image

Aina mbalimbali za michubuko

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za michubuko,kwa Sababu michubuko utokea sehemu tofauti tofauti na pia Kuna aina mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Aina mbalimbali za michubuko.

1. Michubuko kwenye ngozi.

Hii ni aina mojawapo ya michubuko ambayo mara nyingi utokea kwenye ngozi ya juu ya mtoto hasa hasa ni kwa sababu ya kuzalisha watoto kwa kutumia vyuma, ambapo michubuko hii utokea kwenye ngozi ya juu ya kichwani , kwa kawaida uweza kugunduliwa na wahudumu wa afya mara tu mtoto akimaliza kuzaliwa, kwa hiyo ikitokea mtoto amevutwa na vyuma ni vizuri kabisa watoa huduma kuwa makini kukagua mtoto kama Kuna sehemu ambayo imeathirika na kuweza kutoa msaada . Pamoja na kazi za wahudumu na wazazi pia wanapaswa kuwa waangalifu katika kuona mabadiliko yoyote kwa mtoto na kutoa taarifa Ili mtoto aweze kuhudumiwa.

 

2. Kwa kawaida michubuko kwenye sehemu za ngozi ya juu ya mtoto mara nyingi haiitaji matibabu zaidi ila kusafishwa na kuiweka sehemu safi na kukausha usaidia sana kupona kwa ngozi hiyo ,vile vile na dawa za kupunguza maambukizi utolewa ambazo dawa hizo kwa kitaamu huiitwa antibiotics. Kwa kawaida mikwaruzo kwenye sehemu ya juu ya ngozi ya kichwa upona mapema na pia wazazi au ndugu hawapaswi kuweka dawa yoyote ambayo ni kinyume na dawa za hospital kwa sababu dawa nyingine uongeza matatizo zaidi kuliko kupona.

 

3. Vile vile aina nyingine ya michubuko kwenye ngozi ni kuvimba kwenye ngozi ya kichwani ambayo Kwa kitaamu huiitwa caput succedaneum,u uvimbe huu utokea kwa watoto hasa pale wanapopambana kutoka kwenye tumbo la mama na kuzaliwa ukutana na obstacles au ukutana na vitu ambavyo umsababishia hali ya kushindwa kutoka vizuri au kutoka kwa shida na kusababisha uvimbe kwenye sehemu ya kichwa , kwa kawaida uvimbe huu uonekana tu baada ya mtoto kuzaliwa na ndani ya siku tatu uvimbe huo uisha taratibu na hatimaye kutoweka kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kuwaelimisha wazazi na ndugu kutoweka vitu vyovyote kwenye uvimbe.

 

4. Michubuko kwenye sehemu za misuli.

Kuna wakati mwingine michubuko utokea kwenye sehemu za misuli au kwa kitaamu kwenye muscle ni kutokana na mishipa kupasuka au kukwaruzwa kwa ngozi hasa za kwenye misuli .kwa kawaida misuli inayoshambuliwa Zaid ni misuli ya kwenye shingo ambayo Kwa kitaamu huiitwa Torticollis muscle, hali hii utokea hasa pale mtoto anapozaliwa hasa kama ametanguliza bega au bega katika kuvutwa misuli ya shingoni inawezekana kulegea na kusababisha michubuko kwenye ngozi, kwa hiyo kama mtoto amezaliwa kwa shida ni vizuri kabisa kuangalia sehemu mbalimbali za misuli Ili kuweza kugundua tatizo lolote ambalo linaweza kujitokeza.

 

5. Mikwaruzo kwenye nevu.

Pia Kuna Kipindi ambapo mikwaruzo utokea kwenye nevu na kwa kiwango kikubwa nevu ambazo zinakuwa affected au zinazoathiriwa ni nevu za kwenye uso na pia na nevu za kwenye mabega, mikono,na kwenye vidole, ndio maana unaweza kumkuta mtoto amelemaa mkono,au bega na pia sehemu yote kuanzia kwenye bega na mikono kwa hiyo kama Kuna Neva yoyote ambayo imeathirika ni kuangalia kwa kutumia utrasound au x- ray kwa Sababu huwezi kuona kuaribika kwa Neva kwa macho ila unaweza kutumia dalili ila kufahamu ni Neva gani imeathirika ni kutumia utrasound au x-ray. Kwa hiyo tutaweza kuona nevu Moja badala ya nyingine kama ifuatavyo.

 

6. Nevu za kwenye uso.

Kuna wakati panakuwepo na kuharibika kwa nevu za kwenye uso kwa kitaamu huiitwa facial nevu.

 Kwa kawaida mtoto kama amezaliwa kwa kuvutwa na vyuma au wakati mwingine kuzaliwa kwa shida kwa sababu mbalimbali ambazo uchangia matatizo ya uzazi, Kuna mda mwingine mtoto uzaliwa akiwa na matatizo kwenye nevu za uso kwa sababu pengine zinakuwa zimevutwa hali ambayo usababisha mtoto kuzaliwa akiwa mdomo wazi, macho yanakuwa yamefunguka na mtoto hawezi kuyafumba, hali ambayo usababisha mtoto kushindwa kunyonya au pengine kabisa anashindwa kumeza, kwa hiyo ukimwona mtoto wa hivyo Kuna dawa ambayo Kwa kitaamu huiitwa methyl cellulose usaidia kurahisisha nevu za usoni na kumfanya mtoto kufumba macho na mdomo na kuanza kunyonya kawaida.

