Fahamu aina ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu
Post hii inahusu zaidi aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, dawa hii kwa kitaamu huiitwa procaine benzyl penicillin.
Fahamu kuhusu dawa ya procaine benzyl penicillin.
1. Ni aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, kwa sababu yenyewe udili na bakteria ambao ushambulia mwili na kusababisha madhara ya mda mrefu na kwa hiyo ikiingia mwili inawezekana kukaa kwa masaa Ili kuweza kudili na bakteria ambao wameleta madhara ya mda mrefu.
2. Kwa kawaida dawa hii utumika kutibu maambukizi mbalimbali ya bakteria ambayo ujitokeza kwenye mwili wa binadamu na pia utumika kwa watu wazima na watoto kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya na pia kwenye kundi hili Kuna dawa nyingine ambayo Kwa kitaamu huiitwa fortified procaine penicillin nayo ufanya kazi kama procaine benzyl penicillin.
3. Dawa hii kwa kawaida huwa kwenye mfumo wa unga na huwa kwenye ki chupa Fulani hivi na pia uchanganywa na maji maalumu kwa ajili ya dawa ambayo Kwa kitaamu huiitwa sterile water,na uchanganywa kwa pamoja , yaani dawa na maji na pia utikiswa kumhakikishia kuwa unga umachanganyika kabisa na maji .
4. Dose kwa mgonjwa utegemea mtoto na mtu mzima,uzito na umri wa mtu,na pia dawa hii inaweza kutolewa kwa kupigwa sindano kwenye mapaja au Tako, na kwa wakati mwingine uweza kupitia kwenye damu, kwa hiyo mchanganyiko wa kupitia kwenye paja au Tako ni tofauti na ule mchanganyiko wa kupitia kwenye mishipa ya damu.
5. Dawa hii pia utumiwa na watu mbalimbali ila kwa wale wote wenye aleji na dawa ya penicillin hawapaswi kutumia dawa hii, kwa hiyo watatumia dawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya.
6. Pia dawa hii Ina maudhi madogo madogo baada ya kuitumia, maudhi yenyewe ni kama maumivu kwenye jointi, unaweza kupata upungufu wa damu ukiitumia kwa mda mrefu, kwa hiyo wenye tatizo la upungufu wa damu wanapaswa kuitumia kwa taahadhari,pia dawa hazipaswi kutumiwa kiholela Bali ni kwa ushauri wa wataalamu wa afya.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Dawa za kutibu kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia
Soma Zaidi...Ijue Dawa ya lignocaine
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji.
Soma Zaidi...Dawa ya kutibu UTI
Nitakujuza dalili za UTI na dawa za kutibu UTI. Pia tutaona njia za kujikinga na UTI pamoja na dalili za UTI
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Dawa za mitishamba za kutibu meno
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za mitishamba za kutibu meno
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa
Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili.
Soma Zaidi...