image

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani

3.

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani

3. JAMII ZA KIAFRIKA



Katika bara Ia Afrika pamoja na kuwa na jamii nyingi zenye mila na desturi zinazotofautiana hatupati hata jamii moja ya kitwaghuti iliyompa mwanamke sauti katika nyumba wala katika jamii. Matatizo au makosa yote yaliyofnayika nyumbani yalisukumizwa kwa mwanamke. Mwanamke alifanyishwa kazi na kubebeshwa mizigo kama punda. Mwanamke hakuwa na haki ya kumiliki mali aliyoichuma mwenyewe. Kutokana na mahari yaliyolipwa wakati wa kuolewa mwanamke alifanywa mali ya mumewe ambaye aliweza kumfanya lolote alitakalo kama anavyofanyiwa mtumwa.


Pia katika jamii nyingi za Kiafrika, situ kwamba mwanamke hakuwa na haki ya urithi bali yeye mwenyewe alirithiwa kwa nguvu na mmoja wa shemeji zake. Akili ya mwanamke katika jamii nyingi imelinganishwa na ile ya mtoto mdogo. Kwa sababu hii mwanamke hakutakiwa ushauri kwa jambo lolote lile katika familia. Mara nyingi ushauru wa mtoto wa kiume ulithaminiwa kuliko ule wa mama yake. Kwa ujumla katika jamii nyingi za Kiafrika mwanamke alidunishwa kwa kiasi kikubwa.


Pamoja na kazi kubwa ya uzazi na malezi ya watoto, mwanamke aliachiwa majukumu yote ya nyumbani na alikuwa mshiriki mkuu katika shughuli za uchumi ambapo mali aliyoichuma kwa jasho lake ilichukuliwa na mwanamume bila hata kushauriwa. Hivi ndivyo alivyo nyanyaswa na kudunishwa mwanamke katika jamii mbali mbali za ulimwengu katika nyakati mbali mbali za historia. Je hivi leo zimechukuliwa hatua gani ili kukomesha uonevu huu dhidi ya mwanamke?



Katika miaka hii pamekuwa na vuguvugu Ia kumkomboa mwanamke ili kumrudishia haki zake na hadhi yake iliyodhulumiwa na wanaume. Vyama vingi vya kisiasa vimelipa suala hili kipa umbele na vimeundwa vyama vya wanawake vya Kitaifa na Kimataifa vinavyojishughulisha tu na kumkomboa mwanamke. Je, vyama hivi vimeleta mafanikio yoyote?


Ukichunguza mbinu zinazotumiwa na vyama hivi katika ukombozi huu wa mwanamke, utakuta hazina tofauti kabisa na zile zilizotumiwa na Ulaya na Marekani katika kipindi cha mapinduzi ya viwanda za kumtaka mwanamke.



(a)Awe sawa na mwanamume kwa kila kitu bila ya kuzingatia tofauti za kimaumbile na nafasi ya mwanamke na mwanamume katika jamii.
(b)Ashiriki sawa na mwanamume katika uchumi na siasa na kumfanya ajitegemee kiuchumi.
(c)Awe huru kutoka nyumbani kwake na kuchanganyika na wanaume apendavyo.



Tuliona kuwa, matokeo ya kumtetea mwanamke kwa mtazamo huu haikuwa kumkomboa bali kumdhalilisha zaidi na kumvua haya na utu wake. Pia ukombozi wa mwanamke kwa mtazamo huu haukuleta nafuu yoyote katika jamii bali umezidi kuidumaza na kuigharimu kiasi kikubwa. Kampeni hii ya ukombozi wa mwanamke imechangia sana katika kuvunja maisha ya familia na kueneza magonjwa ya zinaa na kuongeza idadi ya wavuta bangi, wazururaji na majambazi kaitka jamii.



Ni nani hasa aliyemkombozi wa mwanamke? Bila shaka ni yule aliyemuumba na kumleta hapaduniani kama mwenza wa mwanamume. Hivyo haki na hadhi ya mwanamke itapatikana kwa kumuamini Allah (s.w) na kufuata muongozo wa maisha aliouweka katika kukiendea kila kipengele cha maisha ya binafsi, familia.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 216


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Nasaba ya mtume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Uchaguzi wa Abubakari kuwa Khalifa wa kwanza baada ya kufariki Mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)
Tukirejea Qurโ€™an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...

Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii
Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s. Soma Zaidi...

Muhutasari wa sifa za wanafiki
Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)
Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA WATU WEMA WALIOTAJWA KWENYE QURAN
Soma Zaidi...

NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE
Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a. Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

Khalifa na Uendeshaji wa Dola kwa ujumla, kulinda wasio waislamu na haki zao na mali zao.
Soma Zaidi...

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa
Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AANALELEWA NA BABU YAKE MZEE ABDUL-ALMUTALIB AKIWA NA UMRI WA MIAKA SITA (6)
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee โ€˜Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...