image

Aina mbalimbali za michubuko

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za michubuko,kwa Sababu michubuko utokea sehemu tofauti tofauti na pia Kuna aina mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Aina mbalimbali za michubuko.

1. Michubuko kwenye ngozi.

Hii ni aina mojawapo ya michubuko ambayo mara nyingi utokea kwenye ngozi ya juu ya mtoto hasa hasa ni kwa sababu ya kuzalisha watoto kwa kutumia vyuma, ambapo michubuko hii utokea kwenye ngozi ya juu ya kichwani , kwa kawaida uweza kugunduliwa na wahudumu wa afya mara tu mtoto akimaliza kuzaliwa, kwa hiyo ikitokea mtoto amevutwa na vyuma ni vizuri kabisa watoa huduma kuwa makini kukagua mtoto kama Kuna sehemu ambayo imeathirika na kuweza kutoa msaada . Pamoja na kazi za wahudumu na wazazi pia wanapaswa kuwa waangalifu katika kuona mabadiliko yoyote kwa mtoto na kutoa taarifa Ili mtoto aweze kuhudumiwa.

 

2. Kwa kawaida michubuko kwenye sehemu za ngozi ya juu ya mtoto mara nyingi haiitaji matibabu zaidi ila kusafishwa na kuiweka sehemu safi na kukausha usaidia sana kupona kwa ngozi hiyo ,vile vile na dawa za kupunguza maambukizi utolewa ambazo dawa hizo kwa kitaamu huiitwa antibiotics. Kwa kawaida mikwaruzo kwenye sehemu ya juu ya ngozi ya kichwa upona mapema na pia wazazi au ndugu hawapaswi kuweka dawa yoyote ambayo ni kinyume na dawa za hospital kwa sababu dawa nyingine uongeza matatizo zaidi kuliko kupona.

 

3. Vile vile aina nyingine ya michubuko kwenye ngozi ni kuvimba kwenye ngozi ya kichwani ambayo Kwa kitaamu huiitwa caput succedaneum,u uvimbe huu utokea kwa watoto hasa pale wanapopambana kutoka kwenye tumbo la mama na kuzaliwa ukutana na obstacles au ukutana na vitu ambavyo umsababishia hali ya kushindwa kutoka vizuri au kutoka kwa shida na kusababisha uvimbe kwenye sehemu ya kichwa , kwa kawaida uvimbe huu uonekana tu baada ya mtoto kuzaliwa na ndani ya siku tatu uvimbe huo uisha taratibu na hatimaye kutoweka kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kuwaelimisha wazazi na ndugu kutoweka vitu vyovyote kwenye uvimbe.

 

4. Michubuko kwenye sehemu za misuli.

Kuna wakati mwingine michubuko utokea kwenye sehemu za misuli au kwa kitaamu kwenye muscle ni kutokana na mishipa kupasuka au kukwaruzwa kwa ngozi hasa za kwenye misuli .kwa kawaida misuli inayoshambuliwa Zaid ni misuli ya kwenye shingo ambayo Kwa kitaamu huiitwa Torticollis muscle, hali hii utokea hasa pale mtoto anapozaliwa hasa kama ametanguliza bega au bega katika kuvutwa misuli ya shingoni inawezekana kulegea na kusababisha michubuko kwenye ngozi, kwa hiyo kama mtoto amezaliwa kwa shida ni vizuri kabisa kuangalia sehemu mbalimbali za misuli Ili kuweza kugundua tatizo lolote ambalo linaweza kujitokeza.

 

5. Mikwaruzo kwenye nevu.

Pia Kuna Kipindi ambapo mikwaruzo utokea kwenye nevu na kwa kiwango kikubwa nevu ambazo zinakuwa affected au zinazoathiriwa ni nevu za kwenye uso na pia na nevu za kwenye mabega, mikono,na kwenye vidole, ndio maana unaweza kumkuta mtoto amelemaa mkono,au bega na pia sehemu yote kuanzia kwenye bega na mikono kwa hiyo kama Kuna Neva yoyote ambayo imeathirika ni kuangalia kwa kutumia utrasound au x- ray kwa Sababu huwezi kuona kuaribika kwa Neva kwa macho ila unaweza kutumia dalili ila kufahamu ni Neva gani imeathirika ni kutumia utrasound au x-ray. Kwa hiyo tutaweza kuona nevu Moja badala ya nyingine kama ifuatavyo.

 

6. Nevu za kwenye uso.

Kuna wakati panakuwepo na kuharibika kwa nevu za kwenye uso kwa kitaamu huiitwa facial nevu.

 Kwa kawaida mtoto kama amezaliwa kwa kuvutwa na vyuma au wakati mwingine kuzaliwa kwa shida kwa sababu mbalimbali ambazo uchangia matatizo ya uzazi, Kuna mda mwingine mtoto uzaliwa akiwa na matatizo kwenye nevu za uso kwa sababu pengine zinakuwa zimevutwa hali ambayo usababisha mtoto kuzaliwa akiwa mdomo wazi, macho yanakuwa yamefunguka na mtoto hawezi kuyafumba, hali ambayo usababisha mtoto kushindwa kunyonya au pengine kabisa anashindwa kumeza, kwa hiyo ukimwona mtoto wa hivyo Kuna dawa ambayo Kwa kitaamu huiitwa methyl cellulose usaidia kurahisisha nevu za usoni na kumfanya mtoto kufumba macho na mdomo na kuanza kunyonya kawaida.

