image

Aina za fangasi

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya aina za fangasi

AINA ZA FANGASI

Fangasi wamegawanyika katika makundi mengi. Na wamekuwa wakisababisha maradhi mblimbali na katika sehemu mbalimbali za miili yetu. Hapa nitakutajia aina za fangasi hawa kama ifuatavyo:-

 

1.Fangasi wa kwenye kucha.

Hawa ni fangasi ambao wanashambulia sana kwenye kucha za vidole vya mikonobna miguu. Jina la kitaalamu la fangasi hawa ni onychomycosis. Wanakifanya kidole kivimbe, na kupoteza rangi yake ya asili. Kidole kinaweza kuwa na mipasuko. Fangasi hawa wanaathiri zaidi kwenye vidole vya miguu kuliko vya mikono. Fangasi hawa hawana maumivu lamda kama wataathiri zaidi.

 

 

Dalili za fangasi hawa:-

?Kucha kuwa na utandu mweupe au njano

?Kidole kuwa kigumu na kuvimba

?Kupasuka kwa vidole

 

Fangasi hawa tunaweza kuwapata kwenye mazingira yetu, wanaingia kupitia mipasuko kwenye miguu ama kwa namna nyingine. Kila mtu anaweza kupata fangasi hawa ila kuna watu wapo hatarini sana yaani ni rahisi kupata fangasi hawa.

 

Watu walio hatari kupata fangasi hawa

Watu hawa ni kama:-

?Mtu mwenye majeraha kwenye kucha ama aliyefanyiwa upasuaji

?Watu wenye kisukari

?Watu wenye mfumo wa kinga ulio dhaifu

?Watu wenye matatizo katika mfumo wa damu

?Watu wenye minyoo kwenye miguu.

 

Njia za kuepuka fangasi hawa:

1.Weka vidole vyako safi na vikavu muda wote

2.Kata kucha zako ziwe fupi na usiweke safi muda wote

3.Usitembee bila ya viatu kwenye maeneo yasiyo salama.

4.Usishiriki kifaa cha kukatia kucha na watu wengine

 

2.Fangasi wa mapunye;

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis. Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-

?Kuwasha kwa ngozi na maumivu wakati mwingine

?Kuwepo kwa mapele ama ukurutu uliotengeneza umbo la duara

?Ngoz kuwa nyekundu, kupasuka ama kuwa kavu

?Kukatika ama kunyonyoka kwa nywele kwenye sehemu iliyo athirika

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-

 

Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.

 

Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.

 

Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.

 

Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.

 

Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.

 

Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa

Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.

?Watu wenye mfumo wa kinga dhaifu

?Watu wanotumia changia sehemu moja ya kuwekea nguo

?Watu wanaofanya shughuli ambazo hugusana gusana kwa mfano wanaofanya miereka.

?Watu wanaovaa nguo za kubana sana

?Watu wanaogusana gusana na wanyama wenye mapunye.

 

Namna ya kujilinda na mapunye

1.Weka ngozi yako katika hali ya usafi

2.Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako

3.Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi

4.Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi

5.Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku

6.Usichangie nguo zako na mtu mwingine

7.Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.

 

3.Fangasi aina ya Candidiasis

Huu ni ugonjwa wa fangasi wanaosababishwa na mashambulizi ya fangani aia ya yeast waitwao candida. Miongoni mwa fangasi maarufu sana katika kudi hili ni wale wanaoitwa candida albican. Fangasi hawa wanaishi juu ya ngozi, na ndani ya mwili katika maeneo kama mdomo, koo, tumbo, na katika uke. Wanaeza kuishi maeneo haya bila ya kusababisha madhara yeyote.

 

Candida wanaweza kusababisha madhara endapo tu watakuwa wengi sana tofauti na kawaida, ama kama wakiingia ndani zaidi kama kweny mfumo wa damu, ama kwenye organ za ndani kama figo, moyo ama ubongo. Na wapo baadhi ya fangasi hawa ni sugu sana kwa madawa.

 

Fangasi hawa ambao hupatikana kwenye mdomo kitaalamu hufahamika kama thrush au oropharyngeal candidiasis. Na wale ambao hukaa ukeni hutambulika kama yeast infection. Pindi wakiingia kwenye mfumo wa damu ama wakiathiri organ za ndani kama figo, koyo na ubongo hutambulika kama invasive candidiasis.

