Aina mbalimbali za michubuko

Aina mbalimbali za michubuko

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za michubuko,kwa Sababu michubuko utokea sehemu tofauti tofauti na pia Kuna aina mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Aina mbalimbali za michubuko.

1. Michubuko kwenye ngozi.

Hii ni aina mojawapo ya michubuko ambayo mara nyingi utokea kwenye ngozi ya juu ya mtoto hasa hasa ni kwa sababu ya kuzalisha watoto kwa kutumia vyuma, ambapo michubuko hii utokea kwenye ngozi ya juu ya kichwani , kwa kawaida uweza kugunduliwa na wahudumu wa afya mara tu mtoto akimaliza kuzaliwa, kwa hiyo ikitokea mtoto amevutwa na vyuma ni vizuri kabisa watoa huduma kuwa makini kukagua mtoto kama Kuna sehemu ambayo imeathirika na kuweza kutoa msaada . Pamoja na kazi za wahudumu na wazazi pia wanapaswa kuwa waangalifu katika kuona mabadiliko yoyote kwa mtoto na kutoa taarifa Ili mtoto aweze kuhudumiwa.

 

2. Kwa kawaida michubuko kwenye sehemu za ngozi ya juu ya mtoto mara nyingi haiitaji matibabu zaidi ila kusafishwa na kuiweka sehemu safi na kukausha usaidia sana kupona kwa ngozi hiyo ,vile vile na dawa za kupunguza maambukizi utolewa ambazo dawa hizo kwa kitaamu huiitwa antibiotics. Kwa kawaida mikwaruzo kwenye sehemu ya juu ya ngozi ya kichwa upona mapema na pia wazazi au ndugu hawapaswi kuweka dawa yoyote ambayo ni kinyume na dawa za hospital kwa sababu dawa nyingine uongeza matatizo zaidi kuliko kupona.

 

3. Vile vile aina nyingine ya michubuko kwenye ngozi ni kuvimba kwenye ngozi ya kichwani ambayo Kwa kitaamu huiitwa caput succedaneum,u uvimbe huu utokea kwa watoto hasa pale wanapopambana kutoka kwenye tumbo la mama na kuzaliwa ukutana na obstacles au ukutana na vitu ambavyo umsababishia hali ya kushindwa kutoka vizuri au kutoka kwa shida na kusababisha uvimbe kwenye sehemu ya kichwa , kwa kawaida uvimbe huu uonekana tu baada ya mtoto kuzaliwa na ndani ya siku tatu uvimbe huo uisha taratibu na hatimaye kutoweka kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kuwaelimisha wazazi na ndugu kutoweka vitu vyovyote kwenye uvimbe.

 

4. Michubuko kwenye sehemu za misuli.

Kuna wakati mwingine michubuko utokea kwenye sehemu za misuli au kwa kitaamu kwenye muscle ni kutokana na mishipa kupasuka au kukwaruzwa kwa ngozi hasa za kwenye misuli .kwa kawaida misuli inayoshambuliwa Zaid ni misuli ya kwenye shingo ambayo Kwa kitaamu huiitwa Torticollis muscle, hali hii utokea hasa pale mtoto anapozaliwa hasa kama ametanguliza bega au bega katika kuvutwa misuli ya shingoni inawezekana kulegea na kusababisha michubuko kwenye ngozi, kwa hiyo kama mtoto amezaliwa kwa shida ni vizuri kabisa kuangalia sehemu mbalimbali za misuli Ili kuweza kugundua tatizo lolote ambalo linaweza kujitokeza.

 

5. Mikwaruzo kwenye nevu.

Pia Kuna Kipindi ambapo mikwaruzo utokea kwenye nevu na kwa kiwango kikubwa nevu ambazo zinakuwa affected au zinazoathiriwa ni nevu za kwenye uso na pia na nevu za kwenye mabega, mikono,na kwenye vidole, ndio maana unaweza kumkuta mtoto amelemaa mkono,au bega na pia sehemu yote kuanzia kwenye bega na mikono kwa hiyo kama Kuna Neva yoyote ambayo imeathirika ni kuangalia kwa kutumia utrasound au x- ray kwa Sababu huwezi kuona kuaribika kwa Neva kwa macho ila unaweza kutumia dalili ila kufahamu ni Neva gani imeathirika ni kutumia utrasound au x-ray. Kwa hiyo tutaweza kuona nevu Moja badala ya nyingine kama ifuatavyo.

