Fahamu kuhusu dawa ya mebendazole
Post hii inahusu zaidi dawa ya mebendazole ni dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo utokea kwa watoto na watu wazima.
Fahamu kuhusu dawa ya mebendazole .
1. Dawa hii ni mojawapo kwa dawa ambazo zimependekezwa kutibu ugonjwa wa minyoo, hii dawa ikitumika inavyopaswa uwezo wa kuua minyoo ni kwa kiwango kikubwa sana kwa sababu uua aina mbalimbali za minyoo kama ifuatavyo. Aina hii ya minyoo imo kwenye lugha ya kitaalamu kwa majina yake lakini lengo ni kuua minyoo majina hayo ni hookworm, thread worm, round worm na whipworm hao wote ni aina ya minyoo.
2. Kwa watumiaji wa dawa hii kwa kawaida uitumia kabla ya chakula au baada ya kumaliza kula chakula na kwa kawaida utafunwa na kumezwa na iko kwenye mfumo wa vidonge .
3. Dawa hi inaweza kutumika kwa watu mbalimbali watoto na watu wazima ila haipaswi kutumiwa na watoto chini ya miaka miwili na pia wanawake wenye mimba changa kwa sababu dawa hii inawezekana kutoa mimba changa na kwa watoto wadogo wenye chini ya miaka miwili uweza kupata degedege ikiwa wanatumia dawa hii mara kwa mara.
4. Pia dawa hii inawezekana kuleta maudhui madogo madogo kwa watumiaji kama vile maumivu ya tumbo na tumbo kujaa gesi, maumivu ya kichwa na pia kichefuchefu na kutapika.
5. Kwa sababu dawa hii ina madhara kwa watoto na mama wenye mimba changa ni vizuri kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 web hosting 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin
Soma Zaidi...Ijue dawa ya sulphadoxine na pyrimethamine (sp)
Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria.
Soma Zaidi...Tiba mbadala za vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Faida za vidonge vya antroextra
Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya antroextra, ni vidonge kwa ajili ya mifupa, viungo na gegedu, hivi vidonge vimetumiwa na watu wengi na matokeo yake ni mazuri sana, kwa hiyo zifuatazo ni faida za vidonge hivi.
Soma Zaidi...Matibabu ya ugonjwa wa uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mgonjwa wa uti wa mgongo, kwa kawaida tunajua kuwa homa hii ya uti wa mgongo usababisha na wadudu mbalimbali kama vile bakteria, virus, fungasi, sumu mbalimbali kama vile madini ya lead na arseni, na vitu kama vile Mag
Soma Zaidi...