haki na wajibu kwa wakubwa

haki na wajibu kwa wakubwa

Wajibu wa Wakubwa kwa wadogo na wa Wadogo kwa Wakubwa



Katika utamaduni wa Kiislamu wakubwa kwa umri au kwa Maarifa au kwa mamlaka ya (uongozi), wanawajibika kuwahurumia, kuwapenda, kuwaongoza, kuwaelekeza, kuwashauri na kuwaasa wadogo zao kiumri au kimaarifa au mamlaka. Wakubwa wanawajibika kuwamrisha wadogo zao kufanya mema na wanawajibika kukataza maovu wenyewe wakiwa ni viigizo nyema. Kwa kutumia uzoefu wao wanawajibika kuwaelekeza na kuwaongoza katika njia iliyonyooka, wale walio chini yao kiumri na kimamlaka.
Kwa upande mwingine, wadogo kiumri au kimamlaka wanawajibika kuwatii na kuwaheshimu wale walio juu yao kama tunavyoamrishwa:


"Enyi mlioamini! Mtiini Mwenyezi Mungu na mtiini Mtume na wenye mamlaka juu yenu, walio miongoni mwenu.Na kama mkikhitilafiana juu ya jambo lolote basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamwamini Mwenyezi na siku ya Mwisho. Hiyo ndiyo kheri nayo ma matokeo bora kabisa." (4:59).
Kutokana na aya hii tunawajibika kuwatii wakubwa zetu na wale wenye mamlaka juu yetu, baada ya kumtii Allah (s.w) na Mtume (s.a.w).


Lakini hatuwajibiki kuwatii wakubwa zetu na wenye mamlaka juu yetu kinyume na kumtii Allah (s.w) na Mtume (s.a.w).. Wale wenye mamlaka juu yetu wakituamrisha kumuasi Allah (s.w) na Mtume wake (s.a.w), tuwakatalie kwa heshima huku tukiwarejesha kwa mafundisho ya Qur-an na sunnah kuwa: "Hapana utii kwa kiumbe katika kumuasi Muumba."



Msisitizo wa kuwatii na kuwaheshimu wakubwa zetu kiumri na kimamlaka pia tunaupata katika Hadith zifuatazo:
Ibn Abbas (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Si katika sisi (si muumini) yule asiyewahurumia wadogo zetu na kuwaheshimu wakubwa zetu wala haamrishi mema na kukataza mabaya ". (Tirmidh)



Anas (r.a) anaeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Kama kijana atamuheshimu mtu mzima kutokana na umri wake, naye Allah atajaalia mtu atakayemheshimu katika uzee wake." (Tirmidh)



Pamoja na msisitizo wa kuwaheshimu wakubwa zetu, hatunabudi kuzingatia mipaka ya Uislamu katika kufanya hivyo. Wakati mwingine kuwaheshimu na kuwatii wakubwa kupita kiasi, hutupelekea kwenye shirk. Kwa kuchelea hili, Mtume (s.a.w) aliwakataza Waislamu kumsifu kupita kiasi kama wakristo walivyofanya kwa mwana wa Maryamu (Issa (a.s) na kumfanya mwana wa Mungu. Hivyo Mtume (s.a.w) ametuelekeza tumsifu kwa kumwita "Mja na Mtume wa Allah".



Pia kwa kuchelea shirk, Mtume (s.a.w) aliwakataza Waislamu wasimsimamie wakati akiingia kwenye mkutano au akipita njiani kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:
Anas (r.a) ameeleza: "Hapana mtu tuliyempenda kuliko Mtume wa Allah.Hatukuwa tunamsimamia kwa sababu alikuwa hapendi kusimamiwa." (Tirmidh)
Muawiyah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yeyote yule anayependa watu wamuheshimu kwa kumsimamia, atarajie kuwa mkazi wa motoni." (Tirmidh, Abu Daud)



Tunajifunza kutokana na Hadithi hizi kuwa "heshima" isipelekee kuwafanya wengine kuwa wanyonge na dhalili na wengine kuwa watukufu na bora. Tunapo heshimu au kuheshimiwa, hatunabudi kuiweka mbele yetu aya ifuatayo:


Enyi watu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamume (mmoja; Adamu) na (yule yule) mwanamke (mmoja; Hawa). Na tumekufanyeni matafa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu basi siyo mkejeliane).Hakika ahishimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye habari (za mambo yote). (49:13)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1534

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Swala ya tarawehe jinsi ya kuiswali

Post hii itakwenda kukufundisha kuhusi swala ya tarawehe, faida zake na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga

Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga.

Soma Zaidi...
Je ni nani mwenye haki ya kutaliki

Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya zakat na sadaqat

Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Madhara ya riba kwenye jamii

Haya ni madhara ya riba katika jamii. Ni kwa namna gani jamii inadhurika kutokana na riba?

Soma Zaidi...
Utaratibu wa kuzuru makaburi na dua zinazosomwa wakati wa kuzuru kaburi

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika katika kuzuru kaburi la muislamu.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu

Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala.

Soma Zaidi...
maana ya uchumi kiislamu

Maana ya UchumiMfumo wa maisha wa Kiislamu humuelekeza binaadamu kujenga na kudumisha uhusiano wake na Al-lah (s.

Soma Zaidi...