 

1.Fangasi hawa wa kwenye mdomo watambulikao kama thrush ama oropharyngeal candidiasis wanaweza kuishi kwenye koo na tundu zima la koo kuelekea kwenye tumbo na hawa wanajulikana kama esophageal candidiasis ama candida esophagitis. Fangasi hawa ni maarufu sana kwa watu wanaoishi na HIV ana UKIMWI.

 

Dalili za fangasi hawa

?Kuwa na madoa meupe kwenye sehemu ya ndani ya shavu, ulimi, sehemu ya juu ya mdomo, na koo.

?Unahisi kama kuna pambai kwenye mdomo

?Kupetea kwa ladha ya unachokila

?Maumivu wakati wa kula ama kumeza

?Kupasuka na kuwa wekundu kwenye kona za mdomo

 

Walio hatarini kupata fangasi hawa:

Fangasi hawa si kawaida sana kuwapata watu wenye afya madhubuti. Ijapokuwa wapo watu ambao wapo hatarini sana kupata fangasi hawa kama watoto chini ya umri wa mwaka mmoja, na watu wenye matatizo ya kiafya kam wenye:-

?Watu wanaotumia meno bandia

?Watu wenye kisukari

?Watu wenye saratani

?Watu wenye HIV ama UKIMWI

?Watu wanaotumia dawa amazo zinakausha mdomo

?Watu wanaovuta sigara.

?Watu wanaotumia dawa za kupulizia za pumu

 

Njia ya kupambana na fangasi hawa:

Wengi wanaopata fangasi hawa ni wale ambao mfumo wao wa kinga umeathirika hivyo miili yao haiwezi kupambana vyema na mashambulizi. Hivyo kupambana na fangasi hawa hakikisha unaweka mwili wako katika hali njema ya kiafya. Muone daktari akuelekeze namna ya kuboresha afya yako. Pia piga mswaki kila unapotumia dawa ya kupulizia ya pumu. Wacha kuvuta sigara.

 

2.Fangasi wa kwenye uke.

Fangasi hawa kitaalamu wanafahamika kama vagina yeast infection na majina mengine ya kitaalamu ni kama vagina candidiasis, u vulvovaginal candidiasis au candidal vaginitis. Majina yete haya yanalenga vagina yaani uke.

 

Dalili za fangasi hawa wa ukeni

?Uke kuwasha na kuweka kama makovu

?Maumivu wakati wa tendo la ndoa

?Paumivu wakati wa kukojoa

?Kutokwa na majimaji yasiyo ya kawaida kwenye uke.

 

Wakati mwingine fangasi hawa wa kwenye uke wanakuwa hatari sana na kusababisha mipasuko kwenye ukuta wa uke, kuvimba na kuwa kwekundu. Hali hizi humfanya mwanamke kukosa hali ya kujiamini.

 

 

 

Walio hatarini zaidi

Fangasi hawa ni kawaida lakini kuna watu ambao wapo hatarini zaidi kupata fangasi hawa. Tafiti nyingi bado zinafanyika kuweza kugundua kwa nini watu flani wapo hatarini zaidi kuapa fangasi hawa. Watu hawa ni:-

?Wajawazito

?Wanaotumia njia za uzazi wa mpango za homoni

?Watu wenye kisukari

?Watu wenye mfumo dhaifu wa kinga kama wenye HIV

?Wtu wanaotumia antibiotics

 

Kupambana na fangasi hawa

1.Vaa nguo za ndani zinazotokana na pamba

2.Usivae nguo za kubana

3.Vaa nguo zilizo kavu

4.Zungumza na daktari kuhusu matumizi ya antibiotics kama zinakuletea madhara

 

3.Fangasi watambulikao kama invasive candidiasis.

Hawa huweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenda maeneo mengine nyeti sana ya mwili. Kwa mfano kwenye figo, moyo na ubongo machi, mifupa na viungia. Fangasi hawa wakiingia maeneo haya wanakuwa ni hatari sana kwa afya ha mtu.

