picha

Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kushoto

MAUMIVU YA TUMBO KWA CHINI UPANDE WA KUSHOTO

 

Sehemu ya kushoto ya tumbo lako kwa chini hupatikana mwishilizo wa utumbo mkubwa. Pia kwa upande wa wanawake sehemu hii hupatikana ovari ya kushoto. Katika hali za kawaida maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto sio jambo la kuogopesha sana. Kwani maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe bila ya kuhitaji uangalizi wa kidaktari.

 

Je na wewe ni mmoja kati ya wanaosumbuliwa na maumivu ya tumbo kwa shini upande wa kushoto? Je una muda gani na tatizo hili?. makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza sababu za maumivu ya tumbo sehemu ya chini upand wa kushoto.

 

Kama nilivyotangulia kukuijuza kuwa maumivu haya si jambo la kuogopesha. Basi ni vyema kwa haraka ukamuona daktari endapo utaona dalili zifuatazo:-A.HomaB.Sehemu husika kuwa na ugumu na maumivuC.Kuvimba kwa tumboD.Kuona damu kwenye kinyesiE.Kuendelea kuwa na kichefuchefu na kutapika kwa masik kadhaaF.Kupungua uzitoG.Ngozi kuwa na njano.

 

Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto1.Kuwa na shida kwenye utumbo mkubwa.Hii hutikea pale kwenye utumbo mkubwa kunapoota kama vijifuko vijidogo. Hivi sio jambo la kuogopa sana kiafya maana mara nyingi havina madhara na hupotea vyenyewe. Hali hii huwapata sana wenye umri zaidi ya miaka 40. sasa ikitokea vijifuko hivi vimeshambuliwa na vijidudu huvimba na kuleta maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Dalili zake ni kama:-

 

A.HomaB.KichefuchefuC.KutapikaD.Tumbo kujaa na kuiwa gumuE.KuharishaF.Kukosa choo

 

2.Gesi tumboni.Sababu nyingine ni kujaa gesi tumboni. Gesi tumboni inaweza kusababishwa na:-A.Kumeza hewa sanaB.Kula kupitilizaC.Kuvuta sigaraD.Kutafuna bigjiiE.Chakula kutokumeng’enywa vyemaF.Kula vyakula vyenye gesiG.Kuwa na bakteria kwenye utumbo mkubwa.

 

3.Kuvimbiwa ama chakula kutokumeng’enywa vyema tumboni. Hali hii huplekea maumivu ya tumbo kwa juu. Maumivu haya wakati mwingine husambaa na kuathiri chini ya tumbo upande wa kushoto. Mtu pia ataona dalili kama:-A.KiunguliaB.Kuhisi kishiba na tumbo kujaaC.Kucheua gesiD.kichefuchefu

 

4.Ngiri henia; henia ina dalili kama:-A.Kuongezeka uvimbe maeneo ya tumboni (si kila henia)B.Maumivu kuongezekaC.Maumivu wakati unaponyanyua kituD.Kujihisi umeshiba5. kuwa na vijiwe kwenye figoVijiwe vya kwenye vigo vinatokana na mkusanyiko wa madini ya chumvi. Vijiwe hivi vinaweza kutokea kwenye figo, kibofu ama maeneo mengine kwenye mfumo wa mkojo. Vijijiwe hvi vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Pia vinaweza kusababisha maumivu ya mgongo upande mmoja na nyuma pia na kwenye mbavu. Tofauti na dalili hizi pia mgonjwa anaweza kupata dalili zifuatazo:-

 

A.Mkojo wenye rangi ya kahawiya, nyekundu ama mawingu mawingu na haruu kaliB.Mkojo wenye maumivu makali unaotokea mra kwa maraC.KichefuchefuD.VomitingE.Homa

 

Maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kulia kwa wanawake, husababishwa na yafuatayo:-A.Tumbo la changoB.Kuota tishu za tumbo la uzazi maeneo mengineC.Kuwa na shida kwenye ovariD.Kuwa na ujauzito uliotungia njeE.Kuwa na ugonjwa wa PID

 

?

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 5641

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 web hosting     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 ai web app     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Fangasi wa kwenye uke.

Fangasi hawa kitaalamu wanafahamika kama vagina yeast infection na majina mengine ya kitaalamu ni kama vagina candidiasis, u vulvovaginal candidiasis au candidal vaginitis.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo (Peptic ulcers)

Vidonda vya tumbo ni vidonda vilivyo wazi vinavyotokea kwenye utando wa ndani wa umio, tumbo na sehemu ya juu ya utumbo wako. Dalili ya kawaida ya Peptic ulcer ni maumivu ya tumbo. Vidonda vya tumbo ni pamoja na: Vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani

Soma Zaidi...
Yajuwe maradhi mbalmbali ya ini na chanzo chake

Ini ni moja ya ogani za mwili ambazo husumbuliwa na maradhi hatari sana. Katika post hii utakwend akuyajuwa maradh hatari ambayo hushambulia ini. Pia utajifunza jinsi a kujikinga na maradhi hayo.

Soma Zaidi...
FAIDA ZA KIAFYA ZA MINYOO: kupunguza aleji, kuchochea utungaji wa mimba, kupona kwa vidonda vya ndani

FAIDA ZA KIAFYA ZA MINYOO Wakati mwingine kuwa na aina flani ya minyoo kunaweza kuwa na faida katika afya.

Soma Zaidi...
Walio kwenye hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa,

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea kwa maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kutokea kwa maumivu ya jino

Soma Zaidi...