Dalili za minyoo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo
DALILI ZA MINYOO
Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-
Kichefuchefu
Kukosa hamu ya kula
Maumivu ya tumbo
Kupungua uzito
Uchovu wa viungo
Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi
Kuona minyoo kwenye kinyesi.
Kuona damu kwenye kinyesi
Tumbo kujaa
Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-
minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:
Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo
Kuwa na alegi
Kuwa na homa
Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa
minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-
Kuwashwa
Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini
Kuwa na uchovu wa hali ya juu.
minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-
Kupata homa
Kuvimba kwa uso
Maumivu ya misuli na kuchoka
Maumivu ya kichwa
Kutokupenda kupigwa na mwanga
Matatizo katika macho (conjuctivist)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
je maambukizi ya virus vya ukimwi yataonekana kwenye kupimo baada ya siku ngap??
Ni muda gani nitaanza kuona dalili za HIV na kilimo kitaonyesha kuwa nimeathirika?
Soma Zaidi...Madhara ya minyoo
Posti hii inaonyesha kiufupi kabisa madhara ya minyoo kwenye mwili wa binadamu. Yafuatayo Ni madhara ya minyoo;
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa hepatitis A
Hepatitis A ni ugonjwa wa kuambukiza wa ini unaosababishwa na virusi vya Hepatitis A. Virusi ni mojawapo ya aina kadhaa za virusi vya Hepatitis vinavyosababisha kuvimba na kuathiri uwezo wa ini wako kufanya kazi.
Soma Zaidi...Fangasi watambulikao kama invasive candidiasis
Hawa huweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenda maeneo mengine nyeti sana ya mwili.
Soma Zaidi...