 

Dalili za invasive candidiasis

Watu wenye fangasi hawa wanaonesha dalili ambao ni za maradhi mengine, hivyo kufanya vigumu kugundulika. Ijapokuwa kuna dalili ambazo ni za kawaida kama vile, kuhisi baridi, homa ambapo mgonjwa hawezi pata nafuu hata akitumia dawa.

 

Watu walio hatarini

?Watu ambao wapo ICU kwa muda mrefu

?Watu wenye mfumo dhaifu wa kinga

?Watu waliofanyiwa upasuaji haswa haswa uliohusisha tumbo

?Watu ambao wametumia antibiotics kwa wingi hivi karibuni

?Watu waliotumia chakula kwa kutumia mirija

?Watu wenye matatizo kwenye figo au hemodialysis

?Watu wenye kisukari

 

5.Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis. Fangasi hawa wanaishi kwenye mazingira yenye majimaji haswahaswa kwenye udongo ama kwenye maozea kama ya miti au majani. Fangasi hawa tunaweza kuwapata kwa kuvuta hewa ambayo imekusanya fangasi hawa.

 

Dalili za fangasibhawa:-

1.Homa na maumivu vya kichwa

2.Kukohoa

3.Kutokwa na jasho usiku

4.Maumivu ya mivuli na viungio

5.Kupoteza uzito

6.Maumivu ya kifua

7.Uchovu wa hali ya juu sana

 

Kwa ufupi zipo aina nyingi sana za fangasi, na yapo maradhi mengi sana yasababishwayo na fangasi. Nadhani hapo juu nimekutajia aina maarufu za mangasi ana mago njwa yako. Pia nimekutajia baadhi ya njia za kutumia ili kupambana na fangasi hoa. Sasa nakwenda kukuorodheshea maradhi 7 yatokanayo na fangasi:-





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2215


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Hatua za kupambana na ugonjwa wa UTI
Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu. Soma Zaidi...

Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia
Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia Soma Zaidi...

Samaani nilikuwa nauriza ninasumburiwa na fanga ya mdomoni naomba ushauri
Fangasi mdomoni wanaweza kuwa tatizo endapo hawatatibiwa mapema. Wanaweza kuongeza majeraha kwenye kinywa. Soma Zaidi...

Mambo ambayo yanaweza kuongeza hatari ya Ugonjwa wa Homa ya ini yenye sumu.
Posti hii inazungumzia zaidi kuhusiana na Homa ya ini yenye sumu ni kuvimba kwa ini lako kutokana na kuguswa na vitu fulani ambavyo umeathiriwa navyo. Homa ya ini yenye sumu inaweza kusababishwa na pombe, kemikali, madawa ya kulevya au virutubisho vya lis Soma Zaidi...

Sababu za Maambukizi kwenye mifupa.
Post hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ni Maambukizi ambayo hutokea kwenye mifupa kwa sababu mbalimbali ambazo usababisha ugonjwa huu. Soma Zaidi...

Fangasi wa kwenye uke.
Fangasi hawa kitaalamu wanafahamika kama vagina yeast infection na majina mengine ya kitaalamu ni kama vagina candidiasis, u vulvovaginal candidiasis au candidal vaginitis. Soma Zaidi...

FAIDA ZA KIAFYA ZA MINYOO: kupunguza aleji, kuchochea utungaji wa mimba, kupona kwa vidonda vya ndani
FAIDA ZA KIAFYA ZA MINYOO Wakati mwingine kuwa na aina flani ya minyoo kunaweza kuwa na faida katika afya. Soma Zaidi...

YAJUE MARADHI YA KISUKARI
Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari Soma Zaidi...

Fahamu Ugonjwa wa mshtuko wa sumu.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria. Soma Zaidi...

Sababu zinazopelekea maumivu ya Matiti.
 Maumivu ya matiti hutokea zaidi kwa watu ambao hawajamaliza hedhi, ingawa yanaweza kutokea baada ya kukoma hedhi.  Soma Zaidi...

Ni bakteria gani husababisha ugonjwa wa pumu
Post hii inakwenda kujibu swali linalosema je ni bakteria aina gani husababisha igonjwa wa pumu. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.
Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa vipele kwenye midomo na sehemu za siri .Ni ugonjwa ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster Soma Zaidi...