu atafanya ngono zembe na akapata virusi je ataweza kuambukiza.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na mambo hatari yanayosababisha ugonjwa wa moyo.
Soma Zaidi...Kutokwa na mate mengi mdomoni si ugojwa ni hali inayoweza kutokea kwa mtu yeyote. Mara nyingi hali hii haihitaji matibabu wa dawa, na huondoka yenyewe. Lakini hutokea baadhi ya nyakati ikawa mate yanatoka zaidi mdomoni. Je na wewe ni miongoni mwao? Makala
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,
Soma Zaidi...Makala hii itazungumzia dalili za Malaria, athari za kuchelewa kutibu malaria, na matibabu ya malaria
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.
Soma Zaidi...