Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani

3.

Download Post hii hapa

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani

3. JAMII ZA KIAFRIKA



Katika bara Ia Afrika pamoja na kuwa na jamii nyingi zenye mila na desturi zinazotofautiana hatupati hata jamii moja ya kitwaghuti iliyompa mwanamke sauti katika nyumba wala katika jamii. Matatizo au makosa yote yaliyofnayika nyumbani yalisukumizwa kwa mwanamke. Mwanamke alifanyishwa kazi na kubebeshwa mizigo kama punda. Mwanamke hakuwa na haki ya kumiliki mali aliyoichuma mwenyewe. Kutokana na mahari yaliyolipwa wakati wa kuolewa mwanamke alifanywa mali ya mumewe ambaye aliweza kumfanya lolote alitakalo kama anavyofanyiwa mtumwa.


Pia katika jamii nyingi za Kiafrika, situ kwamba mwanamke hakuwa na haki ya urithi bali yeye mwenyewe alirithiwa kwa nguvu na mmoja wa shemeji zake. Akili ya mwanamke katika jamii nyingi imelinganishwa na ile ya mtoto mdogo. Kwa sababu hii mwanamke hakutakiwa ushauri kwa jambo lolote lile katika familia. Mara nyingi ushauru wa mtoto wa kiume ulithaminiwa kuliko ule wa mama yake. Kwa ujumla katika jamii nyingi za Kiafrika mwanamke alidunishwa kwa kiasi kikubwa.


Pamoja na kazi kubwa ya uzazi na malezi ya watoto, mwanamke aliachiwa majukumu yote ya nyumbani na alikuwa mshiriki mkuu katika shughuli za uchumi ambapo mali aliyoichuma kwa jasho lake ilichukuliwa na mwanamume bila hata kushauriwa. Hivi ndivyo alivyo nyanyaswa na kudunishwa mwanamke katika jamii mbali mbali za ulimwengu katika nyakati mbali mbali za historia. Je hivi leo zimechukuliwa hatua gani ili kukomesha uonevu huu dhidi ya mwanamke?



Katika miaka hii pamekuwa na vuguvugu Ia kumkomboa mwanamke ili kumrudishia haki zake na hadhi yake iliyodhulumiwa na wanaume. Vyama vingi vya kisiasa vimelipa suala hili kipa umbele na vimeundwa vyama vya wanawake vya Kitaifa na Kimataifa vinavyojishughulisha tu na kumkomboa mwanamke. Je, vyama hivi vimeleta mafanikio yoyote?


Ukichunguza mbinu zinazotumiwa na vyama hivi katika ukombozi huu wa mwanamke, utakuta hazina tofauti kabisa na zile zilizotumiwa na Ulaya na Marekani katika kipindi cha mapinduzi ya viwanda za kumtaka mwanamke.



(a)Awe sawa na mwanamume kwa kila kitu bila ya kuzingatia tofauti za kimaumbile na nafasi ya mwanamke na mwanamume katika jamii.
(b)Ashiriki sawa na mwanamume katika uchumi na siasa na kumfanya ajitegemee kiuchumi.
(c)Awe huru kutoka nyumbani kwake na kuchanganyika na wanaume apendavyo.



Tuliona kuwa, matokeo ya kumtetea mwanamke kwa mtazamo huu haikuwa kumkomboa bali kumdhalilisha zaidi na kumvua haya na utu wake. Pia ukombozi wa mwanamke kwa mtazamo huu haukuleta nafuu yoyote katika jamii bali umezidi kuidumaza na kuigharimu kiasi kikubwa. Kampeni hii ya ukombozi wa mwanamke imechangia sana katika kuvunja maisha ya familia na kueneza magonjwa ya zinaa na kuongeza idadi ya wavuta bangi, wazururaji na majambazi kaitka jamii.



Ni nani hasa aliyemkombozi wa mwanamke? Bila shaka ni yule aliyemuumba na kumleta hapaduniani kama mwenza wa mwanamume. Hivyo haki na hadhi ya mwanamke itapatikana kwa kumuamini Allah (s.w) na kufuata muongozo wa maisha aliouweka katika kukiendea kila kipengele cha maisha ya binafsi, familia.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 547

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Kuanzishwa kwa dola ya kiislamu madinah
Kuanzishwa kwa dola ya kiislamu madinah

Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...
 Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah
Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah

Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a.

Soma Zaidi...
tarekh
tarekh

MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU).

Soma Zaidi...
Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri
Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri

Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a.

Soma Zaidi...
Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.
Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba Γ°ΕΈβ€’β€Ή

Soma Zaidi...
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...