Dalili za ugonjwa wa kaswende
Post hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kaswende kwa wajawazito, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa watu wote, kwa sababu ugonjwa huu una dalili ambazo upitia kwa hatua mbalimbali kama tutakavyoona.
Dalili za ugonjwa wa kaswende.
1. Kwa kuwa tangu mwanzoni nimejaribu kueleza kwamba ugonjwa huu upitia kwenye hatua mbalimbali,kwa hiyo tutaanza na hatua ya kwanza ambayo kwa kitaalamu huitwa primary symptoms, kwenye hatua hii mgonjwa anakuwa na vipele ambazo havina maumivu kwa kitaalamu huitwa chancres hivi vidonda hivyo ujitokeza baada ya wiki tatu baada ya maambukizi, hivi vidonda mara nyingi utokea sehemu ambayo sex imefanyiwa kama ni mdomoni vitajitokeza hapo kama ni kwa njia ya haja kubwa vitajitokeza hapo au kama ni kwa njia ya kawaida na penyewe vitajitokeza hapo, kwa hiyo vidonda hivyo kama havijapata matibabu utoweka ndani ya wiki tatu mpaka sita.
2. Kwa hiyo kama ikitokea mtu akapatwa na tatizo kama hili na anajua kabisa alifanya ngono bila kinga ni vizuri kabisa kupata matibabu mapema ili kuondoa tatizo kubwa kubwa zaidi, changamoto ni kwamba vidonda hivi mara nyingi huwa haviumi ndio maana watu wengi hawajishughulishi kupima badala yake ni kupotezea na ukizingatia havina maumivu yoyote, madhara ya kutotibu mapema usababisha hali ambayo sio nzuri kama tutakavyoona hapo baadaye.
3. Hatua ya pili utokea pale ambapo vidonda vya hatua ya kwaza kutotibiwa , hatua hiyo kwa kitaalamu huitwa primary symptoms,hivi vidonda ambavyo vilikuwepo vinatudi tena sio kwenye sehemu ambayo sex ilifanyika tu bali ni katika sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye mikono hasa hasa kwenye sehemu ya viganja, kwenye miguu hasa kwenye ukanyagio,pia na rangi yake inakuwa kama ya nyekundu ila sio nyekundu iliyokaza, na pia vidonda hivi vinaweza kuwa hata mdomoni, hali hiyo utokea kwa sababu ya ugonjwa kueneza kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
4. Katika hatua hii mgonjwa anaweza kushindwa kutembea kwa sababu ya kuwepo kwa vidonda kwenye nyayo za miguu na wakati mwingine hatua hii uambatana na homa, mwili mzima kuchoka,Madonda kwenye koo, kuvimba kwa lymph nodes kwa sababu ya maambukizi, pengine nywele kwenye kichwa unyonyoka , maumivu makali ya kichwa, kupungua uzito, na pia mwili kuishiwa nguvu.
Pengine watu uchanganya dalili hizi na mgonjwa wa HIV kwa sababu dalili za mgonjwa wa HIV hatua ya nne na tatu huwa na dalili kama hizi, mtu kuja kufikia hatua hiyo ni kwamba ugonjwa huu unakuwa umemaliza miaka kama kumi na tano mwilini na ndipo dalili za hapo juu zinaweza kutokea.
5 . Kwa hiyo jamii inapaswa kuelezwa wazi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu kuna wakati watu wanaenda kupima baada ya kuona dalili kama hizi wakidhani ni maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, na baadae unakuta mtua anapewa majbu kwamba hana maambukizi ya ukimwi na ni kweli anakuwa hana ila shida watu wengi hawapimi kaswende na yenyewe kama haijatibiwa inaweza kumfikisha mtu sehemu mbaya , kwa hiyo kupima kaswende ni lazima ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali.
6. Pia hatua ya mwisho ni hatua ya tatu ambayo kwa kitaalamu huitwa latent phase, ni hatua ya mwisho utokea mara nyingi kama hatua ya pili haijatibiwa na kama matibabu hayajafikiwa mgonjwa anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo kupima kaswende ni lazima ili kuweza kuepukana na vifo vya akina mama na watoto wao, twende hospitali dawa ipo na watu wengi wanapona.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Simulizi za Hadithi Audio π2 Dua za Mitume na Manabii π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Kitau cha Fiqh π5 ai web app π6 web hosting
Post zinazofanana:
Vyakula Vinavyosaidia Afya ya Uzazi kwa Mwanamke
βAfya ya uzazi kwa mwanamke inategemea sana usawa wa homoni, ubora wa mayai, na mazingira salama ya mfuko wa uzazi. Lishe bora ni nguzo kuu katika kuboresha maeneo haya. Makala haya yanachambua vyakula muhimu vinavyoweza kuongeza uwezo wa kushika mimba, kusawazisha homoni, na kulinda mfumo wa uzazi kwa ujumla, yakisindikizwa na ukweli wa kisayansi
Soma Zaidi...Nini husababisha Fangasi sehemu za Siri
Katika somo hili tutaeleza sababu kuu zinazopelekea kupata fangasi sehemu za siri, mazingira yanayochochea kuongezeka kwa fangasi, pamoja na vitu vinavyochangia maambukizi na kurudia-rudia kwa tatizo.
Soma Zaidi...Tofauti ya Dalili za UKIMWI na Magonjwa Mengine
βWatu wengi huishi kwa hofu wakihisi dalili za kawaida za magonjwa ni ishara ya VVU/UKIMWI. Posti hii inafafanua kwa nini dalili za VVU si maalum (non-specific) na kwa nini kipimo cha maabara ndiyo njia pekee sahihi ya kujua hali ya afya yako.
Soma Zaidi...Vyakula vya kuepuka kama una shinikizo la damu.
Shinikizo la damu (hypertension) ni hali ambayo mara nyingi haionyeshi dalili za wazi, lakini ikipuuzwa, inaweza kusababisha madhara makubwa kama vile kiharusi, magonjwa ya moyo, na figo. Mkakati mkuu wa kudhibiti shinikizo la damu hauhusishi dawa pekee, bali ni mabadiliko ya mfumo wa maisha, hususan lishe. Makala haya yanachambua vyakula vinavyopaswa kuepukwa ili kusaidia kupunguza shinikizo na kuimarisha afya ya mfumo wa mzunguko wa damu.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu
Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa.
Soma Zaidi...Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Soma Zaidi...