Dalili za minyoo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo
DALILI ZA MINYOO
Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-
Kichefuchefu
Kukosa hamu ya kula
Maumivu ya tumbo
Kupungua uzito
Uchovu wa viungo
Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi
Kuona minyoo kwenye kinyesi.
Kuona damu kwenye kinyesi
Tumbo kujaa
Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-
minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:
Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo
Kuwa na alegi
Kuwa na homa
Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa
minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-
Kuwashwa
Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini
Kuwa na uchovu wa hali ya juu.
minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-
Kupata homa
Kuvimba kwa uso
Maumivu ya misuli na kuchoka
Maumivu ya kichwa
Kutokupenda kupigwa na mwanga
Matatizo katika macho (conjuctivist)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π2 Kitau cha Fiqh π3 Simulizi za Hadithi Audio π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Bongolite - Game zone - Play free game π6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Dalili za Homa ya uti wa mgongo (meningitis)
Posti hii inahusu zaidi dalili za Homa ya uti wa mgongo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye maambukizi kwenye uti wa mgongo.
Soma Zaidi...Dalili za ovulation kwa mwanamke
βOvulation (kipindi cha upevu wa yai) ni hatua muhimu zaidi katika mzunguko wa hedhi wa mwanamke, hasa kwa wale wanaopanga kupata ujauzito au wanaotaka kuepuka mimba kwa njia za asili. Makala haya yanachambua dalili kuu zinazoonyesha mwili upo kwenye hatua hii, jinsi ya kuzitambua, na kuweka sawa baadhi ya dhana potofu kupitia ukweli wa kisayansi (Fact Check).
Soma Zaidi...Sababu za mdomo kuwa mchungu
Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu.
Soma Zaidi...Je, kuna vyakula vya kuepuka wakati wa ujauzito?
Lishe bora ni msingi wa ukuaji wa mtoto mwenye afya na ustawi wa mama mjamzito. Hata hivyo, kuna baadhi ya vyakula ambavyo vinaweza kuwa na vimelea hatari, sumu, au kemikali zinazoweza kusababisha madhara makubwa kama vile maambukizi ya bakteria, kuharibika kwa mimba, au matatizo ya ukuaji wa mtoto. Makala hii inaorodhesha vyakula unavyopaswa kuepuka ili kulinda afya yako na ya kiumbe ulichobeba.
Soma Zaidi...Dalili za minyoo ya tumbo
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za minyoo ya tumbo ambapo minyoo hawa husababishwa na mtu kula vyakula vichafu ambavyo havijaiva vizuri au maji machafu pia au bacteria.
Soma Zaidi...je..! naweza kuambukizwa fangasi kwa kujamiiana na mtu mwenye fangasi?
Je ukifanya mapenz na mtu mweny aina hi ya fangasi na akawa anayo maambukizi ya ukimwi.
Soma Zaidi...