Haki ya kumiliki mali katika uislamu

Haki ya kumiliki mali katika uislamu

Haki ya kumiliki mali



Kumiliki mali ni suala la kimaumbile na limeshikamana na silka ya kujihami (self presevation).Katika historia ya binaadamu suala la kumiliki mali limekuwa likiandamana na itikadi au falsafa inayotawala mahali.


Kwa mfano katika baadhi ya jamii za kitwaghuti umilikaji wa mali uko chini ya familia au huwa chini ya “watu wote” (mali ya umma) au huwa chini ya mtu au watu binafsi. Katika Uislamu kila kitu kipo chini ya miliki ya Mwenyezi Mungu:


“Sema Ee Mola uliyemiliki Ufalme wote! Humpa ufalme umtakaye na humuondolea ufalme umtakaye na humtukuza umtakaye na humdhalilisha umtakaye, kheri imo mikononi mwako. Bila shaka wewe ni Mwenye Uwezo juu ya kila kitu ”. (3:26).



Hivyo ni dhahiri kuwa Mwenyezi Mungu ndiye mmilikaji wa hakika wa vitu vyote. Binaadamu anamiliki mali kwa dhamana tu siyo kwa hakika na kwa sababu hiyo ataulizwa jinsi alivyotumia. Katika Qur-an Allah (s.w) ameruhusu watu binafsi au kwa vikundi kumiliki mali pale aliposema:


“Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe kwa ajili ya hizo (sadaka zao) na kuwataja kwa vizuri (mbele yangu) na uwaom bee dua. Hakika kuwaombea kwako kutawapa utulivu (watengenekewe); na Mwenyezi Mungu ndiye asikiaye na ajuaye.” (9:103)


Hivyo Uislamu unakubali na kuheshimu haki ya mtu au watu binafsi kumiliki mali.



Mipaka ya Umilikaji mali
(i)Mali hiyo iwe imechumwa kwa njia ya halali. Uislamu unaitambua haki ya kumiliki mali na haki ya kuilinda mali hiyo, lakini mali yenyewe iwe ya halali.



(ii)Mtu anaweza kuiuza au kuitumia mali yake apendavyo maadamu ana akili timamu. Iwapo hana akili timamu, itabidi apatikane mdhamini wa kuingalia mali hiyo kwa niaba na manufaa yake na manufaa ya jamii.



(iii)Maadamu mtu anayo mali basi anao pia wajibu wa kutekeleza majukumu yanayohusiana na mali aliyo nayo.



(iv)Uislamu unakataza ubakhili na israfu (ubadhirifu) katika matumizi. Mwenyezi Mungu anasema:


Wala usifanye mkono wako (kama) uliofungwa shingoni mwako, wala usikunjue ovyo ovyo, utakuwa ni mwenye kulaumiwa na kufilisika. (17:29).


Enyi wanaadamu! Chukueni mapambo yenu wakati wa kila sala; na kuleni (vizuri) na kunyw eni (vizuri). Lakini msipite kiasi tu. Hakika Yeye hawapendi wapitao kiasi. (7:3 1).


Ubadhilifu ni kufanya mojawapo ya mambo matatu
Kwanza,
kununua kitu usichokihitaji. Au kununua kitu unachokihitaji lakini kwa kiasi kingi kuliko unavyoweza kutumia. Kwa mfano kutengeneza chapati tano ilihali uwezo wako ni wa kula chapati mbili tu, halafu zile tatu ukazitupa jalalani.


Pili ni ubadhilifu kununua kitu chochote kile cha haramu, hata ikiwa kwa thamani ndogo namna gani. Kwa mfano hata kama masanduku laki moja ya bia yanauzwa kwa shilingi hamsini ukiitoa shilingi hamsini hiyo kununua pombe hiyo unaandikiwa madhambi ya ubadhilifu.


Tatu kutoa sadaka kwa ajili ya kujionesha kwa watu, badala ya kuandikiwa thawabu unaandikiwa madhambi ya israfu.



(v) Uislamu unakataza rasilimali zilizo katika jamii kuachwa bila kutumiwa Mtume (s.a.w) amesema mtu akiendeleza ardhi ana haki ya kuimiliki. Lakini akiiwacha kwa miaka mitatu bila kuitumia mtu mwingine ana haki ya kuiendeleza na kuimiliki.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 905

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Zoezi la 6 kusimamisha swala

Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
Njia za kudhibiti riba

Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana.

Soma Zaidi...
Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada

Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudi kumfanya Mtume (s.

Soma Zaidi...
Hawa ndio wanaoruhusiwa kurithi

Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu.

Soma Zaidi...
Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi

Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.

Soma Zaidi...
Fiqh.

Kipengele hichi tutajifunza chimbuko la fiqh na maana ya figh.

Soma Zaidi...