 

6. Nevu za kwenye uso.

Kuna wakati panakuwepo na kuharibika kwa nevu za kwenye uso kwa kitaamu huiitwa facial nevu.

 Kwa kawaida mtoto kama amezaliwa kwa kuvutwa na vyuma au wakati mwingine kuzaliwa kwa shida kwa sababu mbalimbali ambazo uchangia matatizo ya uzazi, Kuna mda mwingine mtoto uzaliwa akiwa na matatizo kwenye nevu za uso kwa sababu pengine zinakuwa zimevutwa hali ambayo usababisha mtoto kuzaliwa akiwa mdomo wazi, macho yanakuwa yamefunguka na mtoto hawezi kuyafumba, hali ambayo usababisha mtoto kushindwa kunyonya au pengine kabisa anashindwa kumeza, kwa hiyo ukimwona mtoto wa hivyo Kuna dawa ambayo Kwa kitaamu huiitwa methyl cellulose usaidia kurahisisha nevu za usoni na kumfanya mtoto kufumba macho na mdomo na kuanza kunyonya kawaida.

 

7. Mikwaruzo kwenye nevu za kuanzia kwenye bega mpaka kwenye mikono ambazo kwa kitaamu huiitwa branchial plexus.

Ni nevu ambazo pamoja na kuhathiri mabega na mikono vile vile uingiliana na uti wa mgongo katika nevu za mbavu ya nane na pia kuelekea kwenye shingo, ndio maana Kuna watoto wanaozaliwa wakiwa na shingo limelegea na pengine kushindwa kulisimamisha shingo kabisa, kwa hiyo watoto wa namna hiyo hawapaswi kufanyiwa mazoezi kiholela kwa lengo la kufanya shingo zao ziwe vizuri ila badala ya kumsaidia unaweza kuleta matatizo zaidi, kwa hiyo ni vizuri watu wa mifupa ndio wawafanyie mazoezi kwa kitaamu huiitwa watu wa physiotherapy,na wenyewe baada ya kutumia utrasound na x-ray na kuangalia mtiririko wa nevu ndipo waanze kazi mara moja.

 

8. Vile vile Kuna kupalalizi kwenye bega na sehemu ya juu ya mikono na sio kwenye vidole.

Kuna wakati mwingine kwa sababu ya michubuko kwenye mikono hali ambayo usababisha mtoto kupalalizi kwenye bega na pia kwenye mikono ya juu, kwa sababu nevu za sehemu ya juu ziliaribiwa wakati wa kuzaliwa inawezekana kabisa ni kwa sababu ya kutumia vyuma wakati wa kuzaliwa au mtoto kushindwa kutoa au kwa sababu ya mtoto kuvutwa sana na hatimaye kuharibika kwa nevu za mkono na bega, pia hali hii kwa kitaamu huiitwa erb;s palsy, kwa matibabu zaidi ni kuwaona wataalamu wa physiotherapy Ili waweze kumfanyia mtoto mazoezi kulingana na jinsi alivyoumia.

 

9.  Vile vile Kuna mikwaruzo ya kwenye nevu za vidole na sehemu ya chini kabisa ya vidole , ambapo unakuta mtoto Kwa upande wa bega na shingo yupo vizuri kabisa ila kwenye vidole na sehemu ya chini amepalalize na hawezi kufanya chochote au kushika chochote, hali hii utokea kwa sababu ya nevu za chini kwenye mikono zinakuwa zimehadhiriwa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa waangalifu punde mtoto anapozaliwa Ili kuweza kutambua kama Kuna tatizo lolote linalohusiana na kuharibika kwa nevu kwa sababu mtoto asipoangaliwa mapema anaweza kupata madhara zaidi.

