Post hii unahusu mtu mwenye ugonjwa wa akili ambao huitwa ugonjwa wa wasiwasi Kwa kitaalamu huitwa anxiety,ni pale mtu anapokuwa na wasiwasi Kwa vitu nafasi mbali mbali kama tutakavoona.
Dalili za mtu mwenye wasiwasi Kwa kitaalamu huitwa anxiety ni kama zifuatazo
1.kuwepo Kwa mawazo mda wote
Mtu mwenye wasiwasi anaweza kuwa na mawazo yanayozunguka kichwani mwake mara kwa mara, bila uwezo wa kuyaacha mara nyingi mawazo hayo yanaweza kusababisha huzuni na kushindwa kula au kufanya mambo mengine ya muhimu Kwa hiyo uendeleee kuwaza hata kuwaza mambo ambayo hayapo.
2.kuwepo Kwa hofu za mara Kwa mara
; inaweza kuwa na uhusiano na matukio ya kila siku au matukio yaliyopita au Kwa sababu ya kuwaza mambo ambayo hayapo na yaliyo makubwa ambayo humjengea hofu na mara nyingi mgonjwa huanza kuogopa watu na vitu vidogo hasa ambavyo havina maaana Kwa mfano unaweza kukuta mtu mzima anamwogopa mtoto wadudu na vitu vidogo vya aina hiyo.
.3.Moyo Kufanya Kazi kwa Kasi:
Mtu anaweza kuhisi mapigo ya moyo kuwa ya haraka au kuwa na mtikisiko wa mwili, hali hii inawezekana kabisa kusababishwa na pointi ya juu yake Kwa sababu mtu anapokuwa na hofu na kuogopa kila kitu pamoja na wasiwasi na mwili Kwa ujumla unareact ambapo mapigo ya moyo yanaenda mbio Kwa sababu ya woga na wasiwasi wa mgonjwa.
.4.Kukosa usingizi.
Wasiwasi unaweza kusababisha mtu kuwa na ugumu wa kuingia au kubaki katika usingizi,Kwa sababu ya kuwaza vitu ambavyo havipo pamoja na wasiwasi kusababisha mtu kukosa Usingizi Kwa sababu uwepo wa usingizi utegemea na Amani ,Kwa hiyo mtu anapoendelea kuwaza mambo ambayo hayapo hasa makubwa anashutuka kutoka Usingizini,Kwa mfano mtu anawaza kwamba Kuna watu wanakuja kumuua hawezi kulala Kwa sababu anaona anakuja kuuliwa na pengine anaweza kukimbia bila sababu,ndio maana unaweza kumwona mwehu anakimbia pasipokuwepo na sababu yoyote ya kukimbia.
.5.kutokuwa na Hamasa
Mtu mwenye wasiwasi anaweza kukosa hamasa ya kufanya mambo aliyokuwa akiyapenda mara nyingi,Kwa sababu haoni umuhimu wa kufanya jambo hilo na pia Huwa na wasiwasi kama kitu anachokifanya ni Cha ukweli au amekosea unaweza kukuta mtu anatengeneza kitu anakiharibu au pengine anakuja kutengeneza anasema Kuna watu watakuja kuharibu hali ya kuwaza na kutojiamini, kuwaza na kutowaamini wengine kusababisha mgonjwa wa aina hii kutokuwa na hamasa ya kufanya kitu chochote.Au pengine akitaka kufanya kitu mpaka anawaza matokeo hasi.
6.Kutokuwepo na umakini katika utendaji
Wasiwasi unaweza kufanya mtu awe mgumu wa kuzingatia vitu hivyo kushindwa kufikia malengo,Kwa sababu Kila anachokifanya anakifanya akiwa na wasiwasi na kutojiamini hali ambayo kusababisha kutokuwepo na umakini katika utendaji.
Mabadiliko katika Hamu ya Chakula
Watu wenye wasiwasi wanaweza kula zaidi au kupunguza kula kulingana na hali Kwa sababu yeye anawaza labda atakufa,anawaza labda anayoyafanya hayaeleweki Kwa watu,Hana Amani Kwa hiyo hata na wakati wa kula hali vizuri kitu ambacho kupelekea kupungua uzito na Kukonda Kwa sababu ya kutokuwepo hamu ya chakula.
Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi tunapaswa kutambua kwamba huu ni ugonjwa Kwa hiyo tuwatendee kama ndugu zetu na Kwa upande,Kuna watu wengine wanakoswa msaada jamii inawatenga hali ambayo kusababisha wenyewe kujitenga na jamii hatimaye wengine wanaamua maamuzi magumu na kujiua.kwa hiyo jamii inaapaswa kuonyesha ushirikiano na kuwapeleka kwenye vituo vya afya Kwa sababu huu ni ugonjwa na una chanzo chake pia unatibika.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
posti hii inahusu dalili za Homa ya Manjano ni maambukizi ya virusi yanayoenezwa na aina fulani ya mbu. Maambukizi hayo ni ya kawaida zaidi na kuathiri wasafiri na wakazi wa maeneo hayo.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia zaidi kuhusiana na Homa ya ini yenye sumu ni kuvimba kwa ini lako kutokana na kuguswa na vitu fulani ambavyo umeathiriwa navyo. Homa ya ini yenye sumu inaweza kusababishwa na pombe, kemikali, madawa ya kulevya au virutubisho vya lis
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa
Soma Zaidi...Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kiafya yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex. Kwa binadamu sababu ya kawaida ni Mycobacterium tuberculosis.
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha mambo mbalimbali yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi msaada kwa aliye na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni huduma maalumu ambayo utolewa kwa mtu ambaye ana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo. Zifuatazo ni huduma maalumu kwa mwenye uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa sumu mwilini, kwa sababu kuna wakati mwingine tunapata magonjwa na matatizo mbalimbali ya ki afya tunaangaika huku na huko kumbe sababu kubwa ni kuwepo kwa sumu mwilini na vyanzo vya sumu hiyo ni kama ifuatavy
Soma Zaidi...