Hapa utakwendabkuijuwabhistoria ya uandishi wa hadithi. Pia utaijuwa sababu iliyopelekea uandishi wa hadithi kuwa mdogo .
Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.a.w)
Tofauti na Qur-an, ambayo iliandikwa mara tu baada ya kushushwa chini ya malekezo na usimamizi wa Mtume (s.a.w) mwenyewe, Hadith za Mtume (s.a.w) ambamo ndani yake ndio tunapata sunnah yake, zimeandikwa na watu kulingana na walivyomuona, au walivyomsikia. Historia ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.a.w) katika vitabu vya Hadith , imechukua takriban muda wa karne tatu. Kwa kurahisisha tutaigawa historia ya kuhifadhiwa Hadith katika maandishi katika hatua nne zifuatazo: - Wakati wa Mtume (s.a.w).
- Wakati wa Maswahaba wa Mtume (s.a.w).
- Wakati wa Tabi'iina.
- Wakati wa Tabii Tabi'iina.
Wakati wa Mtume (s.a.w)
Wakati wa Mtume (s.a.w), hapakuwa na uandishi mkubwa wa Hadith kwa sababu:
Kwanza, Mtume mwenyewe alikuwepo, hivyo kilichokuwa muhimu kwa Masahaba ni kufuata mafundisho ya Mtume(s.a.w) na kuigiza mwenendo wake,kila walipokwama katika utendaji au kila walipotatizwa na tatizo lolote, walimwendea Mtume(s.a.w) na aliwakwamua au kuwatatulia tatizo lolote walilokuwa nalo.
Pili, Masahaba katika kipindi hiki walijishughulisha sana na kuandika, kusoma na kuhifadhi Qur-an moyoni na kuitekeleza katika maisha yao ya kila siku.
Tatu, kwa kuwa mwanzoni Mtume (s.a.w) aliwakataza Masahaba wake kuandika Hadith, walizoea kutoandika Hadith hata wakati waliporuhusiwa kuandika na walipendelea kutoandika kuliko kuandika Hadith.
Nne, katika wakati huu wa Mtume (s.a.w) Masahaba walishughulika sana katika harakati za kuuhami Uislamu ambao ulikuwa umesongwa sana na maadui wake ambao walipania sana kumuua Mtume, Uislamu na Waislamu.
Kutokana na sababu hizi nne na nyinginezo, uandishi wa Hadith haukupewa nafasi nzito katika kipindi hiki cha Mtume (s.a.w). Hivyo, Hadith nyingi zilibakia katika matendo na vifua vya Masahaba. Masahaba waliokuwa karibu sana na Mtume (s.a.w) kwa muda mrefu wa maisha yao, walihifadhi Hadith nyingi zaidi kuliko wale waliokaa mbali na Mtume (s.a.w).
Miongoni mwa Masahaba waliofahamika kuwa mashuhuri kwa kuhifadhi Hadith nyingi ni Abu Hurairah, bibi Aysha (mkewe Mtume (s.a.w)) 'Abdullah bin 'Umar, 'Abdullah bin 'Abbas, na Abdullah bin 'Amr na Abdallah bin Masu'ud (r.a)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu “LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha ni nyakati zipi ambazo Allah hukubali dua kwa urahisi.
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukufundisha maneno unayotakiwa kuyasema unapozuru makaburi.
Soma Zaidi...عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صل?...
Soma Zaidi...