HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO
HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO Unaweza kupunguza hatari yako ya vidonda vya tumbo ikiwa unafuata mikakati sawa inayopendekezwa kama tiba ya nyumbani kutibu vidonda.
HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO
Unaweza kupunguza hatari yako ya vidonda vya tumbo ikiwa unafuata mikakati sawa inayopendekezwa kama tiba ya nyumbani kutibu vidonda. Inaweza pia kusaidia:
Jilinde dhidi ya maambukizo. Haijulikani wazi jinsi bakteria aina ya H. pylori inavyoenea, lakini kuna ushahidi fulani kwamba inaweza kupitishwa kutoka kwa mtu hadi mtu au kupitia chakula na maji.
Unaweza kuchukua hatua za kujikinga na maambukizo, kama vile H. pylori, kwa kuosha mikono yako mara kwa mara kwa sabuni na maji na kwa kula vyakula ambavyo vimepikwa kabisa.
Chukua tahadhari dhidi ya dawa za kupunguza maumivu. Ikiwa unatumia kila wakati dawa za kupunguza maumivu ambazo zinaongeza hatari ya vidonda vya tumbo, chukua hatua za kupunguza hatari hiyo. Kwa mfano, kunywa dawa yako pamoja na chakula.
Zungumza na daktari kupata dawa ambayo itakupa utulivu wa maumivu bila ya kusababisha hatari zaidi.
Epuka au punguza kunywa pombe wakati unatumia dawa. Kama tulivyoona unywaji wa pombe unaweza kuhatarisha zaidi vidonda vya tumbo kwa kuchochea uzalishwaji wa asidi tumboni.
Ikiwa unahitaji dawa za kutuli za maumivu na zile za NSAID, unaweza kuhitaji pia kuchukua dawa za ziada kama vile antacid, PPI, blocker acid au cytoprotective agents. Kikundi cha NSAIDs kinachoitwa COX-2 inhibitors kinaweza kuwa na nafasi ndogo ya kusababisha vidonda vya tumbo, lakini vinaweza kuongeza hatari ya mshtuko wa moyo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 web hosting 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Visababishi vya maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya maambukizi kwenye milija na, ni mambo yanayosababisha maambukizi kwenye milija na ovari.
Soma Zaidi...Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,
Soma Zaidi...Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo
Soma Zaidi...Dalili na Ishara za mawe kwenye figo
Mawe kwenye figo yana sababu nyingi na yanaweza kuathiri sehemu yoyote ya njia yako ya mkojo kutoka kwa figo hadi kibofu chako.
Soma Zaidi...vidonda vya tumbo, dalili zake, chanzo chake na tiba yake
Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya vidonda vya tumbo, nini hasa chanzo chake, vipi vinatokea ni zipi dalili zake, ni zipi njia za kujilinda dhidi ya vidonda vya tumbo. Pia tutaangalia matibabu ya kutibi vidonda vya tumbo.
Soma Zaidi...