Dalili za minyoo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo
DALILI ZA MINYOO
Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-
Kichefuchefu
Kukosa hamu ya kula
Maumivu ya tumbo
Kupungua uzito
Uchovu wa viungo
Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi
Kuona minyoo kwenye kinyesi.
Kuona damu kwenye kinyesi
Tumbo kujaa
Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-
minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:
Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo
Kuwa na alegi
Kuwa na homa
Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa
minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-
Kuwashwa
Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini
Kuwa na uchovu wa hali ya juu.
minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-
Kupata homa
Kuvimba kwa uso
Maumivu ya misuli na kuchoka
Maumivu ya kichwa
Kutokupenda kupigwa na mwanga
Matatizo katika macho (conjuctivist)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili za saratani (cancer)
Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.
Soma Zaidi...Dalili za UKIMWI kwa Mtu Aliyeambukizwa Karibuni
Makala hii inaelezea hatua ya awali ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU), inayojulikana kama hatua ya maambukizi makali (acute HIV infection). Inafafanua dalili za kawaida zinazoweza kujitokeza wiki chache baada ya mtu kupata maambukizi, umuhimu wa kupima mapema, na kuondoa dhana potofu kuhusu dalili hizi.
Soma Zaidi...Namna ya kujikinga na VVU/UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza namna mbalimbali za kujikinga na VVU/UKIMWI
Soma Zaidi...ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.
Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.
Soma Zaidi...Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Soma Zaidi...