Nabii Ibrahim(a.
Nabii Ibrahim(a.s), baada ya kupingwa mawe na kufukuzwa na baba yake mzazi, hakukata tamaa bali aliamua kuikabili jamii na kuifikishia ujumbe wa Uislamu kwa hekima kwa kutumia hoja madhubuti.
(Na kumbukeni) Ibrahimu alipomwambia baba yake Azara “Unawafanya masanamu kuwa waungu? Hakika ninakuona wewe na watu wako mumo katika upotofu (upotevu) ulio dhahiri.(6:74)
Na namna hivi tulimwonyesha Ibrahimu Ufalme wa mbingu na ardhi (kuwa ni wa Mwenyezi Mungu), na ili awe miongoni mwa wenye yakini.(6:75)
Na usiku ulipomwingilia (Ibrahimu na hali kakaa na makafiri) akaona nyota, alinena “(Nyota) hii ni Mola wangu.” Ilipotua (ikapotea), alisema (kuwaambia wale makafiri kama kwamba yu pamoja nao katika Ibada ile): “Sipendi waola wanaopotea (hawawepo ila wakati makhsusi tu).(6:76)
Na (usiku wa pili) alipouona mwezi unachomoza alisema: “Huu (mwezi) ndio Mola wangu.” Ulipotua alisema: “Asiponiongoza Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa watu wapotofu(Na Mola huyu hawezi kuniongoza kwani anakuwa hayupo wakati mwingine).” (6:77).
Na (siku ya tatu) alipoliona jua linachomoza alisema (kuwaambia): “Hili (jua) ndilo Mola wangu. Huyu Mola mkubwa kabisa.” Lilipotua alisema “Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha (na Mungu).(6:78)
(Mimi) nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Hali ya kuwa nimewacha dini za upotevu. Mimi (ni Mwislamu) si miongoni mwa washirikina.” (6:79)
Watu wa jamii yake walimshangaa kwa msimamo wake wa kumpwekesha Allah(s.w) na kujadiliana naye kama ifuatavyo:
Na watu wake wakajadiliana naye (kwa kumwambia Unaacha Ibada ya wazee! Utadhurika)! Akasema: “Je, Mnanihoji juu ya Mwenyezi Mungu, mnaowashirikisha naye. Isipokuwa Mola wangu akipenda jambo (kuwa, basi litakuwa). Mola wangu anakijua vyema kila kitu. Basi je, hamshiki mauidha (6:80)
“Na nitawaogopaje hao mnaowashirikisha, hali nyinyi hamwogopi kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kile ambacho
hakukiteremshia dalili kwenu (yoyote ya kuonyesha kuwa ni mungu)? Basi kundi gani katika mawili haya (langu au lenu) linastahiki zaidi kupata amani? Kama nyinyi mnajua jambo (lijibuni hili).(6:81)
“(Hapana shaka kuwa) wale walioamini na hawakuchanganya imani yao na ushirikina kuwa hao ndio watakaopata amani, nao ndio walioongoka.(6:82)
Na hizi ndizo (baadhi ya) hoja zetu tulizompa Ibrahimu juu ya watu wake. Tunamyanyua katika vyeo yule tumtakaye (kwa kuwa anakwenda mwendo tunaoutaka). Hakika Mola wako ndiye Mwenye hikima (na) ndiye ajuaye. (6:83)
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 938
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya
👉2 Simulizi za Hadithi Audio
👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉4 Kitau cha Fiqh
👉5 kitabu cha Simulizi
👉6 Madrasa kiganjani
Mafunzo ya sura zilizochaguliwa
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)
Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a. Soma Zaidi...
NAMNA MTUME(S.A.W) ALIVYOSIMAMISHA DOLA YA KIISLAMU MADINAH
Safari ya Mtume(s. Soma Zaidi...
Mbinu na njia walizotumia maadui wa uislamu dhidi ya waislamu na dola ya kiislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina
Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s. Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...
Khalifa na Utungaji Sheria, na utiifu juu ya sheria na usimamiaji wa haki
Soma Zaidi...
HISTORIA YA BI KHADIJA (HADIJA) MKE WA KWANZA WA MTUME MUHAMMAAD (S.A.W)
HISTORIA YA BI KHADIJABi Khadija jinalake halisi ni Khadija bint Khuwald bin Asab baba yake alikuwa ni mfanya biashara. Soma Zaidi...
MTUME(S.A.W) KULINGANIA UISLAMU MAKKA
Historia ya harakati za Mtume(s. Soma Zaidi...
Nasaba ya Mtume Muhammad S.A.W na familia yake.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 1 Soma Zaidi...
tarekh 02
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...