Dalili za minyoo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo
DALILI ZA MINYOO
Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-
Kichefuchefu
Kukosa hamu ya kula
Maumivu ya tumbo
Kupungua uzito
Uchovu wa viungo
Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi
Kuona minyoo kwenye kinyesi.
Kuona damu kwenye kinyesi
Tumbo kujaa
Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-
minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:
Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo
Kuwa na alegi
Kuwa na homa
Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa
minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-
Kuwashwa
Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini
Kuwa na uchovu wa hali ya juu.
minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-
Kupata homa
Kuvimba kwa uso
Maumivu ya misuli na kuchoka
Maumivu ya kichwa
Kutokupenda kupigwa na mwanga
Matatizo katika macho (conjuctivist)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 web hosting π3 kitabu cha Simulizi π4 Bongolite - Game zone - Play free game π5 ai web app π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Sababu za Kuchoka Sana Mwilini
βUchovu wa mwili (fatigue) ni hisia ya kukosa nguvu, kutaka kulala mara kwa mara, na kuhisi mwili ni mzito, hali ambayo haiishi hata baada ya kupata mapumziko. Ingawa mara nyingi ni matokeo ya mtindo wa maisha, wakati mwingine inaweza kuwa ishara ya tatizo la kiafya linalohitaji uangalizi. Makala hii inaangazia sababu kuu za uchovu huu na hatua za kurejesha nguvu zako.
Soma Zaidi...Bawasili usababishwa na nini?
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.
Soma Zaidi...Homa ya matone (Mumps): Dalili na tiba yake.
Homa ya matone, inayojulikana kama Mumps, ni maambukizi ya virusi yanayoathiri tezi zinazozalisha mate (salivary glands), hasa tezi zilizopo pande zote mbili za shavu (tezi za parotidi). Ugonjwa huu huambukiza kwa urahisi kupitia matone ya maji yanayotoka unapopiga chafya, kukohoa, au kuzungumza. Ingawa kwa sasa ni nadra kutokana na chanjo, bado inaweza kuwapata watu ambao hawajapata chanjo hiyo. Makala haya yanakupa uelewa wa dalili zake na jinsi ya kutoa huduma ya kwanza.
Soma Zaidi...Matatizo ya kisaikolojia yanayosababishwa na matumizi ya mtandao.
βGundua athari za kisaikolojia zinazotokana na matumizi ya mtandao, ikiwemo wasiwasi, msongo wa mawazo, na uraibu. Pata maarifa ya kitaalamu ya jinsi ya kulinda afya yako ya akili katika ulimwengu wa kidijitali.
Soma Zaidi...UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA
Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles.
Soma Zaidi...