picha

DALILI ZA MIMBA BAADA YA TENDO LA NDOA

Je unahitaji kujuwa kama umepata ujauzito baada ya kufanya tendo la ndoa? hakika sio rahisi ila kama utakuwa makini utaweza.

DALILI ZA UJAUZITO BAADA YA TENDO LA NDOA

Je umeshawahi kujiuliza ni zipi zinaweza kuwa dalili za kwanza za ujauzito baada ya kushiriki tendo la ndoa? Hakika hili ni swali zuri na hapa niyakujuza majibu yake. Ukweli ni kuwa ni vigumu kuona dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa kama hutakuwa makini. Yes inawezekana kuzijuwa ila inahitaji uangalizi wa umakini kabisa. Mwanamke mmoja alishaniambia kuwa yeye ndani ya masaa matano baada ya kufanya tendo la ndoa anaweza kujuwa kama amebeba mimba ama laa. Nilipojaribu kumuuliza alikataa kabisa kunieleza.

 

Je naweza kuziona dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa?

Kabla ya kulijibu swahi hili inapasa kujuwa mabadiliko ya mwili wako kabla ya ujauzito ama kabla ya kushiriki tendo la ndoa. Kwanza zingatia mabo haya kabla ya kushiriki tendo la ndoa:-

  1. Jeoto la mwili wako. Hakikisha unatambuwa vyema kama mwili wako joto lake lipo kiasi gani. Na hakikisha unaweza kutofautisha kati ya joto la homa na joto la kawaida.
  2. Zingatia majimaji ya kwenye uke wako. Zingatia kama uke wako upo katika majimaji ama upo mkavu. Pia angalia rangi za mashavu ya uke.
  3. Zingatia tarehe zako. Kabla ya kushiriki tebdo la ndoa hakikisha tarehe zako unazifahamu vyema, pamoja na siku zako za hatari ni lini.

 

Je nitazijuaje sasa hizo dalili baada ya kuzingatia mambo hayo?

Kujuwa kama umebeba mimba ama laa inaweza kuchukuwa hata wiki moja kuona mabadiliko kwenye mwili wako, mabadiliko haya yataweza kukuambia kwamba huwenda umebebe mimba. Ila pia kuna baadhi ya waanwake wanaweza kuyana mabadiliko hayo mapema kabisa. Ila tambuwa kuwa mabadiliko hayo yote yanaweza kuwa ni vyanzo vya sababu zingine na si ujauzito.

 

Mabadiliko hayo ni kama:-

  1. Kuongezeka kwa joto la mwili. Kama ulizingatia vyema joto la mwili wako wakati ukiwa katika siku za hatari linakuwa kubwa kulinganisha ziku za nyuma. Baada ya kushiriki tendo la ndoa angalia je joto litapunguwa ama kuongezeka. Kama litapunguwa baada ya kupita siku za hatari huwenda bado hujabeba ujauzito. Lakini endapo utaona joto halipungui na huwenda likaongezeka hii huonyesha kuwa una mabadiliko kwenye mwili wako ambayo huwenda ni ujauzito. Jifunze pia kutofautisha kati ya homa na joto la kawaida.

 

  1. Majimaji kwenye uke na njia ya kuelekea kwenye tumbo la mimba. Kikawaida wakati wa siku za hatari kiasi cha majimaji kwenye uke huongezeka, hii ni kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kuweza kubeba mimba. Zinapopita siku za hatari majimaji hupunguwa na hatimaye kurudi hali ya kawaida ya ukavu. Sasa endapo majimaji hayatapunguwa na vinginevyo yakawa yanabadilika na kuwa mazito kuliko hapo mwanzo hii huashiria huwenda amebeba ujauzito.

 

  1. Ok sasa zingatia ziku zako za hatari.kama ulishiriki tendo la ndoa katika siku hatari kisha ukaanza kuona mabadiliko kama kutokwa na damu chache iliyo tofauti na hedhi, ama maumivu ya tumbo ya ghafla, ama kichwa kuhisi chepesi mabadiliko kama haya na mengineyo huashiria ujauzito.

 

  1. Mabadiliko ya rangi kwenye chuchu na mashavu ya uke yanaweza kuwa n dalili ya ujauzito. Matiti kuuma ama kuwa magumu hii ni katika dalili wanayoiona wengi katka wanawake. Mashavu ya uke hubadilika kuwa na uweuzi ama uwekundu kutokana na mishipa ya damu kuja juu na kupitisha damu kwa wingi maeneo ya chini ili kuandaa ukuaji wa mimba.

