picha

Dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo

Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa

1. Maumivu makali wakati wa kujamiiana.

Kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo bakteria tayari wameshambulia sehemu mbalimbali kwenye kibofu Cha  mkojo na sehemu zinazozunguka kama vile via vya uzazi kwa hiyo wakati wa kujamiiana  mtu anapata maumivu hali hii uwatokea hasa watu wale ambao maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo yanapokuwa yamesambaa sana na yamekaa mda mrefu.kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa tunaangalia afya zetu mara kwa mara Ili kuepusha matatizo makubwa yanayoweza kujitokeza.

 

 

2.Mtu mwenye uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo anasikia maumivu wakati wa kukojoa.

Hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria ambao uingia kwenye kibofu Cha mkojo na kusababisha maambukizi na pengine kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe na uharibifu wowote ambao umeshafanyika kwenye kibofu Cha mkojo kwa hiyo wakati wa kukojoa mkojo ugusa sehemu ya majeraha na kusababisha maumivu wakati wa kukojoa kwa hiyo basi baada ya kujua hayo yote tunapaswa kutumia madawa ambayo yanatibu ugonjwa huu kwa sababu yapo na wengi wamepona na tusiyameze bila ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya.

 

3. Kuwepo kwa damu kwenye mkojo.

Hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na Maambukizi hayo yamekuwa makubwa zaidi na kusababisha kuvuja damu kwenye sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo ndio maana mkojo utoka n damu au uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo inakuwa unavuja damu ndo maana  mkojo utoka pamoja na damu, hali hii sio nzuri inaweza kuleta madhara makubwa zaidi kwa hiyo mgonjwa anapaswa kuwaona wataalamu wa afya kwa msaada zaidi kwa sababu magonjwa haya yanatibika na dawa zipo hospitalini.

 

4. Maumivu makali kwenye Tumbo la chini.

Kwa wakati mwingine Kunakuwepo na maumivu kwenye sehemu ya tumbo la chini , hali hii usababishwa na Maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo ambapo kibofu Cha mkojo kinakuwa kimeshambuliwa na bakteria ambapo maumivu huwa mengi kwenye tumbo la chini.

 

5. Mkojo kutoa harufu mbaya.

Watu wenye matatizo ya uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, mkojo wao utoa harufu mbaya hali hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo ambayo usababisha harufu ya mkojo kubadilika na kuwa mbaya kwa hiyo pengine mkojo unaweza kuwa na usaha ambao usababisha  mkojo kutoa harufu mbaya. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi mgonjwa inabidi kwenda hospitalini kwa matibabu zaidi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3306

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 ai web app     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Vidonda vya tumbo husababishwa na nini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu visababishi vya vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Dalili za Ukimwi

Makala hii itaeleza dalili za ukimwi, dalili za VVU, magonjwa nyemelezi na matumizi ya ARV

Soma Zaidi...
Dalili za maumivu ya uti wa Mgongo

Posti hii inahusu zaidi dalili za uti wa mgongo ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uti wa Mgongo.

Soma Zaidi...
Sababu za miguu kufa ganzi.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.

Soma Zaidi...
Dalili za gonorrhea - gonoria

Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume

Soma Zaidi...
Dalilili na sababu za magonjwa ya zinaa

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalilili,SABABU,mambo ya hatari katika Magonjwa ya zinaa (STDs), au magonjwa ya zinaa (STIs), kwa ujumla hupatikana kwa kujamiiana. Vimelea vinavyosababisha magonjwa ya zinaa vinaweza kupita kutoka kwa mtu hadi kwa mtu

Soma Zaidi...