Dalili za minyoo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo
DALILI ZA MINYOO
Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-
Kichefuchefu
Kukosa hamu ya kula
Maumivu ya tumbo
Kupungua uzito
Uchovu wa viungo
Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi
Kuona minyoo kwenye kinyesi.
Kuona damu kwenye kinyesi
Tumbo kujaa
Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-
minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:
Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo
Kuwa na alegi
Kuwa na homa
Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa
minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-
Kuwashwa
Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini
Kuwa na uchovu wa hali ya juu.
minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-
Kupata homa
Kuvimba kwa uso
Maumivu ya misuli na kuchoka
Maumivu ya kichwa
Kutokupenda kupigwa na mwanga
Matatizo katika macho (conjuctivist)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Jifunze kuhusu ugonjwa wa bawasiri na dalili zake
Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu ugonjwa wa Bawasiri na dalili zake. Pia utajifunza njia za kujilinda nao.
Soma Zaidi...Sababu zinazopelekea maumivu ya Matiti.
 Maumivu ya matiti hutokea zaidi kwa watu ambao hawajamaliza hedhi, ingawa yanaweza kutokea baada ya kukoma hedhi.Â
Soma Zaidi...Sababu za maumivu wakati wa kujamiiana
Maumivu wakati wa kujamiiana (kitaalamu dyspareunia) ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi, ingawa mara nyingi halizungumzwi wazi kutokana na unyanyapaa au aibu. Maumivu haya yanaweza kusababishwa na sababu za kisaikolojia, matatizo ya kimwili, au mabadiliko ya kihomoni. Makala haya yanachambua vyanzo vikuu vya maumivu hayo na kutoa ukweli wa kisayansi (Fact Check) ili kukusaidia kujua hatua za kuchukua.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa coma
Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la Kichwa, Kiharusi, Uvimbe kwenye ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi,
Soma Zaidi...Dalili za uchovu wa joto mwilini.
Uchovu wa joto ni hali ambayo dalili zake zinaweza kujumuisha kutokwa na jasho kubwa na mapigo ya haraka, ambayo ni matokeo ya joto la mwili wako. Ni mojawapo ya magonjwa matatu yanayohusiana na joto, huku tumbo la joto likiwa kali zaidi na Kihar
Soma Zaidi...MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k
Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.
Soma Zaidi...