Faida za kula Palachichi

Palachichi lina virutubisho vingi na vitamini, kula palachichi uiokoe afya yako

Faida za kula Palachichi

3.Palachichi (avocado)

Hili ni katika matunda yenye fat (mafuta). Itambulike kuwa si kila mafuta ni hatari ndani ya miili yetu. Tunahitaji vyakula vya fat yaani mafuta kwa ajili ya kutupatia joto kwenye miili yetu. Pia fati husaidia kuipa miili yetu nguvu. Katika tunda hili palachichi mafuta yake ni aina ya oleic acid yaani yapo katika aina flani ya asidi ambayo husaidia katika kupunguza uvimbe mwilini na kusaidia kuboresha afya ya moyo.

Palachici pia hutambulika kitaalamu kuwa lina lina madini ya potassium na magnesium kwa wingi sana. Pia ni katika vyakula vyenye kambakamba yaani fiber. Vyakula hivi vyenye fiber husaidia katika kuweka usalama wa tumbo yaani kuhakikisha chakula kinatembea ipasavyo ndani ya tumbo kutoka sehemu moja mpaka sehemu nyingine mpaka kufika kwenye njia ya haja kubwa.

Pia tunda hili husaidia kupungusa hatari za kupata maradhi ya stroke yaani kupalalaizi kutokana na kiwango kikubwa cha madini ya magnessium ambayo husaidia katika kupunguza shinikizo kubwa la damu. Hivyo palachichi husaidia katika kudhibiti afya ya moyo. Palachichi moja linaweza kutoa 28% ya mahitaji ya mwili ya madini haya.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1721

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Upungufu wa protini na dalili zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu upungufu wa protini na dalili zake

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula maini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula maini

Soma Zaidi...
Vyakula vyenye vitamini C kwa wingi

Vitamini C kwa wingi hupatikana kwenye machungwa, maembe, mananasi, limao na ndimu

Soma Zaidi...
Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo, na vyakula salama kwa vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Namna nzuri ya kuandaa mchai chai kwa matumizi mbalimbali

Posti hii inahusu zaidi namna nzuri ya kuandaa mchai chai kwa ajili ya matumizi mbalimbali, Ili kutumia mmea wa mchai chai zifuatazo ni mbinu za kuandaa mmea huu.

Soma Zaidi...
Faida za kula Pilipili

Usiogope kuwashwa, kula pilipili ni nzuri kwa afya yako ia virutubisho vingi sana

Soma Zaidi...
FAIDA ZA KULA ZABIBU

Somo hili litakwenda kukueleza kuhusu faida za kula zabibu na umuhimu wake kiafya

Soma Zaidi...
VYANZO VYA VYAKULA VYA VITAMINI NA FAIDA ZAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...