picha

Dalili za minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo

DALILI ZA MINYOO

Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo  wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-

 

Kichefuchefu

Kukosa hamu ya kula

Maumivu ya tumbo

Kupungua uzito

Uchovu wa viungo

Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi

Kuona minyoo kwenye kinyesi.

Kuona damu kwenye kinyesi

Tumbo kujaa

 

 

Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-

 

 

 

minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:

Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo

Kuwa na alegi

Kuwa na homa

Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa

 

 

minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-

Kuwashwa

Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini

Kuwa na uchovu wa hali ya juu.

 

 

minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-

Kupata homa

Kuvimba kwa uso

Maumivu ya misuli na kuchoka

Maumivu ya kichwa

Kutokupenda kupigwa na mwanga

Matatizo katika macho (conjuctivist)

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3546

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 web hosting     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ugonjwa huu uaribu zaidi kwenye mifupa na sehemu nyingine ambazo zinakaribia kwenye mifupa

Soma Zaidi...
Dalili za uvumilivu wa pombe

Uvumilivu wa pombe unaweza kusababisha athari za haraka, zisizofurahi baada ya kunywa pombe. Ishara na dalili za kawaida za kutovumilia kwa pombe ni pua iliyojaa na Kuvuta ngozi. Uvumilivu wa pombe husababishwa na hali ya maumbile ambayo mwili hauwezi k

Soma Zaidi...
Magonjwa yanayowashambulia watoto wachanga

Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk,

Soma Zaidi...
dalili za ukimwi huchukua muda gani?

Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya maradhi haya ya ukimwi, dalili zake, tiba na kinga zake na mengineyo zaidi.

Soma Zaidi...
Matatizo ya kisaikolojia kwa watoto (mfano, ADHD): Dalili zake.

Afya ya akili ya watoto ni msingi wa maendeleo yao ya baadaye. Katika ulimwengu wa sasa, matatizo ya kisaikolojia kama ADHD (Upungufu wa Umakini na Usikivu) yanazidi kuongezeka, lakini mara nyingi huchanganyikiwa na utovu wa nidhamu. Makala haya yanalenga kutoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu dalili za matatizo ya kisaikolojia kwa watoto, yakigusia kwa kina hali ya ADHD na jinsi wazazi wanavyoweza kutofautisha kati ya tabia za kawaida za utotoni na changamoto zinazohitaji msaada wa kisaikolojia.

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi kwenye ovari

Posti hii inahusu zaidi dalili za maambukizi kwenye ovari, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye ovari na kusababisha matatizo makubwa kama mgonjwa haujatibiwa mapema.

Soma Zaidi...