Dalili za ugonjwa wa kaswende

Post hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kaswende kwa wajawazito, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa watu wote, kwa sababu ugonjwa huu una dalili ambazo upitia kwa hatua mbalimbali kama tutakavyoona.

Dalili za ugonjwa wa kaswende.

1. Kwa kuwa tangu mwanzoni nimejaribu kueleza kwamba ugonjwa huu upitia kwenye hatua mbalimbali,kwa hiyo tutaanza na hatua ya kwanza ambayo kwa kitaalamu huitwa primary symptoms, kwenye hatua hii mgonjwa anakuwa na vipele ambazo havina maumivu kwa kitaalamu huitwa chancres hivi vidonda hivyo ujitokeza baada ya wiki tatu baada ya maambukizi, hivi vidonda mara nyingi utokea sehemu ambayo sex imefanyiwa kama ni mdomoni vitajitokeza hapo kama ni kwa njia ya haja kubwa vitajitokeza hapo au kama ni kwa njia ya kawaida na penyewe vitajitokeza hapo, kwa hiyo vidonda hivyo kama havijapata matibabu utoweka ndani ya wiki tatu mpaka sita.

 

2. Kwa hiyo kama ikitokea mtu akapatwa na tatizo kama hili na anajua kabisa alifanya ngono bila kinga ni vizuri kabisa kupata matibabu mapema ili kuondoa tatizo kubwa kubwa zaidi, changamoto ni kwamba vidonda hivi mara nyingi huwa haviumi ndio maana watu wengi hawajishughulishi kupima badala yake ni kupotezea na ukizingatia havina maumivu yoyote, madhara ya kutotibu mapema usababisha hali ambayo sio nzuri kama tutakavyoona hapo baadaye.

 

3. Hatua ya pili utokea pale ambapo vidonda vya hatua ya kwaza kutotibiwa , hatua hiyo kwa kitaalamu huitwa primary symptoms,hivi vidonda ambavyo vilikuwepo vinatudi tena sio kwenye sehemu ambayo sex ilifanyika tu  bali ni katika sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye mikono hasa hasa kwenye sehemu ya viganja, kwenye miguu hasa kwenye ukanyagio,pia na rangi yake inakuwa kama ya nyekundu ila sio nyekundu iliyokaza, na pia vidonda hivi vinaweza kuwa hata mdomoni, hali hiyo utokea kwa sababu ya ugonjwa kueneza kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

 

4. Katika hatua hii mgonjwa anaweza kushindwa kutembea kwa sababu ya kuwepo kwa vidonda kwenye nyayo za miguu na wakati mwingine hatua hii uambatana na homa, mwili mzima kuchoka,Madonda kwenye koo, kuvimba kwa lymph nodes kwa sababu ya maambukizi, pengine nywele kwenye kichwa unyonyoka , maumivu makali ya kichwa, kupungua uzito, na pia mwili kuishiwa nguvu. 

 

Pengine watu uchanganya dalili hizi na mgonjwa wa HIV kwa sababu dalili za mgonjwa wa HIV hatua ya nne na tatu huwa na dalili kama hizi, mtu kuja kufikia hatua hiyo ni kwamba ugonjwa huu unakuwa umemaliza miaka kama kumi na tano mwilini na ndipo dalili za hapo juu zinaweza kutokea.

 

5 . Kwa hiyo jamii inapaswa kuelezwa wazi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu kuna wakati watu wanaenda kupima baada ya kuona dalili kama hizi wakidhani ni maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, na baadae unakuta mtua anapewa majbu kwamba hana maambukizi ya ukimwi na ni kweli anakuwa hana ila shida watu wengi hawapimi kaswende na yenyewe kama haijatibiwa inaweza kumfikisha mtu sehemu mbaya , kwa hiyo kupima kaswende ni lazima ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali.

 

6. Pia hatua ya mwisho ni hatua ya tatu ambayo kwa kitaalamu huitwa latent phase, ni hatua ya mwisho utokea mara nyingi kama hatua ya pili haijatibiwa na kama matibabu hayajafikiwa mgonjwa anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo kupima kaswende ni lazima ili kuweza kuepukana na vifo vya akina mama na watoto wao, twende hospitali dawa ipo na watu wengi wanapona.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1958

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Heti kama mtu kafany mapenzi na mtu mwe ukimwi siku hihiyo akenda hospitali kapewa dawa kweli hataweza kuwabukizwa

Swali hili limeulizwa na mdau mmoja. Kuwa endapo mtu atafanya ngono zembe na akapata virusi je ataweza kuambukiza.

Soma Zaidi...
VIRUSI VYA KORONA AU CORONA (CORONAVIRUS)

Virusi vya korona ni katika aina za virusi ambavyo asili yake ni kutoka kwa wanyama na kuja kwa binadamu.

Soma Zaidi...
dalili za mwanzo za ukimwi kwa mwanamke

Katika makala hii utakwenda kuzijuwa baadhi ya dalili za ukimwi ama HIV kwa mwanamke

Soma Zaidi...
Maradhi ya Ini na dalili zake, na vipi utajikinga nayo

MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu.

Soma Zaidi...
KISUKARI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi uken

Posti hii inahusu zaidi dalili za fangasi uken, hizi ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la fangasi uken.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jipu la Jino

Jipu la jino ni mfuko wa usaha unaosababishwa na maambukizi ya bakteria.

Soma Zaidi...
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.

Soma Zaidi...
Matatizo yanayoweza kusababisha Saratani.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na matatizo yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa Saratani.

Soma Zaidi...