Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo


DALILI ZA UKIMWI NA HIV KWENYE ULIMU NA MDOMO


HIV hivi ni virusi vilivyopata umaarufu sana kwa kufahamika kuwa ndio virusi pekee vinavyoweza kusababisha upungufu wa kinga mwilini yaani UKIMWI. Virusi hivi anaweza kuvipata binadamu yeyote yule. Zipo njia nyingi ambazo unaweza kupata virusi hivi kama kushiriki ngono zembe, kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kijifungua, kushiriki vitu vyenye ncha kali, kupewa damu yenye virusi, na njia nyingine kibao. Dalili za HIV na UKIMWI zinatofautiana kulingana na hatua ya mgonjwa. Lanini kuna wakati Ulimi na Mdomo kuweza kuonyesha dalili hizi wazi wazi.


Dalili za HIV na UKIMWI kupitia mdomoni zinaweza kuwa ni dalili za mwanzoni sana za UKIMWI kwa baadhi ya watu. Ukweli ni kuwa dalili hizi zinaweza kumpata yeyote lakini kuna watu wapo hatarini zaidi kama watoto wachanga, wazee na watu wenye upungufu wa kinga yaani UKIMWI. Dalili hizi tutaziona moja hadi nyingine hapo chini.


Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi
1.Kukauka kwa mdomo na kuoza kwa meno.
Virusi vya HIV vinaweza kupelekea mdomo kukauka na kukosa mate ya kutosha. Hivyo miongoni mwa kazi za mate ni kulinda meno na mdomo. Hivyo kupelekea meno kuoza. Ni vyema mgonjwa kama anatatizo hili kuonana na daktari aweze kumpa ushauri. Unaweza kutumia dawa maalumu kwa ajili ya kuchochea mate ama kutafuna bigji ambazo hazina sukari.


2.Kupata fangasi wa kwenye mdomo wajulikanao kama candidiasis (thrush).
Fangasi hawa wanaweza kusababisha madoa mekundu kwenye ulimi, ama mdoa meupe kwenye mdomo. Pia wanaweza kusababisha kupasuka kwa kona za mdomo na kutengeneza weupe kwenye kona za mdomo. Pia mdomoni kunaweza kuta buda la nyama lisilokuwa na maumivu. Fangasi hawa wanaweza kuhamia kwenye koo na kusababisha maumivu. Fangasi hawa ni rahisi sana kuondoka baada ya matibabu ila kwa baadhi ya sababu wanaweza kuwa sugu.


3.Vidonda kwenye mdomo na ulimi
Hivi ni vijidonda vijidogo ambavyo vipo duara. Vinaweza kutokea kwenye ulimi na kwenye mashavu kwa ndani. Pia vinaweza kutokea nyuma ya koo. Vidonda hivi vinakuwa na rangi nyekunu pembeni na rangi ya kijivu katikati. Misongo ya mawzo na baadhi ya vyakula vinaweza kuwa ni sababu.


4.Vidonda vya homa.
Kama umeshawahi kushuhudia vidonda ambavyo vinatokana na homa. Vidonda hivi kwa watu wenye UKIMWI vina tabia ya kujirudia mara kwa mara. Dawa za ART huweza kusaidia hali hii kutotokea.


5.Maradhi ya ufinzi ama periodontitis or gingivitis
Haya ni maradhi ya ufizi ambapo ufinzi unakosa nguvu na kushindwa kuzuia meno vyema. Hal hii inaweza kupelekea kung’oka kwa meno. Hali hii inaweza tokea mapema sana miezi 18 baada ya kupata HIV. Ukavu kwenye mdomo, kuvuta sigara kunaweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi.


6.Kuota kwa kambakamba ama vinywele vinywele kwenye ulimi na pembeni ya ulimi.
Kitaalamu hivi hujulikana kama Hairy Leukoplakia. Vikambakamba ama vinyweleo nyweleo hivi havina maumivu lakini pia haviwezi kutoka hata kwa kupiga mswaki. Hii inaweza kuwa ni katika dalili za mwanzo zaidi za UKIMWI. Vyenyewe vipo na rangi nyeupe


7.Madoa ya rangi ya dhambarau iliyowiva ama nyekundu kwenye mafinzi, sehemu ya juu ya mdomo na nyuma ya ulimi. Kitaalamu hufahamika kama Kaposi’s Sarcoma (KS Hii inaweza kuwa ni dalili ya kwanza kwa mtu ambaye hajapima HIV. Na kwa ambaye ameshaanza kutumia dawa dalili hizi ni si rahisi kujionyesha.


8.Kuota chunjua kwenye mdomo,na ulimi. Hizi husababishwa na virusi vinavyojulikana kama Human Papillomavirus, HPV. Kikawaida chunjua inaweza kuota popote pale kwenye mwili hasa hasa hutokea mara nyingi kwenye mikono. Watu wenye HIV chunjia hizi huweza kuvamia ulimi na kuhama maeneo mengine kwenye mdomo. Pia baadhi ya virusi wanao;eta hali hii wanaweza kusababisha saratani.


Mwisho nikufahamishe tu kuwa mdomo ni katika sehemu za kwanza kuonyesha dalili za HIV na UKIMWI. Ni vyema kwenda kupima endapo utagundua una moja ya dalili hizo hapo juu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 14378

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Dalili za malaria

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya dalili za maralia

Soma Zaidi...
DALILI ZA MIMBA BAADA YA TENDO LA NDOA

Je unahitaji kujuwa kama umepata ujauzito baada ya kufanya tendo la ndoa? hakika sio rahisi ila kama utakuwa makini utaweza.

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, hizi ni njia ambazo zinapaswa kufuatwa ili kutokomeza kabisa maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya tishu (leukemia)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na saratani za tishu ambazo kitaalamu hujulikana Kama Leukemia kawaida huhusisha seli nyeupe za damu. Seli zako nyeupe za damu ni wapiganaji hodari wa maambukizo - kwa kawaida hukua na kugawanyika kwa utaratibu, kadri mwi

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa bakteria unaoambukizwa na kupe.

Ugonjwa wa bakteria unaoambukizwa na kupe ambao husababisha dalili kama za mafua. Dalili na ishara za Ugonjwa huu ni kati ya kuumwa na mwili kidogo hadi homa kali na kwa kawaida huonekana ndani ya wiki moja au mbili baada ya kuumwa na kupe. Njia bora ya

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za Ugonjwa wa akili.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa akili .

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

Soma Zaidi...
Uvimbe wa mishipa midogo ya Damu kwenye ngozi

Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wenye uchungu wa mishipa midogo ya damu kwenye ngozi yako ambayo hutokea kutokana na ongezeko la joto la ghafla kutokana na halijoto ya baridi. Pia inajulikana kama pernio, chilblain inaweza kusababisha kuwasha,

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata UTI

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi uken

Posti hii inahusu zaidi dalili za fangasi uken, hizi ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la fangasi uken.

Soma Zaidi...