Dalili za ugonjwa wa kaswende


image


Post hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kaswende kwa wajawazito, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa watu wote, kwa sababu ugonjwa huu una dalili ambazo upitia kwa hatua mbalimbali kama tutakavyoona.


Dalili za ugonjwa wa kaswende.

1. Kwa kuwa tangu mwanzoni nimejaribu kueleza kwamba ugonjwa huu upitia kwenye hatua mbalimbali,kwa hiyo tutaanza na hatua ya kwanza ambayo kwa kitaalamu huitwa primary symptoms, kwenye hatua hii mgonjwa anakuwa na vipele ambazo havina maumivu kwa kitaalamu huitwa chancres hivi vidonda hivyo ujitokeza baada ya wiki tatu baada ya maambukizi, hivi vidonda mara nyingi utokea sehemu ambayo sex imefanyiwa kama ni mdomoni vitajitokeza hapo kama ni kwa njia ya haja kubwa vitajitokeza hapo au kama ni kwa njia ya kawaida na penyewe vitajitokeza hapo, kwa hiyo vidonda hivyo kama havijapata matibabu utoweka ndani ya wiki tatu mpaka sita.

 

2. Kwa hiyo kama ikitokea mtu akapatwa na tatizo kama hili na anajua kabisa alifanya ngono bila kinga ni vizuri kabisa kupata matibabu mapema ili kuondoa tatizo kubwa kubwa zaidi, changamoto ni kwamba vidonda hivi mara nyingi huwa haviumi ndio maana watu wengi hawajishughulishi kupima badala yake ni kupotezea na ukizingatia havina maumivu yoyote, madhara ya kutotibu mapema usababisha hali ambayo sio nzuri kama tutakavyoona hapo baadaye.

 

3. Hatua ya pili utokea pale ambapo vidonda vya hatua ya kwaza kutotibiwa , hatua hiyo kwa kitaalamu huitwa primary symptoms,hivi vidonda ambavyo vilikuwepo vinatudi tena sio kwenye sehemu ambayo sex ilifanyika tu  bali ni katika sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye mikono hasa hasa kwenye sehemu ya viganja, kwenye miguu hasa kwenye ukanyagio,pia na rangi yake inakuwa kama ya nyekundu ila sio nyekundu iliyokaza, na pia vidonda hivi vinaweza kuwa hata mdomoni, hali hiyo utokea kwa sababu ya ugonjwa kueneza kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

 

4. Katika hatua hii mgonjwa anaweza kushindwa kutembea kwa sababu ya kuwepo kwa vidonda kwenye nyayo za miguu na wakati mwingine hatua hii uambatana na homa, mwili mzima kuchoka,Madonda kwenye koo, kuvimba kwa lymph nodes kwa sababu ya maambukizi, pengine nywele kwenye kichwa unyonyoka , maumivu makali ya kichwa, kupungua uzito, na pia mwili kuishiwa nguvu. 

 

Pengine watu uchanganya dalili hizi na mgonjwa wa HIV kwa sababu dalili za mgonjwa wa HIV hatua ya nne na tatu huwa na dalili kama hizi, mtu kuja kufikia hatua hiyo ni kwamba ugonjwa huu unakuwa umemaliza miaka kama kumi na tano mwilini na ndipo dalili za hapo juu zinaweza kutokea.

 

5 . Kwa hiyo jamii inapaswa kuelezwa wazi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu kuna wakati watu wanaenda kupima baada ya kuona dalili kama hizi wakidhani ni maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, na baadae unakuta mtua anapewa majbu kwamba hana maambukizi ya ukimwi na ni kweli anakuwa hana ila shida watu wengi hawapimi kaswende na yenyewe kama haijatibiwa inaweza kumfikisha mtu sehemu mbaya , kwa hiyo kupima kaswende ni lazima ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali.

 

6. Pia hatua ya mwisho ni hatua ya tatu ambayo kwa kitaalamu huitwa latent phase, ni hatua ya mwisho utokea mara nyingi kama hatua ya pili haijatibiwa na kama matibabu hayajafikiwa mgonjwa anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo kupima kaswende ni lazima ili kuweza kuepukana na vifo vya akina mama na watoto wao, twende hospitali dawa ipo na watu wengi wanapona.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image NI WATU GANI WALIO HATARINI ZAIDI KUPATA UKIMWI?
Post hii itakwena kukufundisha kuhusu historia fupi ya Ukimwi na matibabu yake. Ni wapi wapo hatarini kupata maambukizi na ni kitu gani wafanye? Soma Zaidi...

image Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa njia mbalimbali kama tutakavyoona hapo baadaye. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu kizunguzungu
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kizungu Zungu ni tatizo ambalo utokea kwa watu mbalimbali na kwa sababu tofauti tofauti na pengine mtu akipata kizungu sehemu mbaya anaweza kusababisha majeraha au pengine kupata ulemavu Soma Zaidi...

image Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili. Soma Zaidi...

image Walio katika hatari ya kupata homa ya inni
Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata homa ya ini,kwa sababu ya hali zao mbalimbali wanaweza kupata ugonjwa huu. Soma Zaidi...

image Maumivu ya tumbo chini ya kifua, upande wa kulia na chini ya kitomvu.
Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo. Soma Zaidi...

image Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizuri na kuwa na afya nzuri. Soma Zaidi...

image Dalili za kasoro ya moyo za kuzaliwa kwa watoto
Ikiwa mtoto wako ana kasoro ya moyo wa kuzaliwa, ina maana kwamba mtoto wako alizaliwa na tatizo katika muundo wa moyo wake. Baadhi ya kasoro za moyo za kuzaliwa kwa watoto ni rahisi na hazihitaji matibabu, kama vile tundu dogo kati ya chemba za moyo ambazo hujifunga yenyewe.Kasoro nyingine za kuzaliwa kwa moyo kwa watoto ni ngumu zaidi na zinaweza kuhitaji upasuaji kadhaa kufanywa kwa muda wa miaka kadhaa. mtoto wako na kasoro ya kuzaliwa ya moyo inaweza kukuacha ukiwa na wasiwasi kuhusu afya ya mtoto wako sasa na wakati ujao.Lakini, kujifunza kuhusu kasoro ya kuzaliwa ya mtoto wako ya moyo kunaweza kukusaidia kuelewa hali hiyo na kujua unachoweza kutarajia katika miezi ijayo na miaka. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa uti wa mgongo, ni ugonjwa unaoshambulia sehemu inayofunika ubongo na pia sehemu ya spinal cord Soma Zaidi...

image Sababu za miguu kufa ganzi.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili. Soma Zaidi...