 

7. Mikwaruzo kwenye nevu za kuanzia kwenye bega mpaka kwenye mikono ambazo kwa kitaamu huiitwa branchial plexus.

Ni nevu ambazo pamoja na kuhathiri mabega na mikono vile vile uingiliana na uti wa mgongo katika nevu za mbavu ya nane na pia kuelekea kwenye shingo, ndio maana Kuna watoto wanaozaliwa wakiwa na shingo limelegea na pengine kushindwa kulisimamisha shingo kabisa, kwa hiyo watoto wa namna hiyo hawapaswi kufanyiwa mazoezi kiholela kwa lengo la kufanya shingo zao ziwe vizuri ila badala ya kumsaidia unaweza kuleta matatizo zaidi, kwa hiyo ni vizuri watu wa mifupa ndio wawafanyie mazoezi kwa kitaamu huiitwa watu wa physiotherapy,na wenyewe baada ya kutumia utrasound na x-ray na kuangalia mtiririko wa nevu ndipo waanze kazi mara moja.

 

8. Vile vile Kuna kupalalizi kwenye bega na sehemu ya juu ya mikono na sio kwenye vidole.

Kuna wakati mwingine kwa sababu ya michubuko kwenye mikono hali ambayo usababisha mtoto kupalalizi kwenye bega na pia kwenye mikono ya juu, kwa sababu nevu za sehemu ya juu ziliaribiwa wakati wa kuzaliwa inawezekana kabisa ni kwa sababu ya kutumia vyuma wakati wa kuzaliwa au mtoto kushindwa kutoa au kwa sababu ya mtoto kuvutwa sana na hatimaye kuharibika kwa nevu za mkono na bega, pia hali hii kwa kitaamu huiitwa erb;s palsy, kwa matibabu zaidi ni kuwaona wataalamu wa physiotherapy Ili waweze kumfanyia mtoto mazoezi kulingana na jinsi alivyoumia.

 

9.  Vile vile Kuna mikwaruzo ya kwenye nevu za vidole na sehemu ya chini kabisa ya vidole , ambapo unakuta mtoto Kwa upande wa bega na shingo yupo vizuri kabisa ila kwenye vidole na sehemu ya chini amepalalize na hawezi kufanya chochote au kushika chochote, hali hii utokea kwa sababu ya nevu za chini kwenye mikono zinakuwa zimehadhiriwa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa waangalifu punde mtoto anapozaliwa Ili kuweza kutambua kama Kuna tatizo lolote linalohusiana na kuharibika kwa nevu kwa sababu mtoto asipoangaliwa mapema anaweza kupata madhara zaidi.

 

 10. Kwa hiyo kazi ya kumfanya mtoto aonekane jinsi alivyo ni kazi ya wataalamu wa afya na pia ikiwa taratibu za kuzalisha mtoto ni nzuri na kugundua mapema hali ya hatari kwa mtoto kabla ya kuzaliwa ni vizuri kabisa kwa sababu ufanya matatizo mbalimbali yasitokee matatizo kama vile kupalalizi na kuondoa ulemavu kwa watoto. Na pengine tatizo linaweza kuwepo ila kama mtoto ameandaliwa mapema na kufanyia uchunguzi mapema mtoto anaweza kupona na kuendelea na hali yake ya Kawaida.

 

 

11. Pia kwa sababu ya kutokuwepo kwa elimu ya kutosha kwa jamii, Kuna tabia ya watu kutumia madawa ya mbalimbali au kuwafanyia mazoezi bila mpangilio hali inayowafanya kuleta madhara badala ya kusaidia , kwa hiyo tatizo hili likitokea ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na kuweza kuwapa ushauri unaopaswa Ili kuepuka kuleta madhara zaidi.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1064


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa macho.
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa macho, ugonjwa huu kwa kawaida una dalili kuu tano kadri ya maambukizi yanavyoongezeka na madhara yake kwa hiyo tunapaswa kujua dalili hizo Kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Huduma kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi msaada kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa, ni huduma anayopewa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa. Soma Zaidi...

Dalili zinazonesha kuungua kwa Mdomo (burning mouth)
Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuungua kinywani kwa mara kwa mara (kwa muda mrefu) bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea Soma Zaidi...

Ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal. Soma Zaidi...

Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Kuvimba ubongo (Encephalitis)
Post hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa ubongo ambao kitaalamu huitwa Encephalitis, Ni Maambukizi ya virusi ni sababu ya kawaida ya hali hiyo. Ugonjwa wa Kuvimba ubongo unaweza kusababisha dalili zinazofanana na Homa, kama vile Homa au Soma Zaidi...

Dalili, chanzo, sababu na vmambo hatari kuhusu kifua kikuu
Katika makala hii utajifunza kuhusu kifua kikuu, dalili zake, sababu zake, chanzo chake na mambo hatari kwa mgonjwa. Soma Zaidi...

Sababu za kuwepo kwa saratani ya inni.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za kuwepo kwa saratani ya ini, saratani hii imekuwa tishio kwa wengi ila ni vizuri kujua baadhi ya sababu ambazo uchangia sana kuwepo kwa tatizo hili la saratani ya inni. Soma Zaidi...

Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake
Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate na namna ya kutibu tatizo la kujaa kwa mate mdomoni Soma Zaidi...

Dalili za malaria
Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu kwa kitaalamu anaitwa Anopheles.na anasambazwa na mbu jike pale anapotafuta chakula hasa wakati akiwa na mimba. Mbu hawa hupenda kuishi kwenye mnyasi, madibwi haswa kwenye maji yaliyo simama. Soma Zaidi...

Naomb niulize ukiingiliana na mwanmke mweny ukimwi unaweza kuambikizwa na kusaambaaa kwa mda gan ndan ya mwil
Muda gani ukimwi huweza kuonekana mwilini ama kugundulika kama umeathirika, ni dalili zipo hujitokeza punde tu utakapoathirika Soma Zaidi...