Dalili za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za vidonda vya tumbo

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO

 

 

Vidonda vya tumbo huweza kutokea ndani ya tumbo kutokana na mashambulizi ya bakteria aina ya H.pylori, ama kutokana na athari za madawa flani ama mashambulizi ya wadudu wengineo ama kwa sababu ya ugonjwa wa saratani. Makala hii inakwenda kukuletea dalili duu za vidonda vya tumbo.

 

1.Maumivu ya tumbo; hii pengine ndio katika dalili kuu zaidi ambazo wengi wenye vidonda vya tumo wanaipata. Maumivu haya yanawza kuwa makali sana wakati mgonjwa akiwa na njaa.Tumbo hili ni tofauti na tumbo la ngiri ama chango. Maumivu haya yanaweza kuanzia chini ya kitomvu na kupanda juu hadi kifuani. Maumivu haya yanaweza kufuatana na dalili zifuatazo hapo chini.

 

2.Tumbo kujaa; tumbo linaweza kujaa gesi hata akashindwa kula vyema. Huenda mgonjwa akajihisi ameshiba badala ya kuka kidogo. Uhalisia si kwamba ameshiba ila tumbo ndio limejawa na gesi.

 

3.Kukosa hamu ya kula; hii ni katika dalili ya hatari sana, maana umuhimu wa chakula unafahamika vyema. Mgonjwa anaumwa na tumbo na anakosa kabisa hamu ya kula pia anahisi tumbo kujaa.

 

4.Kupata kiungulia cha mara kwa mara. Kiungulia unaweza kukitibu kwa kutumia dawa, kwani hazina tabu kwa vidonda vya tumbo. Pia unaweza kulamba majivu, hii ni tiba mbadala ambayo inatumka kutibu kiungulia. Lakini epuka kula vyakula vyenye gesi.

 

5.Kupungua uzito; vidonda vya tumbo vinaweza kusababisha mtu kupungua uzito, bila ya kujuwa sababu maalumu. Inaweza kuwa ni kutokana na kutokula kwake kwa sababu ya kukosa hamu ya kula.

 

6.Kichefuchefu na kutapika. mgonjwa wa vidonda vya tumbo wakati mwingine anapata kichefuchefu kisicho na sababu maalumu. Hali hii inaweza kumpelekea akatapika ama asitapike. Na wakati mwingine anaweza kuona dmau kwenye matapishi yake.

 

7.Mapadiliko kwenye kinyesi. Mgonjwa anaweza kuona mabadiliko kwenye rangi ya kinyesi chake. Kinaweza kuwa cheusi sana na chenye harufu mbaya sana. Na wakati mwingine kinaweza kuwa na damu.

 

 

Masharti kwa mwenye vidonda vya tumbo.

 

 

Makala hii inakwenda kukuletea masharti yanayompasa mwenye vidonda vya tumbo ayafate. Je ni vyakula gani vinafaha sana kwa mwenye vidonda vya tumbo?

Masharti ya vidonda vya tumbo

1.Punguza ama wacha kabisa unywaji wa pombe

 

2.Punguza misongo ya mawazo

 

3.Epuka vyakula vyenye gesi kama baadhi ya aina za maharagwe

 

4.Hakikisha unakula kwa wakati.

 

5.Epuka kukaa na njaa kwa muda mrefu

 

6.Epuka matumizi ya madawa ya aspirin na jamii za madawa hayo. Kama ni lazima utumie madawa mbalimbali na ya mchanganyiko hasa yale ya kuzuia maumivu, basi kwanza zungumza na daktari akupe maelekezo.

 

7.Punguza ama wacha kabisa uvutaji wa sigara

 

8.Hata kama hutakuwa na hamu ya kula jilazimishe ule ama tumia dawa za kuongeza hamu ya kula.

 

9.Epuka vyakula vyenye mafuta kwa wingi.

 

10.Kunywa maji mengi ya ya kutosha kila siku

 

11.Onana na daktari mara kwa mara unapohisi mabadiliko ya hatari mwilini mwako.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2467

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Njia za kuondokana na fangasi

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.

Soma Zaidi...
Dalili za vidonda vya tumbo, matibabu na dawa zake, sababu za kutokea kwake

Utajifunza chanzo cha vidonda vya tumbo, dalili zake, dawa na matibabu yake pamoja na njia za kujilinda na vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Madhara ya maambukizi kwenye tumbo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa

Soma Zaidi...
Mzio (aleji) na Dalili zake

Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Sababu za Kuvimba kwa kope.

Post hii inazungumzia kuhusiana na Sababu zinazopelekea kuvimba kwa kope, kawaida huhusisha sehemu ya kope ambapo kope hukua na kuathiri kope zote mbili. Pia hutokea wakati tezi ndogo za mafuta ziko karibu na msingi wa kope huziba. Hii inasababisha kuw

Soma Zaidi...
Ni nini husababisha kuziba kwa Njia ya machozi

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa kuziba kwa Njia ya machozi yaani kukosa machozi ambayo husababishwa na maambukizi.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

Soma Zaidi...
ninaisi kma kunakitu kwenye koo alafu kuna ali ya weupe kwenye ulimi na Mashavu kwa ndan

Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya.

Soma Zaidi...
Dalili za selulitis.

Selulitis ni maambukizi ya ngozi ya bakteria ya kawaida, ambayo yanaweza kuwa mbaya. Cellulitis inaonekana kama sehemu nyekundu ya ngozi iliyovimba na inahisi joto na laini. Inaweza kuenea kwa kasi kwa sehemu nyingine za mwili. Cellulitis haienei kuto

Soma Zaidi...