FAIDA ZA MATUNDA

FAIDA ZA MATUNDA

Somo hili linakwenda kukuletea faida za MATUNDA mbalimbali na mboga, upatikanaji wake na faida zake kiafya. Pia utakwenda kuona MATUNDA na mboga ambayo Ni kinga dhidi ya maradhi hatari Kama kisukari, saratani, maradhi ya moyo na mfumo wa fahamu pamoja na

1. Faida za kula zabibu

1. Zabibu Lina virutubisho vingi Kama vile vitamin C, B6 na K pia fati na madini ya shaba na manganese

2. Ina antioxidants zinazohusika kuondoa sumu za kemikali za vyakula mwilini

3. Hupunguza athari na hatari za magonjwa Kama vile kisukari, saratani na maradhi ya moyo na mishipa ya damu

4. Huondoa stress na misongo ya mawazo

5. Hushusha shinikizo la damu

6. Hupunguza cholesterol mbaya

7. Hushusha kiwango cha sukari kwenye damu

8. Husaidia kuimarisha afya ya macho

9. Huimarisha afya ya ubongo na utunzaji wa kumbukumbu

10. Husaidia kuboresha afya ya mifupa

11. Husaidia kupunguza maambukizi ya baadhi ya bakteria, fangasi na virusi

12. Hupunguza kasi ya kuzeeka mapema

 

2. Faida za kula nanasi

1. Nanasi Lina virutubisho Kama vile fati, protini, vitamin C na B6, madini ya chuma, manganese na shaba

2. Hupunguza misongo ya mawazo (stress)

3. Nanasi ni rahisi kumeng'enywa tumboni

4. Hupunguza hatari ya ugonjwa wa saratani

5. Huboresha na kuimarisha mfumo wa kinga mwilini

6. Hupunguza maumivu ya viungio

7. Husaidia kupona haraka baada ya kufanyiwa upasuaji

8. Ni tunda tamu

 

3. Faida za kula parachichi

1. Parachichi Lina virutubisho Kama vile wanga, vitamin C, E,K pia lina madini ya magnesium na potassium

2. Husaidia kuboresha na kuimarisha afya ya moyo

3 husaidia kupunguza kupata kwa ugonjwa wa mifupa kuwa dhaifu

3. Huzuia na kupunguza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani

4. Huboresha afya ya watoto wadogo na ukuaji wao

5. Hupunguza misongo ya mawazo

6. Huondoa tatizo la kutopata choo kikubwa

7. Husaidia kuondoa sumu za vyakula na kemikali mwilini

8. Husaidia kupunguza maambukizi ya baadhi ya bakteria fangasi na virusi

9. Husaidia kutokupata maradhi ya kisukari

 

4. Faida za kula apple(tufaha)

1. Tufaha Lina virutubisho vingi Kama vile vitamin C, K, E, B1, B2 na B6 pia madini ya potassium

2. Husaidia kupunguza uzito wa ziada mwilini

3. Husaidia kuboresha na kuimarisha afya ya moyo

4. Hupunguza athari za ugonjwa wa kisukari

5 husaidia kupambana na pumu

6. Husaidia kuzuia saratani

7. Husaidia kuboresha na kuimarisha afya ya mifupa

8. Hulinda tumbo dhidi ya majeraha yanayotokana na matumizi ya madawa

9. Husaidia kuimarisha afya ya ubongo

 

5. Faida za kula Embe

1. Huzuia tatzo la kukosa choo kikubwa

2. Huboresha mfumo wa kinga

3. Huimarisha afya ya macho

4. Hupunguza cholesterol mbaya

5. Huboresha muonekano wa ngozi na kuufanya uwe na afya njema

6. Embe ni zuri hata kwa wenye kisukari

7. Husaidia katika kupunguza uzito

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views: 2524

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 ai web app     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Namna nzuri ya kuandaa mchai chai kwa matumizi mbalimbali

Posti hii inahusu zaidi namna nzuri ya kuandaa mchai chai kwa ajili ya matumizi mbalimbali, Ili kutumia mmea wa mchai chai zifuatazo ni mbinu za kuandaa mmea huu.

Soma Zaidi...
Vyakula vinavyoweza kuboresha afya ya akili na utendaji wa ubongo.

Ubongo wako ni kama injini ya gari inayofanya kazi masaa 24, hata ukiwa umelala. Mafuta unayoweka kwenye injini hiyo (vyakula unavyokula) ndiyo yanayoamua kama itafanya kazi kwa ufanisi mkubwa au itachoka mapema. Makala haya yanakuletea orodha ya vyakula vyenye uwezo mkubwa wa kuboresha kumbukumbu, kuongeza umakini, na kulinda afya yako ya akili dhidi ya msongo wa mawazo na unyogovu

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume

Vijuwe vyakula vya kyongeza nguvu za kiume na mambo yanayopunguza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
Faida za kula stafeli/soursop

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za stafel/soursop

Soma Zaidi...
Vyakula Vya vitamini B, kazi za Vitamini B na dalili za Upungufu wa Vitamini B mwilini

hapa Tutakwenda kuona Vyakula Vya vitamini B, kazi za Vitamini B na dalili za Upungufu wa Vitamini B mwilini

Soma Zaidi...