Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.
Fahamu dawa mbalimbali za kutibu minyoo .
1. Kama nilivyoeleza hapo juu kwamba kuna dawa mbalimbali za kutibu minyoo, kabla ya kuona dawa hizo tunapaswa kujua aina mbalimbali za minyoo ambazo usababisha ugonjwa kwa binadamu na pia tutaweza kuonesha dawa hizo.
2. Kama tunavyojua kwamba kuna makundi mbalimbali ya minyoo ambayo kwa kitaalamu huitwa Nematode, cestode na Trematode na pia kila kundi lina makundi yake na makundi hayo utibiwa kwa dawa tofauti kutokana na mnyoo uliosababisha ugonjwa huo.
3. Kuna kundi la nematode ambalo lina makundi madogo madogo kama vile giant roundworms, pinworms, hookworms, whipworm na thread worm hiyo minyoo utibiwa na dawa zake maalum kadri ya kundi lilivyo.
4. Kundi la pili ni kundi ambalo kwa kitaalamu huitwa cestode, na huwa na kundi lake ambalo ni beef tapeworm minyoo inayopatikana kwenye nyama, pork tape worm ni minyoo inayopatikana kwenye nyama ya nguruwe, fish tape worm ni minyoo inayopatikana kwenye samaki, hili kundi nalo lina dawa zake kama tutakavyokuja kuchambua moja na nyingine.
5. Kundi lingine kwa kitaalamu linajulikana kama Trematodes na lenyewe lina makundi yake madogo madogo kama vile blood fluke, intestine fluke, lungs fluke, liver fluke,Clonorchis sinensis, na pia hili kundi lina dawa zake maalum za kutibu kulingana na sehemu na aina ya mnyooo kwa hiyo baada ya kujua minyoo mbalimbali ni vizuri kufahamu na dawa zake kama ifuatavyo.
6. Dawa za kutibu minyoo
- Dawa hizi utumika kutibu aina mbalimbali za minyoo kadri ya makundi au kadri ya mnyoo mwenyewe aliyesababisha ugonjwa, dawa zenyewe ni kama ifuatavyo.
- Mebendazole
- Albendazole
- Levamisole
- Niclosamide
- Thiabendazole
7.Pia dawa hizi huwa na maudhi mbalimbali ambayo ni kama vile maumivu ya tumbo, kutapika, kuharisha, kizunguzungu na maudhi madogo madogo kama hayo ila uisha taratibu na pia katika matumizi ya dawa hizi hali ya maudhi ikizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya kwa maelekezo zaidi.
8. Kwa hiyo hizi dawa hazitumiwa kiholela kuna watu ambao hawapaswi kutumia dawa fulani na wengine wanapaswa kutumia kwa hiyo tutaenda kuchambua dawa moja baada ya nyingine hapo mbeleni.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya mucolytic dawa ya kutibu kikohozi
Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto.
Soma Zaidi...Fahamu aina ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu
Post hii inahusu zaidi aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, dawa hii kwa kitaamu huiitwa procaine benzyl penicillin.
Soma Zaidi...Dawa ya kutibu mapunye
DAWA YA MAPUNYEMatibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya haloperidol katika matibabu ya akili
Post hii inahusu dawa ya haloperidol katika matibabu ya magonjwa ya akili, ni mojawapo ya dawa ambayo utumiwa na wagonjwa ambao wamechananyikiwa.
Soma Zaidi...Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu
Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.
Soma Zaidi...