picha

Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kushoto

MAUMIVU YA TUMBO KWA CHINI UPANDE WA KUSHOTO

 

Sehemu ya kushoto ya tumbo lako kwa chini hupatikana mwishilizo wa utumbo mkubwa. Pia kwa upande wa wanawake sehemu hii hupatikana ovari ya kushoto. Katika hali za kawaida maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto sio jambo la kuogopesha sana. Kwani maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe bila ya kuhitaji uangalizi wa kidaktari.

 

Je na wewe ni mmoja kati ya wanaosumbuliwa na maumivu ya tumbo kwa shini upande wa kushoto? Je una muda gani na tatizo hili?. makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza sababu za maumivu ya tumbo sehemu ya chini upand wa kushoto.

 

Kama nilivyotangulia kukuijuza kuwa maumivu haya si jambo la kuogopesha. Basi ni vyema kwa haraka ukamuona daktari endapo utaona dalili zifuatazo:-A.HomaB.Sehemu husika kuwa na ugumu na maumivuC.Kuvimba kwa tumboD.Kuona damu kwenye kinyesiE.Kuendelea kuwa na kichefuchefu na kutapika kwa masik kadhaaF.Kupungua uzitoG.Ngozi kuwa na njano.

 

Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto1.Kuwa na shida kwenye utumbo mkubwa.Hii hutikea pale kwenye utumbo mkubwa kunapoota kama vijifuko vijidogo. Hivi sio jambo la kuogopa sana kiafya maana mara nyingi havina madhara na hupotea vyenyewe. Hali hii huwapata sana wenye umri zaidi ya miaka 40. sasa ikitokea vijifuko hivi vimeshambuliwa na vijidudu huvimba na kuleta maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Dalili zake ni kama:-

 

A.HomaB.KichefuchefuC.KutapikaD.Tumbo kujaa na kuiwa gumuE.KuharishaF.Kukosa choo

 

2.Gesi tumboni.Sababu nyingine ni kujaa gesi tumboni. Gesi tumboni inaweza kusababishwa na:-A.Kumeza hewa sanaB.Kula kupitilizaC.Kuvuta sigaraD.Kutafuna bigjiiE.Chakula kutokumeng’enywa vyemaF.Kula vyakula vyenye gesiG.Kuwa na bakteria kwenye utumbo mkubwa.

 

3.Kuvimbiwa ama chakula kutokumeng’enywa vyema tumboni. Hali hii huplekea maumivu ya tumbo kwa juu. Maumivu haya wakati mwingine husambaa na kuathiri chini ya tumbo upande wa kushoto. Mtu pia ataona dalili kama:-A.KiunguliaB.Kuhisi kishiba na tumbo kujaaC.Kucheua gesiD.kichefuchefu

 

4.Ngiri henia; henia ina dalili kama:-A.Kuongezeka uvimbe maeneo ya tumboni (si kila henia)B.Maumivu kuongezekaC.Maumivu wakati unaponyanyua kituD.Kujihisi umeshiba5. kuwa na vijiwe kwenye figoVijiwe vya kwenye vigo vinatokana na mkusanyiko wa madini ya chumvi. Vijiwe hivi vinaweza kutokea kwenye figo, kibofu ama maeneo mengine kwenye mfumo wa mkojo. Vijijiwe hvi vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Pia vinaweza kusababisha maumivu ya mgongo upande mmoja na nyuma pia na kwenye mbavu. Tofauti na dalili hizi pia mgonjwa anaweza kupata dalili zifuatazo:-

 

A.Mkojo wenye rangi ya kahawiya, nyekundu ama mawingu mawingu na haruu kaliB.Mkojo wenye maumivu makali unaotokea mra kwa maraC.KichefuchefuD.VomitingE.Homa

 

Maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kulia kwa wanawake, husababishwa na yafuatayo:-A.Tumbo la changoB.Kuota tishu za tumbo la uzazi maeneo mengineC.Kuwa na shida kwenye ovariD.Kuwa na ujauzito uliotungia njeE.Kuwa na ugonjwa wa PID

 

?

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 6165

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Jinsi ya Kutambua Mimba Bila Kipimo

Wakati njia ya uhakika zaidi ya kutambua mimba ni kutumia kipimo cha mkojo (test kit) au kupima damu hospitalini, kuna dalili mbalimbali za kimwili ambazo mwanamke anaweza kuzihisi katika hatua za mwanzo za ujauzito. Makala hii inaelezea ishara hizi za awali ambazo mwili hutoa ili kukuashiria kuwa kuna mabadiliko ya kibaolojia yanayoendelea ndani ya mfumo wako wa uzazi.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kitovuni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya tumbo kitovuni

Soma Zaidi...
Walio katika hatari ya kupata homa ya inni

Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata homa ya ini,kwa sababu ya hali zao mbalimbali wanaweza kupata ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Madhara ya kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtu hajatibiwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

Soma Zaidi...
Sababu za Kichwa Kuuma Mara kwa Mara

​Kichwa kuuma mara kwa mara ni changamoto inayomfanya mtu kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi. Makala hii inaangazia sababu mbalimbali za maumivu ya kichwa ya mara kwa mara, jinsi ya kuyatofautisha, na wakati mwafaka wa kutafuta msaada wa kitaalamu

Soma Zaidi...
Namna ya kugundua mtu mwenye kaswende.

Post hii inahusu zaidi njia za kumgundua mgonjwa wa kaswende, njia hizi utumika baada ya kuongea na mgonjwa kuhusu maisha yake hasa kujamiiana na watu mbalimbali.

Soma Zaidi...