image

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo


DALILI ZA UKIMWI NA HIV KWENYE ULIMU NA MDOMO


HIV hivi ni virusi vilivyopata umaarufu sana kwa kufahamika kuwa ndio virusi pekee vinavyoweza kusababisha upungufu wa kinga mwilini yaani UKIMWI. Virusi hivi anaweza kuvipata binadamu yeyote yule. Zipo njia nyingi ambazo unaweza kupata virusi hivi kama kushiriki ngono zembe, kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kijifungua, kushiriki vitu vyenye ncha kali, kupewa damu yenye virusi, na njia nyingine kibao. Dalili za HIV na UKIMWI zinatofautiana kulingana na hatua ya mgonjwa. Lanini kuna wakati Ulimi na Mdomo kuweza kuonyesha dalili hizi wazi wazi.


Dalili za HIV na UKIMWI kupitia mdomoni zinaweza kuwa ni dalili za mwanzoni sana za UKIMWI kwa baadhi ya watu. Ukweli ni kuwa dalili hizi zinaweza kumpata yeyote lakini kuna watu wapo hatarini zaidi kama watoto wachanga, wazee na watu wenye upungufu wa kinga yaani UKIMWI. Dalili hizi tutaziona moja hadi nyingine hapo chini.


Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi
1.Kukauka kwa mdomo na kuoza kwa meno.
Virusi vya HIV vinaweza kupelekea mdomo kukauka na kukosa mate ya kutosha. Hivyo miongoni mwa kazi za mate ni kulinda meno na mdomo. Hivyo kupelekea meno kuoza. Ni vyema mgonjwa kama anatatizo hili kuonana na daktari aweze kumpa ushauri. Unaweza kutumia dawa maalumu kwa ajili ya kuchochea mate ama kutafuna bigji ambazo hazina sukari.


2.Kupata fangasi wa kwenye mdomo wajulikanao kama candidiasis (thrush).
Fangasi hawa wanaweza kusababisha madoa mekundu kwenye ulimi, ama mdoa meupe kwenye mdomo. Pia wanaweza kusababisha kupasuka kwa kona za mdomo na kutengeneza weupe kwenye kona za mdomo. Pia mdomoni kunaweza kuta buda la nyama lisilokuwa na maumivu. Fangasi hawa wanaweza kuhamia kwenye koo na kusababisha maumivu. Fangasi hawa ni rahisi sana kuondoka baada ya matibabu ila kwa baadhi ya sababu wanaweza kuwa sugu.


3.Vidonda kwenye mdomo na ulimi
Hivi ni vijidonda vijidogo ambavyo vipo duara. Vinaweza kutokea kwenye ulimi na kwenye mashavu kwa ndani. Pia vinaweza kutokea nyuma ya koo. Vidonda hivi vinakuwa na rangi nyekunu pembeni na rangi ya kijivu katikati. Misongo ya mawzo na baadhi ya vyakula vinaweza kuwa ni sababu.


4.Vidonda vya homa.
Kama umeshawahi kushuhudia vidonda ambavyo vinatokana na homa. Vidonda hivi kwa watu wenye UKIMWI vina tabia ya kujirudia mara kwa mara. Dawa za ART huweza kusaidia hali hii kutotokea.


5.Maradhi ya ufinzi ama periodontitis or gingivitis
Haya ni maradhi ya ufizi ambapo ufinzi unakosa nguvu na kushindwa kuzuia meno vyema. Hal hii inaweza kupelekea kung’oka kwa meno. Hali hii inaweza tokea mapema sana miezi 18 baada ya kupata HIV. Ukavu kwenye mdomo, kuvuta sigara kunaweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi.


6.Kuota kwa kambakamba ama vinywele vinywele kwenye ulimi na pembeni ya ulimi.
Kitaalamu hivi hujulikana kama Hairy Leukoplakia. Vikambakamba ama vinyweleo nyweleo hivi havina maumivu lakini pia haviwezi kutoka hata kwa kupiga mswaki. Hii inaweza kuwa ni katika dalili za mwanzo zaidi za UKIMWI. Vyenyewe vipo na rangi nyeupe


7.Madoa ya rangi ya dhambarau iliyowiva ama nyekundu kwenye mafinzi, sehemu ya juu ya mdomo na nyuma ya ulimi. Kitaalamu hufahamika kama Kaposi’s Sarcoma (KS Hii inaweza kuwa ni dalili ya kwanza kwa mtu ambaye hajapima HIV. Na kwa ambaye ameshaanza kutumia dawa dalili hizi ni si rahisi kujionyesha.


8.Kuota chunjua kwenye mdomo,na ulimi. Hizi husababishwa na virusi vinavyojulikana kama Human Papillomavirus, HPV. Kikawaida chunjua inaweza kuota popote pale kwenye mwili hasa hasa hutokea mara nyingi kwenye mikono. Watu wenye HIV chunjia hizi huweza kuvamia ulimi na kuhama maeneo mengine kwenye mdomo. Pia baadhi ya virusi wanao;eta hali hii wanaweza kusababisha saratani.


Mwisho nikufahamishe tu kuwa mdomo ni katika sehemu za kwanza kuonyesha dalili za HIV na UKIMWI. Ni vyema kwenda kupima endapo utagundua una moja ya dalili hizo hapo juu.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 4990


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo
Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula. Soma Zaidi...

Kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI Soma Zaidi...

Magonjwa yanayowashambulia watoto wachanga
Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk, Soma Zaidi...

Typhoid husabisha mwili kuchoka na maumivu ya kichwa pamoja na joint za miguu kuchoka
Dalili za typhid zinapasa kuangaliwa kwa umakini. Bila vipimo mtu asitumie dawa za tyohod, kwanu dalili za tyohid hufanana na daliki za maradhi mengi. Soma Zaidi...

Upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo.
Post hii inahusu zaidi upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo dalili zake na namna ya kumsaidia mgonjwa mwenye tatizo hilo. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUGUNDUA VIDONDA VYA TUMBO
NAMNA YA KUGUNDUA VIDONDA VYA TUMBO Ili kugundua vidonda, daktari wako anaweza kwanza kuchukua historia ya matibabu na kufanya uchunguzi wa mwili. Soma Zaidi...

Dalili za mtu aliyekula chakula chenye sumu
Post hii inahusu zaidi mtu aliyekula chakula chenye sumu, chakula chenye sumu ni chakula ambacho kikitumiwa na mtu yeyote kinaweza kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu hata kifo. Soma Zaidi...

Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa. Soma Zaidi...

Maambukizi ya magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu athari za maambukizi ya magonjwa ya ngono  ambapo magonjwa ya ngono isipokuwa UKIMWI  yanatibika .mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitali au kituo chochote cha afya kupata matibabu mara anapoona dalili za magonjwa haya. Soma Zaidi...

NJIA ZA KUKABILIANA NA PRESHA YA KUSHUKA
1. Soma Zaidi...

Tatizo la mapafu kuwa na usaha.
Post hii inahusu Zaidi tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni tatizo ambalo usababishwa na bakteria ambao uingia kwenye mapafu na kusababisha madhara na hatimaye mapafu kuwa na usaha . Soma Zaidi...

Mie ni mwanamke ninamaumivu chini ya kitovu upande wa kushoto, na nikishika tumbo nahisi kitu kigumu upande huo huo wa kushoto... hii itakua ni nini?
Je unasumbuliwa na maumivuvya tumbo chini ya kitovu upande wa kushito. Post hii itakuletea sababu za maukivubhayo na nini ufanye. Soma Zaidi...