Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.
Fahamu dawa mbalimbali za kutibu minyoo .
1. Kama nilivyoeleza hapo juu kwamba kuna dawa mbalimbali za kutibu minyoo, kabla ya kuona dawa hizo tunapaswa kujua aina mbalimbali za minyoo ambazo usababisha ugonjwa kwa binadamu na pia tutaweza kuonesha dawa hizo.
2. Kama tunavyojua kwamba kuna makundi mbalimbali ya minyoo ambayo kwa kitaalamu huitwa Nematode, cestode na Trematode na pia kila kundi lina makundi yake na makundi hayo utibiwa kwa dawa tofauti kutokana na mnyoo uliosababisha ugonjwa huo.
3. Kuna kundi la nematode ambalo lina makundi madogo madogo kama vile giant roundworms, pinworms, hookworms, whipworm na thread worm hiyo minyoo utibiwa na dawa zake maalum kadri ya kundi lilivyo.
4. Kundi la pili ni kundi ambalo kwa kitaalamu huitwa cestode, na huwa na kundi lake ambalo ni beef tapeworm minyoo inayopatikana kwenye nyama, pork tape worm ni minyoo inayopatikana kwenye nyama ya nguruwe, fish tape worm ni minyoo inayopatikana kwenye samaki, hili kundi nalo lina dawa zake kama tutakavyokuja kuchambua moja na nyingine.
5. Kundi lingine kwa kitaalamu linajulikana kama Trematodes na lenyewe lina makundi yake madogo madogo kama vile blood fluke, intestine fluke, lungs fluke, liver fluke,Clonorchis sinensis, na pia hili kundi lina dawa zake maalum za kutibu kulingana na sehemu na aina ya mnyooo kwa hiyo baada ya kujua minyoo mbalimbali ni vizuri kufahamu na dawa zake kama ifuatavyo.
6. Dawa za kutibu minyoo
- Dawa hizi utumika kutibu aina mbalimbali za minyoo kadri ya makundi au kadri ya mnyoo mwenyewe aliyesababisha ugonjwa, dawa zenyewe ni kama ifuatavyo.
- Mebendazole
- Albendazole
- Levamisole
- Niclosamide
- Thiabendazole
7.Pia dawa hizi huwa na maudhi mbalimbali ambayo ni kama vile maumivu ya tumbo, kutapika, kuharisha, kizunguzungu na maudhi madogo madogo kama hayo ila uisha taratibu na pia katika matumizi ya dawa hizi hali ya maudhi ikizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya kwa maelekezo zaidi.
8. Kwa hiyo hizi dawa hazitumiwa kiholela kuna watu ambao hawapaswi kutumia dawa fulani na wengine wanapaswa kutumia kwa hiyo tutaenda kuchambua dawa moja baada ya nyingine hapo mbeleni.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Dawa ya kutibu mapunye
DAWA YA MAPUNYEMatibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo.
Soma Zaidi...Dawa mbadala za vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa mbadala za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya mebendazole
Post hii inahusu zaidi dawa ya mebendazole ni dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo utokea kwa watoto na watu wazima.
Soma Zaidi...Fahamu Dawa inayotumika kupunguza maumivu (ibuprofen)
Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin,
Soma Zaidi...Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo
Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya ALU au kwa lugha nyingine ni dawa ya mseto
Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
Soma Zaidi...