Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani

3.

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani

3. JAMII ZA KIAFRIKA



Katika bara Ia Afrika pamoja na kuwa na jamii nyingi zenye mila na desturi zinazotofautiana hatupati hata jamii moja ya kitwaghuti iliyompa mwanamke sauti katika nyumba wala katika jamii. Matatizo au makosa yote yaliyofnayika nyumbani yalisukumizwa kwa mwanamke. Mwanamke alifanyishwa kazi na kubebeshwa mizigo kama punda. Mwanamke hakuwa na haki ya kumiliki mali aliyoichuma mwenyewe. Kutokana na mahari yaliyolipwa wakati wa kuolewa mwanamke alifanywa mali ya mumewe ambaye aliweza kumfanya lolote alitakalo kama anavyofanyiwa mtumwa.


Pia katika jamii nyingi za Kiafrika, situ kwamba mwanamke hakuwa na haki ya urithi bali yeye mwenyewe alirithiwa kwa nguvu na mmoja wa shemeji zake. Akili ya mwanamke katika jamii nyingi imelinganishwa na ile ya mtoto mdogo. Kwa sababu hii mwanamke hakutakiwa ushauri kwa jambo lolote lile katika familia. Mara nyingi ushauru wa mtoto wa kiume ulithaminiwa kuliko ule wa mama yake. Kwa ujumla katika jamii nyingi za Kiafrika mwanamke alidunishwa kwa kiasi kikubwa.


Pamoja na kazi kubwa ya uzazi na malezi ya watoto, mwanamke aliachiwa majukumu yote ya nyumbani na alikuwa mshiriki mkuu katika shughuli za uchumi ambapo mali aliyoichuma kwa jasho lake ilichukuliwa na mwanamume bila hata kushauriwa. Hivi ndivyo alivyo nyanyaswa na kudunishwa mwanamke katika jamii mbali mbali za ulimwengu katika nyakati mbali mbali za historia. Je hivi leo zimechukuliwa hatua gani ili kukomesha uonevu huu dhidi ya mwanamke?



Katika miaka hii pamekuwa na vuguvugu Ia kumkomboa mwanamke ili kumrudishia haki zake na hadhi yake iliyodhulumiwa na wanaume. Vyama vingi vya kisiasa vimelipa suala hili kipa umbele na vimeundwa vyama vya wanawake vya Kitaifa na Kimataifa vinavyojishughulisha tu na kumkomboa mwanamke. Je, vyama hivi vimeleta mafanikio yoyote?


Ukichunguza mbinu zinazotumiwa na vyama hivi katika ukombozi huu wa mwanamke, utakuta hazina tofauti kabisa na zile zilizotumiwa na Ulaya na Marekani katika kipindi cha mapinduzi ya viwanda za kumtaka mwanamke.



(a)Awe sawa na mwanamume kwa kila kitu bila ya kuzingatia tofauti za kimaumbile na nafasi ya mwanamke na mwanamume katika jamii.
(b)Ashiriki sawa na mwanamume katika uchumi na siasa na kumfanya ajitegemee kiuchumi.
(c)Awe huru kutoka nyumbani kwake na kuchanganyika na wanaume apendavyo.



Tuliona kuwa, matokeo ya kumtetea mwanamke kwa mtazamo huu haikuwa kumkomboa bali kumdhalilisha zaidi na kumvua haya na utu wake. Pia ukombozi wa mwanamke kwa mtazamo huu haukuleta nafuu yoyote katika jamii bali umezidi kuidumaza na kuigharimu kiasi kikubwa. Kampeni hii ya ukombozi wa mwanamke imechangia sana katika kuvunja maisha ya familia na kueneza magonjwa ya zinaa na kuongeza idadi ya wavuta bangi, wazururaji na majambazi kaitka jamii.



Ni nani hasa aliyemkombozi wa mwanamke? Bila shaka ni yule aliyemuumba na kumleta hapaduniani kama mwenza wa mwanamume. Hivyo haki na hadhi ya mwanamke itapatikana kwa kumuamini Allah (s.w) na kufuata muongozo wa maisha aliouweka katika kukiendea kila kipengele cha maisha ya binafsi, familia.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 445

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na vita vya uhudi

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Lut (a.s)

(i) Tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuondoa maovu katika jamii kwa mikono yetu na ikiwa hatuwezi tuyakemee kama alivyofanya Nabii Lut(a.

Soma Zaidi...
Yusufu Aokotwa na Kuuzwa nchini Misri

Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji.

Soma Zaidi...
Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.

Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.

Soma Zaidi...