HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO
HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO Unaweza kupunguza hatari yako ya vidonda vya tumbo ikiwa unafuata mikakati sawa inayopendekezwa kama tiba ya nyumbani kutibu vidonda.
HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO
Unaweza kupunguza hatari yako ya vidonda vya tumbo ikiwa unafuata mikakati sawa inayopendekezwa kama tiba ya nyumbani kutibu vidonda. Inaweza pia kusaidia:
Jilinde dhidi ya maambukizo. Haijulikani wazi jinsi bakteria aina ya H. pylori inavyoenea, lakini kuna ushahidi fulani kwamba inaweza kupitishwa kutoka kwa mtu hadi mtu au kupitia chakula na maji.
Unaweza kuchukua hatua za kujikinga na maambukizo, kama vile H. pylori, kwa kuosha mikono yako mara kwa mara kwa sabuni na maji na kwa kula vyakula ambavyo vimepikwa kabisa.
Chukua tahadhari dhidi ya dawa za kupunguza maumivu. Ikiwa unatumia kila wakati dawa za kupunguza maumivu ambazo zinaongeza hatari ya vidonda vya tumbo, chukua hatua za kupunguza hatari hiyo. Kwa mfano, kunywa dawa yako pamoja na chakula.
Zungumza na daktari kupata dawa ambayo itakupa utulivu wa maumivu bila ya kusababisha hatari zaidi.
Epuka au punguza kunywa pombe wakati unatumia dawa. Kama tulivyoona unywaji wa pombe unaweza kuhatarisha zaidi vidonda vya tumbo kwa kuchochea uzalishwaji wa asidi tumboni.
Ikiwa unahitaji dawa za kutuli za maumivu na zile za NSAID, unaweza kuhitaji pia kuchukua dawa za ziada kama vile antacid, PPI, blocker acid au cytoprotective agents. Kikundi cha NSAIDs kinachoitwa COX-2 inhibitors kinaweza kuwa na nafasi ndogo ya kusababisha vidonda vya tumbo, lakini vinaweza kuongeza hatari ya mshtuko wa moyo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 kitabu cha Simulizi π4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π5 Bongolite - Game zone - Play free game π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Dalili za ugonjwa wa UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ugonjwa wa UTI
Soma Zaidi...Sababu kuu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, Tumbo la ngiri na chango
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, na tumbo la ngiri kwa wanaume, na tumbo la chango kwa wanawake
Soma Zaidi...Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani
Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.
Soma Zaidi...Sababu za Uvimbe wa tishu za Matiti kwa wavulana au wanaume
posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wa tishu za matiti kwa wavulana au wanaume, unaosababishwa na kutofautiana kwa homoni za estrojeni na testosterone. Pia unaweza kuathiri matiti moja au zote mbili, wakati mwingine bila usawa. Watoto wachanga,
Soma Zaidi...Je unaweza sex na mwanamke mwenye HIV na ukaenda kupima wiki moja na ukagundurika kwa vipimo vya maabara
Utakapofanya ngono na aliyeathirika haimaanishi na wewe kuwa lazima utakuwa umeathirika. Kuathirika kuna mambo mengi lazima yafanyike.
Soma Zaidi...Dalili za Kisukari Zinazoonekana Mapema
βUgonjwa wa kisukari (Diabetes) ni moja ya magonjwa hatari ya kimfumo yanayokua kwa kasi duniani, lakini habari njema ni kwamba unaweza kudhibitiwa ikiwa utagundulika mapema. Makala haya yanajadili ishara na dalili za awali kabisa ambazo mwili hutoa wakati viwango vya sukari kwenye damu vinapoanza kupanda. Pia, yanabainisha tofauti ya dalili hizi na mabadiliko ya kawaida ya mwili, na kuwasilisha ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu zilizozoeleka mitaani.
Soma Zaidi...