Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya
Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.
Mirathi katika jamii za kijahili
Katika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w), watoto wadogo ambao hawajafikia baleghe, walemavu na wazee ambao hawakuwa na uwezo wa kupigana vita katika kuihami heshima ya familia na kabila kwa ujumla, hawakupata chochote katika mirathi. Aghalabu katika jamii zote za kijahili mwanamke akiwa binti au mke, au mama au katika uhusiano wowote ule kwa marehemu, hakuwa na haki yoyote ile katika urithi.
Badala yake wanawake wenyewe walifanywa mali ya kurithiwa kwa nguvu na ndugu wa marehemu au mtoto mkubwa wa kiume wa marehemu ambaye hakuzaliwa na huyo mama anayerithiwa. Waliwarithi kama wake au vinginevyo waliwaoza kwa wanaume wengine kwa nguvu kinyume cha ridhaa ya wajane hao. Kwa namna hii wanawake walirithiwa kama sehemu ya mali ya marehemu na waliuzwa na kununuliwa kama bidhaa. Uislamu umepiga marufuku tabia hii katika aya ifuautayo:
Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazuie (kuolewa na wanaume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhi ya vile mliiyowapa(Hapana ruhusa haya) isipokuwa wawe wamefanya uovu ulio wazi nakaeni nao kwawema " (4:19).
Wala msiwaoe wake waliowaoa baba zenu, ispokuwa yale yaliyokwisha pita. Bila shakajambo hili ni uovu na chukizo na ni njia mbaya. (4:22).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango
Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.
Soma Zaidi...Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu
Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu.
Soma Zaidi...Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume.
Soma Zaidi...