Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za vidonda vya tumbo
DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo huweza kutokea ndani ya tumbo kutokana na mashambulizi ya bakteria aina ya H.pylori, ama kutokana na athari za madawa flani ama mashambulizi ya wadudu wengineo ama kwa sababu ya ugonjwa wa saratani. Makala hii inakwenda kukuletea dalili duu za vidonda vya tumbo.
1.Maumivu ya tumbo; hii pengine ndio katika dalili kuu zaidi ambazo wengi wenye vidonda vya tumo wanaipata. Maumivu haya yanawza kuwa makali sana wakati mgonjwa akiwa na njaa.Tumbo hili ni tofauti na tumbo la ngiri ama chango. Maumivu haya yanaweza kuanzia chini ya kitomvu na kupanda juu hadi kifuani. Maumivu haya yanaweza kufuatana na dalili zifuatazo hapo chini.
2.Tumbo kujaa; tumbo linaweza kujaa gesi hata akashindwa kula vyema. Huenda mgonjwa akajihisi ameshiba badala ya kuka kidogo. Uhalisia si kwamba ameshiba ila tumbo ndio limejawa na gesi.
3.Kukosa hamu ya kula; hii ni katika dalili ya hatari sana, maana umuhimu wa chakula unafahamika vyema. Mgonjwa anaumwa na tumbo na anakosa kabisa hamu ya kula pia anahisi tumbo kujaa.
4.Kupata kiungulia cha mara kwa mara. Kiungulia unaweza kukitibu kwa kutumia dawa, kwani hazina tabu kwa vidonda vya tumbo. Pia unaweza kulamba majivu, hii ni tiba mbadala ambayo inatumka kutibu kiungulia. Lakini epuka kula vyakula vyenye gesi.
5.Kupungua uzito; vidonda vya tumbo vinaweza kusababisha mtu kupungua uzito, bila ya kujuwa sababu maalumu. Inaweza kuwa ni kutokana na kutokula kwake kwa sababu ya kukosa hamu ya kula.
6.Kichefuchefu na kutapika. mgonjwa wa vidonda vya tumbo wakati mwingine anapata kichefuchefu kisicho na sababu maalumu. Hali hii inaweza kumpelekea akatapika ama asitapike. Na wakati mwingine anaweza kuona dmau kwenye matapishi yake.
7.Mapadiliko kwenye kinyesi. Mgonjwa anaweza kuona mabadiliko kwenye rangi ya kinyesi chake. Kinaweza kuwa cheusi sana na chenye harufu mbaya sana. Na wakati mwingine kinaweza kuwa na damu.
Masharti kwa mwenye vidonda vya tumbo.
Makala hii inakwenda kukuletea masharti yanayompasa mwenye vidonda vya tumbo ayafate. Je ni vyakula gani vinafaha sana kwa mwenye vidonda vya tumbo?
Masharti ya vidonda vya tumbo
1.Punguza ama wacha kabisa unywaji wa pombe
2.Punguza misongo ya mawazo
3.Epuka vyakula vyenye gesi kama baadhi ya aina za maharagwe
4.Hakikisha unakula kwa wakati.
5.Epuka kukaa na njaa kwa muda mrefu
6.Epuka matumizi ya madawa ya aspirin na jamii za madawa hayo. Kama ni lazima utumie madawa mbalimbali na ya mchanganyiko hasa yale ya kuzuia maumivu, basi kwanza zungumza na daktari akupe maelekezo.
7.Punguza ama wacha kabisa uvutaji wa sigara
8.Hata kama hutakuwa na hamu ya kula jilazimishe ule ama tumia dawa za kuongeza hamu ya kula.
9.Epuka vyakula vyenye mafuta kwa wingi.
10.Kunywa maji mengi ya ya kutosha kila siku
11.Onana na daktari mara kwa mara unapohisi mabadiliko ya hatari mwilini mwako.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa
Soma Zaidi...MATIBABU YA VIDONDA VYA TUMBO Matibabu ya vidonda vya tumbo inategemea sababu.
Soma Zaidi...Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya.
Soma Zaidi...Kuharibika kwa mimba ni upotevu wa hiari wa ujauzito kabla ya wiki ya 20. Takriban asilimia 10 hadi 20 ya mimba zinazojulikana huisha kwa kuharibika kwa mimba. Lakini idadi halisi labda ni kubwa zaidi kwa sababu mimba nyingi hutokea mapema sana katika u
Soma Zaidi...Huu ni ugonjwa wa fangasi wanaosababishwa na mashambulizi ya fangani aia ya yeast waitwao candida.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanawake
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za kupunguza maumivu na kazi zake, ni dawa ambazo upunguza maumivu kwenye mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...NAMNA YA KUISHI NA VIDONDA VYA TUMBO Unaweza kupata nafuu kutoka kwa maumivu ya kidonda cha tumbo ikiwa utafata taratibu za kiafya kama:- 1.
Soma Zaidi...