picha

FAIDA ZA MATUNDA

Somo hili linakwenda kukuletea faida za MATUNDA mbalimbali na mboga, upatikanaji wake na faida zake kiafya. Pia utakwenda kuona MATUNDA na mboga ambayo Ni kinga dhidi ya maradhi hatari Kama kisukari, saratani, maradhi ya moyo na mfumo wa fahamu pamoja na

1. Faida za kula zabibu

1. Zabibu Lina virutubisho vingi Kama vile vitamin C, B6 na K pia fati na madini ya shaba na manganese

2. Ina antioxidants zinazohusika kuondoa sumu za kemikali za vyakula mwilini

3. Hupunguza athari na hatari za magonjwa Kama vile kisukari, saratani na maradhi ya moyo na mishipa ya damu

4. Huondoa stress na misongo ya mawazo

5. Hushusha shinikizo la damu

6. Hupunguza cholesterol mbaya

7. Hushusha kiwango cha sukari kwenye damu

8. Husaidia kuimarisha afya ya macho

9. Huimarisha afya ya ubongo na utunzaji wa kumbukumbu

10. Husaidia kuboresha afya ya mifupa

11. Husaidia kupunguza maambukizi ya baadhi ya bakteria, fangasi na virusi

12. Hupunguza kasi ya kuzeeka mapema

 

2. Faida za kula nanasi

1. Nanasi Lina virutubisho Kama vile fati, protini, vitamin C na B6, madini ya chuma, manganese na shaba

2. Hupunguza misongo ya mawazo (stress)

3. Nanasi ni rahisi kumeng'enywa tumboni

4. Hupunguza hatari ya ugonjwa wa saratani

5. Huboresha na kuimarisha mfumo wa kinga mwilini

6. Hupunguza maumivu ya viungio

7. Husaidia kupona haraka baada ya kufanyiwa upasuaji

8. Ni tunda tamu

 

3. Faida za kula parachichi

1. Parachichi Lina virutubisho Kama vile wanga, vitamin C, E,K pia lina madini ya magnesium na potassium

2. Husaidia kuboresha na kuimarisha afya ya moyo

3 husaidia kupunguza kupata kwa ugonjwa wa mifupa kuwa dhaifu

3. Huzuia na kupunguza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani

4. Huboresha afya ya watoto wadogo na ukuaji wao

5. Hupunguza misongo ya mawazo

6. Huondoa tatizo la kutopata choo kikubwa

7. Husaidia kuondoa sumu za vyakula na kemikali mwilini

8. Husaidia kupunguza maambukizi ya baadhi ya bakteria fangasi na virusi

9. Husaidia kutokupata maradhi ya kisukari

 

4. Faida za kula apple(tufaha)

1. Tufaha Lina virutubisho vingi Kama vile vitamin C, K, E, B1, B2 na B6 pia madini ya potassium

2. Husaidia kupunguza uzito wa ziada mwilini

3. Husaidia kuboresha na kuimarisha afya ya moyo

4. Hupunguza athari za ugonjwa wa kisukari

5 husaidia kupambana na pumu

6. Husaidia kuzuia saratani

7. Husaidia kuboresha na kuimarisha afya ya mifupa

8. Hulinda tumbo dhidi ya majeraha yanayotokana na matumizi ya madawa

9. Husaidia kuimarisha afya ya ubongo

 

5. Faida za kula Embe

1. Huzuia tatzo la kukosa choo kikubwa

2. Huboresha mfumo wa kinga

3. Huimarisha afya ya macho

4. Hupunguza cholesterol mbaya

5. Huboresha muonekano wa ngozi na kuufanya uwe na afya njema

6. Embe ni zuri hata kwa wenye kisukari

7. Husaidia katika kupunguza uzito

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views 2176

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 web hosting     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Kazi za vitamini B na vyakula vya vitamini B

Makala hii inakwenda kukuletea kazi za vitamini B, pia tutajwenda kuona makundi ya vitamini B na kazi za kila kundi. Pia makala hii inakwenda kukufundisha vyanzo na vyakula vya vitamini B. Utajifunza pia kazi kuu za vitamini B kwa ujumla wake.

Soma Zaidi...
Faida za karoti

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za karoti na umuhimu wake kiafya

Soma Zaidi...
Vyakula murajabu kea mwenye presha ya kushuka

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula murajabu kea mwenye presha ya kushuka

Soma Zaidi...
Zijuwe faida za kula njegere

zijuwe faida za kula njegere kiafya na umuhimu wa kula jegere pia jifunze njegere zina kazi gani mwilini?

Soma Zaidi...
Vyakula vya wanga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za vyakula vya wanga na umuhimu wake mwilini

Soma Zaidi...