image

dalili za mimba baada ya tendo la ndoa na changa ndani ya wiki moja

Utajifunza dalili za mwanzoni za mimba changa kuanzia wiki moja baada ya tendo la ndoa

dalili za mimba baada ya tendo la ndoa na changa ndani ya wiki moja

DALILI ZA UJAUZITO BAADA YA TENDO LA NDOA

Je umeshawahi kujiuliza ni zipi zinaweza kuwa dalili za kwanza za ujauzito baada ya kushiriki tendo la ndoa? Hakika hili ni swali zuri na hapa niyakujuza majibu yake. Ukweli ni kuwa ni vigumu kuona dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa kama hutakuwa makini. Yes inawezekana kuzijuwa ila inahitaji uangalizi wa umakini kabisa. Mwanamke mmoja alishaniambia kuwa yeye ndani ya masaa matano baada ya kufanya tendo la ndoa anaweza kujuwa kama amebeba mimba ama laa. Nilipojaribu kumuuliza alikataa kabisa kunieleza.



Je naweza kuziona dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa?

Kabla ya kulijibu swahi hili inapasa kujuwa mabadiliko ya mwili wako kabla ya ujauzito ama kabla ya kushiriki tendo la ndoa. Kwanza zingatia mabo haya kabla ya kushiriki tendo la ndoa:-

  1. Jeoto la mwili wako. Hakikisha unatambuwa vyema kama mwili wako joto lake lipo kiasi gani. Na hakikisha unaweza kutofautisha kati ya joto la homa na joto la kawaida.
  2. Zingatia majimaji ya kwenye uke wako. Zingatia kama uke wako upo katika majimaji ama upo mkavu. Pia angalia rangi za mashavu ya uke.
  3. Zingatia tarehe zako. Kabla ya kushiriki tebdo la ndoa hakikisha tarehe zako unazifahamu vyema, pamoja na siku zako za hatari ni lini.


Je nitazijuaje sasa hizo dalili baada ya kuzingatia mambo hayo?

Kujuwa kama umebeba mimba ama laa inaweza kuchukuwa hata wiki moja kuona mabadiliko kwenye mwili wako, mabadiliko haya yataweza kukuambia kwamba huwenda umebebe mimba. Ila pia kuna baadhi ya waanwake wanaweza kuyana mabadiliko hayo mapema kabisa. Ila tambuwa kuwa mabadiliko hayo yote yanaweza kuwa ni vyanzo vya sababu zingine na si ujauzito.



Mabadiliko hayo ni kama:-

  1. Kuongezeka kwa joto la mwili. Kama ulizingatia vyema joto la mwili wako wakati ukiwa katika siku za hatari linakuwa kubwa kulinganisha ziku za nyuma. Baada ya kushiriki tendo la ndoa angalia je joto litapunguwa ama kuongezeka. Kama litapunguwa baada ya kupita siku za hatari huwenda bado hujabeba ujauzito. Lakini endapo utaona joto halipungui na huwenda likaongezeka hii huonyesha kuwa una mabadiliko kwenye mwili wako ambayo huwenda ni ujauzito. Jifunze pia kutofautisha kati ya homa na joto la kawaida.


  1. Majimaji kwenye uke na njia ya kuelekea kwenye tumbo la mimba. Kikawaida wakati wa siku za hatari kiasi cha majimaji kwenye uke huongezeka, hii ni kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kuweza kubeba mimba. Zinapopita siku za hatari majimaji hupunguwa na hatimaye kurudi hali ya kawaida ya ukavu. Sasa endapo majimaji hayatapunguwa na vinginevyo yakawa yanabadilika na kuwa mazito kuliko hapo mwanzo hii huashiria huwenda amebeba ujauzito.


  1. Ok sasa zingatia ziku zako za hatari.kama ulishiriki tendo la ndoa katika siku hatari kisha ukaanza kuona mabadiliko kama kutokwa na damu chache iliyo tofauti na hedhi, ama maumivu ya tumbo ya ghafla, ama kichwa kuhisi chepesi mabadiliko kama haya na mengineyo huashiria ujauzito.


