Dalili za mtu mwenye wasiwasi (anxiety)

Post hii unahusu mtu mwenye ugonjwa wa akili ambao huitwa ugonjwa wa wasiwasi Kwa kitaalamu huitwa anxiety,ni pale mtu anapokuwa na wasiwasi Kwa vitu nafasi mbali mbali kama tutakavoona.

Dalili za mtu mwenye wasiwasi Kwa kitaalamu huitwa anxiety ni kama zifuatazo

 1.kuwepo Kwa mawazo mda wote

 Mtu mwenye wasiwasi anaweza kuwa na mawazo yanayozunguka kichwani mwake mara kwa mara, bila uwezo wa kuyaacha mara nyingi mawazo hayo yanaweza kusababisha huzuni na kushindwa kula au kufanya mambo mengine ya muhimu Kwa hiyo uendeleee kuwaza hata kuwaza mambo ambayo hayapo.

2.kuwepo Kwa hofu za mara Kwa mara

; inaweza kuwa na uhusiano na matukio ya kila siku au matukio yaliyopita au Kwa sababu ya kuwaza mambo ambayo hayapo na yaliyo makubwa ambayo humjengea hofu na mara nyingi mgonjwa huanza kuogopa watu na vitu vidogo hasa ambavyo havina maaana Kwa mfano unaweza kukuta mtu mzima anamwogopa mtoto wadudu na vitu vidogo vya aina hiyo.

.3.Moyo Kufanya Kazi kwa Kasi:

Mtu anaweza kuhisi mapigo ya moyo kuwa ya haraka au kuwa na mtikisiko wa mwili, hali hii inawezekana kabisa kusababishwa na pointi ya juu yake Kwa sababu mtu anapokuwa na hofu na kuogopa kila kitu pamoja na wasiwasi na mwili Kwa ujumla unareact ambapo mapigo ya moyo yanaenda mbio Kwa sababu ya woga na wasiwasi wa mgonjwa.

.4.Kukosa usingizi.

Wasiwasi unaweza kusababisha mtu kuwa na ugumu wa kuingia au kubaki katika usingizi,Kwa sababu ya kuwaza vitu ambavyo havipo pamoja na wasiwasi kusababisha mtu kukosa Usingizi Kwa sababu uwepo wa usingizi utegemea na Amani ,Kwa hiyo mtu anapoendelea kuwaza mambo ambayo hayapo hasa makubwa anashutuka kutoka Usingizini,Kwa mfano mtu anawaza kwamba Kuna watu wanakuja kumuua hawezi kulala Kwa sababu anaona anakuja kuuliwa na pengine anaweza kukimbia bila sababu,ndio maana unaweza kumwona mwehu anakimbia pasipokuwepo na sababu yoyote ya kukimbia.

.5.kutokuwa na Hamasa

Mtu mwenye wasiwasi anaweza kukosa hamasa ya kufanya mambo aliyokuwa akiyapenda mara nyingi,Kwa sababu haoni umuhimu wa kufanya jambo hilo na pia Huwa na wasiwasi kama kitu anachokifanya ni Cha ukweli au amekosea unaweza kukuta mtu anatengeneza kitu anakiharibu au pengine anakuja kutengeneza anasema Kuna watu watakuja kuharibu hali ya kuwaza na kutojiamini, kuwaza na kutowaamini wengine kusababisha mgonjwa wa aina hii kutokuwa na hamasa ya kufanya kitu chochote.Au pengine akitaka kufanya kitu mpaka anawaza matokeo hasi.

6.Kutokuwepo na umakini katika utendaji

Wasiwasi unaweza kufanya mtu awe mgumu wa kuzingatia vitu hivyo kushindwa kufikia malengo,Kwa sababu Kila anachokifanya anakifanya akiwa na wasiwasi na kutojiamini hali ambayo kusababisha kutokuwepo na umakini katika utendaji.

Mabadiliko katika Hamu ya Chakula

 Watu wenye wasiwasi wanaweza kula zaidi au kupunguza kula kulingana na hali Kwa sababu yeye anawaza labda atakufa,anawaza labda anayoyafanya hayaeleweki Kwa watu,Hana Amani Kwa hiyo hata na wakati wa kula hali vizuri kitu ambacho kupelekea kupungua uzito na Kukonda Kwa sababu ya kutokuwepo hamu ya chakula.

Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi tunapaswa kutambua kwamba huu ni ugonjwa Kwa hiyo tuwatendee kama ndugu zetu na Kwa upande,Kuna watu wengine wanakoswa msaada jamii inawatenga hali ambayo kusababisha wenyewe kujitenga na jamii hatimaye wengine wanaamua maamuzi magumu na kujiua.kwa hiyo jamii inaapaswa kuonyesha ushirikiano na kuwapeleka kwenye vituo vya afya Kwa sababu huu ni ugonjwa na una chanzo chake pia unatibika.

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Salvatory image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 217

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu

Post hii inahusu Zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake

Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate na namna ya kutibu tatizo la kujaa kwa mate mdomoni

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.

Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.

Soma Zaidi...
Mambo yanayosababisha kiuno au mgongo kuwa na maumivu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kusababishwa mgongo wAko au kiuno kwa na maumivu, Mgongo ukiwa na maumivu makali Sana yanaweza kusababishwa shida kubwa ata utakapokaa au ukilala au ukitumia bado maumivu yanakuwepo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal.

Soma Zaidi...
Maradhi ya Ini na dalili zake, na vipi utajikinga nayo

MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu.

Soma Zaidi...
Dalili za moyo kutanuka

Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo zinaweza kujitokeza na kuonyesha kwamba moyo umetanuka.

Soma Zaidi...
nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kup

Soma Zaidi...
Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,

Soma Zaidi...
Mambo ambayo yanaweza kuongeza hatari ya Ugonjwa wa Homa ya ini yenye sumu.

Posti hii inazungumzia zaidi kuhusiana na Homa ya ini yenye sumu ni kuvimba kwa ini lako kutokana na kuguswa na vitu fulani ambavyo umeathiriwa navyo. Homa ya ini yenye sumu inaweza kusababishwa na pombe, kemikali, madawa ya kulevya au virutubisho vya lis

Soma Zaidi...