 

NI ZIPI DALILI ZA MWANZO ZA MIMBA KUANZIA SIKU YA KWANZA?

Yes kama tulivyoona hapo juu, mabadiliko hayo sio rahisi kutokea kutoka siku ya kwanza, ila yes mwili huanza kuonyehsa mabadiliko ya ndani punde tu mimba inapoingia, lakini kwa mwanamke kuhusi mabadiliko hayo inaweza kuchukuwa muda. Sasa hapa tutaziona kwa ufupi orodha ya dalili za mimba changa:

  1. Kuingezeka kwa joto la mwili
  2. Kuongezeka kwa maimaji ya ukeni
  3. Kutoka na damu kidogo nyepesi
  4. Maumivu ya matiti na kujaa ama kuwa magmu
  5. Mabadiliko ya rangi kwenye matiti na mashavu ya uke
  6. Kutoziona siku zako
  7. Kichwa kuwa chepesi
  8. Maumivu ya kichwa, tumbo na kizunguzungu
  9. Kichefuchefu na kutapika
  10. Kukojoa mara kwa mara
  11. Maumivu ya tumbo

 

JE KAMA SIO MIMBA NINI KITAKUWA.

Si kila dalili za mimba zinamaanisha ni kweli una ujauzito. Unaweza kuona dalili za mimba lakini ukawa huna. Sababu zinazoweza kupelekea hali hii ni kama:-

  1. Mabadiliko ya homoni
  2. Mashambulizi ya bakteria na virusi kwenye ufumo wa mkojo na mfumo wa uzazi
  3. Vyakula
  4. Mazingira
  5. Maradhi mengineyo yahusuyo mfumo wa uzazi

Soma zaidi kuhusu ujauzito

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 10190

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

IJUE HOMA YA CHIKUNGUNYA (CHIKV) DALILI ZAKE, TIBA YAKE, CHANJO YAKE, NA MBU ANAYESAMBAZA HOMA HII

Haya ni maradhi ambayo husambazwa kutoka kwa mtu kwenda kwa mtu kwa kupitia mbu.

Soma Zaidi...
Kichwa kuuma upande mmoja (Migraine): Vyakula vya kuepuka.

Migraine (kichwa kuuma upande mmoja kwa namna ya kugonga au kudunda) ni zaidi ya maumivu ya kichwa ya kawaida; ni hali ya kineva inayoweza kuambatana na kichefuchefu, kutapika, na usikivu mkali wa mwanga au sauti. Ingawa visababishi ni vingi, tafiti zinaonyesha kuwa vyakula fulani ni vichochezi (triggers) vikuu vya mashambulizi haya kwa watu wengi. Makala haya yanakupa mwongozo wa vyakula vya kuepuka ili kupunguza mzunguko na ukali wa maumivu ya migraine.

Soma Zaidi...
Kujitenga na jamii: Je, ni ishara ya unyogovu?

​Katika ulimwengu wa kisasa uliounganishwa kidijitali, kitendawili cha upweke katikati ya umati kimezidi kuwa kikubwa. Makala haya yanachunguza uhusiano wa kina kati ya tabia ya kujitenga na jamii (social withdrawal) na afya ya akili, hususan unyogovu. Tunachambua dalili, sababu za kisaikolojia, na tofauti kati ya hitaji la muda mfupi la upweke na ugonjwa wa unyogovu wa kitabibu, huku tukitoa mwongozo wa hatua za kuchukua ili kurejesha ustawi wa kijamii

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa fungusi uken

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa fungusi uken, ni ugonjwa unaoshambulia sana sehemu za Siri ambao huwa na dalili kama zifuatazo.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu wakati wa kujamiiana

​Maumivu wakati wa kujamiiana (kitaalamu dyspareunia) ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi, ingawa mara nyingi halizungumzwi wazi kutokana na unyanyapaa au aibu. Maumivu haya yanaweza kusababishwa na sababu za kisaikolojia, matatizo ya kimwili, au mabadiliko ya kihomoni. Makala haya yanachambua vyanzo vikuu vya maumivu hayo na kutoa ukweli wa kisayansi (Fact Check) ili kukusaidia kujua hatua za kuchukua.

Soma Zaidi...