 

7. Mikwaruzo kwenye nevu za kuanzia kwenye bega mpaka kwenye mikono ambazo kwa kitaamu huiitwa branchial plexus.

Ni nevu ambazo pamoja na kuhathiri mabega na mikono vile vile uingiliana na uti wa mgongo katika nevu za mbavu ya nane na pia kuelekea kwenye shingo, ndio maana Kuna watoto wanaozaliwa wakiwa na shingo limelegea na pengine kushindwa kulisimamisha shingo kabisa, kwa hiyo watoto wa namna hiyo hawapaswi kufanyiwa mazoezi kiholela kwa lengo la kufanya shingo zao ziwe vizuri ila badala ya kumsaidia unaweza kuleta matatizo zaidi, kwa hiyo ni vizuri watu wa mifupa ndio wawafanyie mazoezi kwa kitaamu huiitwa watu wa physiotherapy,na wenyewe baada ya kutumia utrasound na x-ray na kuangalia mtiririko wa nevu ndipo waanze kazi mara moja.

 

8. Vile vile Kuna kupalalizi kwenye bega na sehemu ya juu ya mikono na sio kwenye vidole.

Kuna wakati mwingine kwa sababu ya michubuko kwenye mikono hali ambayo usababisha mtoto kupalalizi kwenye bega na pia kwenye mikono ya juu, kwa sababu nevu za sehemu ya juu ziliaribiwa wakati wa kuzaliwa inawezekana kabisa ni kwa sababu ya kutumia vyuma wakati wa kuzaliwa au mtoto kushindwa kutoa au kwa sababu ya mtoto kuvutwa sana na hatimaye kuharibika kwa nevu za mkono na bega, pia hali hii kwa kitaamu huiitwa erb;s palsy, kwa matibabu zaidi ni kuwaona wataalamu wa physiotherapy Ili waweze kumfanyia mtoto mazoezi kulingana na jinsi alivyoumia.

 

9.  Vile vile Kuna mikwaruzo ya kwenye nevu za vidole na sehemu ya chini kabisa ya vidole , ambapo unakuta mtoto Kwa upande wa bega na shingo yupo vizuri kabisa ila kwenye vidole na sehemu ya chini amepalalize na hawezi kufanya chochote au kushika chochote, hali hii utokea kwa sababu ya nevu za chini kwenye mikono zinakuwa zimehadhiriwa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa waangalifu punde mtoto anapozaliwa Ili kuweza kutambua kama Kuna tatizo lolote linalohusiana na kuharibika kwa nevu kwa sababu mtoto asipoangaliwa mapema anaweza kupata madhara zaidi.

 

 10. Kwa hiyo kazi ya kumfanya mtoto aonekane jinsi alivyo ni kazi ya wataalamu wa afya na pia ikiwa taratibu za kuzalisha mtoto ni nzuri na kugundua mapema hali ya hatari kwa mtoto kabla ya kuzaliwa ni vizuri kabisa kwa sababu ufanya matatizo mbalimbali yasitokee matatizo kama vile kupalalizi na kuondoa ulemavu kwa watoto. Na pengine tatizo linaweza kuwepo ila kama mtoto ameandaliwa mapema na kufanyia uchunguzi mapema mtoto anaweza kupona na kuendelea na hali yake ya Kawaida.

 

 

11. Pia kwa sababu ya kutokuwepo kwa elimu ya kutosha kwa jamii, Kuna tabia ya watu kutumia madawa ya mbalimbali au kuwafanyia mazoezi bila mpangilio hali inayowafanya kuleta madhara badala ya kusaidia , kwa hiyo tatizo hili likitokea ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na kuweza kuwapa ushauri unaopaswa Ili kuepuka kuleta madhara zaidi.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1163


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Maambukizi ya H.pylori (Vidonda vya tumbo)
Maambukizi ya H. pylori hutokea wakati aina ya bakteria inayoitwa Helicobacter pylori (H. pylori) inapoambukiza tumbo lako. Hii kawaida hutokea wakati wa utoto. Sababu ya kawaida ya Vidonda vya tumbo, maambukizi ya H. pylori yanaweza kuwa katika za Soma Zaidi...

Namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, hizi ni njia ambazo zinapaswa kufuatwa ili kutokomeza kabisa maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo. Soma Zaidi...

Dalili za kuaribika kwa mishipa ya retina.
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu ambaye ana tatizo kwenye mishipa ya retina,ni tatizo ambalo uwakumba wafu wengi wenye matatizo ya kisukari. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa kisonono, sababu zake nanjia za kujilinda.
Kisonono husababishwa na bakteria. Bakteria ya kisonono mara nyingi hupitishwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine wakati wa kujamiiana, ikiwa ni pamoja na kujamiiana kwa mdomo, mkundu au uke. Soma Zaidi...

Zijue dalili za maambukizi ndani ya sikio na madhara yake
Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu inayotumiwa kwa ajili ya kusikia, Kuna wakati mwingine hushambulia na bakteria na virusi Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Uharibifu wa seli nyekundu za damu
Posti hii inazungumzia kuhusiana na was Uharibifu wa seli nyekundu za damu ambapo hujulikana Kama Ugonjwa wa Hemolytic uremic (HUS) ni hali inayotokana na uharibifu usio wa kawaida wa seli nyekundu za damu mapema. Mara tu mchakato huu unapoanza, seli nye Soma Zaidi...

Njia za kujilinda na kujikinga na UTI
Somo hili linakwenda kukuletea njia za kujilinda na kujikinga na UTI Soma Zaidi...

Sababu za ugonjwa wa mkojo kuwa na damu
Posti hii inaelezea sababu zinazosababisha mkojo kuwa na damu. Soma Zaidi...

MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k
Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende. Soma Zaidi...

AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm
AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa. Soma Zaidi...

Aina ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa. Soma Zaidi...

Fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo Soma Zaidi...