Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea.
1. Kama tunavyojua kwamba kikohozi ni ugonjwa ambao uwapata watu wengi na uleta usumbufu sana hasa kwa watoto na wazee, basi kwa kutumia dawa ya expectorant inaweza kutibu kikohozi kwa sababu dawa hii ufanya kazi kwa kuhakikisha makohozi na material yote yaliyomo kwenye mapafu yanatolewa na kufanya mapafu,koo kuwa huru.
2. Pia dawa hii inapoingia kwenye mwili uhakikisha kwamba sehemu ya kwenye mfumo wa hewa ambayo kwa kitaalamu huitwa bronchial inakuwa safi bila makohozi na inafanya makohozi yaliyozalishwa yanakuwa mepesi na kwa hiyo hata mgonjwa anapokohoa hapati shida zaidi na pia kwa kutumia dawa hii ya expectorant usaidia maumivu kupungua na matibabu yanaweza kuwa mepesi zaidi.
3. Dawa hizi ya expectorant ina maudhui madogo madogo kama vile kichefuchefu na kutapika na pia kwa mara nyingine mgonjwa anaweza kuhisi kubwa na usingizi au mwili kulegea wakati akiwa anatumia dawa hii kwa hiyo ni vizuri kabisa na kujua kwamba hizi ni dalili za kawaida kwa mgonjwa mwenye kutumia dawa hii.
4. Pia dawa hizi utumiwa na watu mbalimbali ambao wana kikohozi na kwa wale wenye shida au aleji na dawa hizi hawapaswi kuitumia kwa sababu wanaweza kupata matatizo yatokanayo na kutoelewana kati ya mtumiaji na dawa yenyewe.
5. Katika matumizi ya dawa hii ni kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya dawa hizi haitumiki kiholela ila kabla ya kuanza kutumia ni vizuri kujua namna unavyopaswa kutumia, uitumia mara ngapi na kazi yake ni nini baada ya kujua hayo unaweza kuitumia na matokeo natumaini yatakuwa mazuri zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici
Soma Zaidi...Zijuwe aina za minyoo na tiba yake. Dawa 5 za kutibu minyoo ya aina zote
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za mitishamba za kutibu meno
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa mbadala za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya isoniazid katika mapambano na kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu ni hatari katika jamii kwa hiyo dawa ya isoniazid ni mkombozi katika mapambano na kifua kikuu.
Soma Zaidi...