 

 10. Kwa hiyo kazi ya kumfanya mtoto aonekane jinsi alivyo ni kazi ya wataalamu wa afya na pia ikiwa taratibu za kuzalisha mtoto ni nzuri na kugundua mapema hali ya hatari kwa mtoto kabla ya kuzaliwa ni vizuri kabisa kwa sababu ufanya matatizo mbalimbali yasitokee matatizo kama vile kupalalizi na kuondoa ulemavu kwa watoto. Na pengine tatizo linaweza kuwepo ila kama mtoto ameandaliwa mapema na kufanyia uchunguzi mapema mtoto anaweza kupona na kuendelea na hali yake ya Kawaida.

 

 

11. Pia kwa sababu ya kutokuwepo kwa elimu ya kutosha kwa jamii, Kuna tabia ya watu kutumia madawa ya mbalimbali au kuwafanyia mazoezi bila mpangilio hali inayowafanya kuleta madhara badala ya kusaidia , kwa hiyo tatizo hili likitokea ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na kuweza kuwapa ushauri unaopaswa Ili kuepuka kuleta madhara zaidi.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1686

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono

Kisonono ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria wa zinaa ambao wanaweza kuwaambukiza wanaume na wanawake. Kisonono mara nyingi huathiri urethra, puru au koo. Kwa wanawake, ugonjwa wa kisonono unaweza pia kuambukiza kizazi.

Soma Zaidi...
Virusi vinavyopelekea Kuharisha Sana na Kutapika Sana(norovirus)
Virusi vinavyopelekea Kuharisha Sana na Kutapika Sana(norovirus)

Maambukizi ya Norovirus yanaweza kusababisha kutapika sana na Kuhara. Virusi huambukiza sana na kwa kawaida huenea kupitia chakula au maji ambayo yamechafuliwa na kinyesi wakati wa kutayarisha. Unaweza pia kuambukizwa kwa kuwasiliana kwa karibu na mtu

Soma Zaidi...
Walio hatarini kupata gonorrhea (gonoria)
Walio hatarini kupata gonorrhea (gonoria)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu watu walio hatarini kupata gonorrhea gonoria

Soma Zaidi...
UGONJWA WA KASWENDE
UGONJWA WA KASWENDE

Kaswende ni maambukizi ya bakteria kawaida huenezwa kwa kujamiiana pia ugonjwa huu hujulikana kama syphilis. Ugonjwa huu huanza kama kidonda kisicho na maumivu kwa kawaida kwenye sehemu zako za siri, rektamu au mdomo

Soma Zaidi...
Njia za kutibu saratani
Njia za kutibu saratani

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za matibabu ya ugonjwa wa saratani,ni ugonjwa ambao unaweza kupona ikiwa umegundulika mapema katika hatua za mwanzo na kama ugonjwa huu umefikia hatua za mwisho Tiba yake huwa ni kupunguza makali ya ugonjwa.

Soma Zaidi...
Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini
Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini

Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wale ambao tayari wameshakuwa na tatizo la asidi mwilini, ni njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza tatizo hili au Mgonjwa anapoendelea kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia
Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia

Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia

Soma Zaidi...
Yaani minasumbuliwa na mgongo kuuma pia kuchoka mgongo na homa zisizo isha
Yaani minasumbuliwa na mgongo kuuma pia kuchoka mgongo na homa zisizo isha

Maumivu ya mgongo yanaweza kuwa ni dalili inayoonyesha tatizo fulani la kiafya ikiwemo magonjwa au majeraha.

Soma Zaidi...
Je inakuaje kama umempiga denda mtu mweny ukimwi ambaye anatumia daw za ARVs na una michubuko midogo mdomon ya kuungua na chai
Je inakuaje kama umempiga denda mtu mweny ukimwi ambaye anatumia daw za ARVs na una michubuko midogo mdomon ya kuungua na chai

Bila shaka umeshawahi kujiuliza kuwa je mate yanaambukiza HIV ama laa. Na kama hayaambukizi ni kwa sababu gani. Sio mate tu pia kuhusu jasho kama pia linaweza kuambukiza ukimwi ama HIV. Wapo pia wanajiuliza kuhusu mkojo kama unaweza kuambukizwa HIV. Kar

Soma Zaidi...