  1. Mabadiliko ya rangi kwenye chuchu na mashavu ya uke yanaweza kuwa n dalili ya ujauzito. Matiti kuuma ama kuwa magumu hii ni katika dalili wanayoiona wengi katka wanawake. Mashavu ya uke hubadilika kuwa na uweuzi ama uwekundu kutokana na mishipa ya damu kuja juu na kupitisha damu kwa wingi maeneo ya chini ili kuandaa ukuaji wa mimba.


NI ZIPI DALILI ZA MWANZO ZA MIMBA KUANZIA SIKU YA KWANZA?

Yes kama tulivyoona hapo juu, mabadiliko hayo sio rahisi kutokea kutoka siku ya kwanza, ila yes mwili huanza kuonyehsa mabadiliko ya ndani punde tu mimba inapoingia, lakini kwa mwanamke kuhusi mabadiliko hayo inaweza kuchukuwa muda. Sasa hapa tutaziona kwa ufupi orodha ya dalili za mimba changa:

  1. Kuingezeka kwa joto la mwili
  2. Kuongezeka kwa maimaji ya ukeni
  3. Kutoka na damu kidogo nyepesi
  4. Maumivu ya matiti na kujaa ama kuwa magmu
  5. Mabadiliko ya rangi kwenye matiti na mashavu ya uke
  6. Kutoziona siku zako
  7. Kichwa kuwa chepesi
  8. Maumivu ya kichwa, tumbo na kizunguzungu
  9. Kichefuchefu na kutapika
  10. Kukojoa mara kwa mara
  11. Maumivu ya tumbo


JE KAMA SIO MIMBA NINI KITAKUWA.

Si kila dalili za mimba zinamaanisha ni kweli una ujauzito. Unaweza kuona dalili za mimba lakini ukawa huna. Sababu zinazoweza kupelekea hali hii ni kama:-

  1. Mabadiliko ya homoni
  2. Mashambulizi ya bakteria na virusi kwenye ufumo wa mkojo na mfumo wa uzazi
  3. Vyakula
  4. Mazingira
  5. Maradhi mengineyo yahusuyo mfumo wa uzazi

Soma zaidi kuhusu ujauzito



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 12837


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Nikila tumbo linauma, mdomo mchungu, matiti yanauma na hedhi sijapata, je ni dalili za mimba?
Mdomo kuwa mchungu ni halia mabayo haiashirii ishara mbaya za kiafya. Mdomo unaweza kuwa mchungu kutokana na vyakula. Pia hutokea ikawa ni ishara ya baadhi ya maradhi, ama ni matokeo ya baadhi ya shda za kiafya. Je vipi kuhusu maumivu ya matiti na tumb? Soma Zaidi...

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito. Soma Zaidi...

je kutokwa na maji mengi wakati wa tendo la ndoa inaashilia nini?
Je kutokwa na maji ukeni ambayo hayana harufu na meupe Hadi kuroanisha chupi, na je kutokwa na maji mengi wakati wa tendo la ndoa inaashilia nini? Soma Zaidi...

Namna ya kutunza uke
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke. Soma Zaidi...

Uchafu unaotoka ukeni na rangi zake.
Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi. Soma Zaidi...

Dalili za mimba changa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba changa Soma Zaidi...

Njia za kuzuia ugumba
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia ugumba, ni njia ambazo utumiwa na wapenzi ambao wameshindwa kupata watoto hasa kwa wale ambao wamezaliwa wakiwa na uwezo wa kupata watoto lakini kwa sababu tofauti tofauti wanashindwa kupata watoto kwa hiyo njia zifu Soma Zaidi...

Tatizo la kutokwa na utelezi wenye damu baada ya hedhi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi. Soma Zaidi...

Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea
Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeย  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu. Soma Zaidi...

Upungufu wa homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili. Soma Zaidi...

Zijuwe Dalili za minyoo na dalili kuu 9 za minyoo
Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini Soma Zaidi...

Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu. Soma Zaidi...