Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.
Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin .
1. Ni mojawapo ya dawa inayotumika kutibu fungasi za kwenye ngozi tu, pia iko kwenye mfumo wa mafuta mafuta hivi, au oil, cream kwa hiyo upakwa kwa mafuta.ni vizuri kabisa kutumiwa kwenye ngozi tu ikitumia kwa namna nyingine ni hatari kwa hiyo ni vizuri kuwaambia watumiaji kwamba makini katika kutumia dawa hii kwa sababu ikitumiwa vinginevyo tofauti na kwenye ngozi ni hatari sana.
2.pia dawa hii haiwezi kumengenywa kama dawa nyingine ambazo umengenywa kwenye mfumo wa chakula ndio maana ni hatari sana ikitumika kwenye system ya chakula, pia dawa hii usaidia kwenye kandida za sehemu mbalimbali kwa mfano dawa hii inaweza kutibu kandida ya kwenye sehemu za siri kwa kupaka dawa hiyo kwenye sehemu za siri.
3. Namna ya kutumia dawa hizi, unanawa mikono kwanza ili kuepuka kuingiza wadudu kwenye dawa , unakuwa tayari umeshasafisha sehemu ambayo unataka kupaka dawa hiyo ,unakaushaa sehemu hiyo vizuri kwa kitambaa kizuri,unapaka dawa yako kadri ya maelekezo ya wataalamu wa afya, kama ni sehemu za siri ni vizuri kabisa kutumia dawa hiyo wakati wa kupumzika au wakati wa usiku ili kuruhusu dawa ifanye kazi yake vizuri.
4. Pengine anayetumia dawa ni mgonjwa ambaye hajiwezi ni vizuri kabisa kumpaka au pengine ni mtoto ambaye hawezi kujihudumia mwenyewe ni vizuri kumpaka na kuzingatia kwamba hakuna kusambaza ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, pia kabla ya kutumia dawa nyingine baada ya kujipaka ni vizuri kabisa kuoga dawa ile ya kwanza na hakikisha unazingatia usafi katika matumizi ya dawa hii.
5. Katika matumizi ya dawa hii zingatia kwamba dawa hii utumika kwenye ngozi ya nje tu na ikitumiwa kwa njia yoyote ni hatari kwa afya kwa hiyo ni vizuri kabisa kuweka dawa hii mbali na watoto ili kuepuka hatari ya kutumia dawa hii kama mafuta au pengine wanaweza Kulamba au kula na mambo kama hayo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kutumia dawa hizi kwa ushauri wa wataalamu wa afya kwa sababu bila ushauri wao matumizi mengine yanaweza kuwa sio sahihi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Fahamu dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi.
Soma Zaidi...Ushauri kabla ya kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi ushauri kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, kabisa ya kubeba mimba akina Mama na wachumba wanapaswa kufanya yafuatayo.
Soma Zaidi...Dawa ya vidonda vya tumbo
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Kazi ya Dawa ya salbutamol
Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.
Soma Zaidi...Dawa ya quinenes katika kutibu Malaria
Post hii inahusu zaidi dawa e quinine katika kutibu Malaria ni dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ikiwa dawa nyingine zimeshindwa kufanya kazi.
Soma Zaidi...